Kakke
JF-Expert Member
- Dec 4, 2010
- 1,883
- 1,482
[h=1][/h]Written by amini // 19/01/2012 // Habari // No comments
na Mauwa Mohammed, Zanzibar
WAJUMBE wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar wamehoji hatua ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupeleka maombi Umoja wa Mataifa (UN) kuomba kuongezewa ukubwa wa eneo la bahari.
Kauli hiyo imewasilishwa na Mwakilishi wa Mji Mkongwe (CUF), Ismail Jussa Ladhu na kutaka kutoa hoja ili baraza hilo lijadili katika kikao kinachoendelea mjini Zanzibar.
Alisema hatua hiyo ya Serikali ya Muungano ni nzito inayogusa wananchi kwa hiyo, ilitakiwa kuangaliwa vema kwani waathirika wakuu huenda wakawa ni Wazanzibari.
Jussa alifahamisha kuwa kwa mujibu wa taarifa iliyotoka ndani ya vyombo vya habari ombi hilo linawasilishwa leo katika ofisi za Umoja huo New York, Marekani.
Spika wa Baraza la Wawakilishi, Pandu Ameir Kificho, alitumia busara kubwa na kuwataka wajumbe wasubiri na kuiagiza Serikali kulifuatilia suala hilo kikamilifu ili wananchi wa Zanzibar wajue lengo la hatua hiyo kwa Tanzania.
Alitoa agizo kwa serikali kutoa maelezo juu ya upande mmoja wa Muungano kupeleka maombi hayo kwa Umoja wa Mataifa bila kuushirikisha upande wa pili.
Aliitaka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kufuatilia jambo hilo kabla ya maamuzi ya Umoja wa Mataifa hayajatolewa kuhusiana na suala hilo.
Naye Mwakilishi wa Kuteuliwa, Ali Mzee Ali, alisema kuwa ingekuwa jambo la maana suala kama hilo likapigiwa kura kutokana na umuhimu wake kitaifa.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, anayedaiwa kusimamia na kuwasilisha hoja hiyo UN, hakuweza kupatikana kutoa maelezo ya jambo hilo.
Jitihada za Tanzania Daima kuonana na Tibaijuka ofisini kwake zilikwama baada ya kupewa maelezo kuwa waziri huyo alikuwa nje ya ofisi kwa shughuli za kikazi na kwamba asingeweza kurudi. Aidha, simu yake ya mkononi iliita mara nyingi bila kupokewa.
chanzo Tanzania Daima
WAJUMBE wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar wamehoji hatua ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupeleka maombi Umoja wa Mataifa (UN) kuomba kuongezewa ukubwa wa eneo la bahari.
Kauli hiyo imewasilishwa na Mwakilishi wa Mji Mkongwe (CUF), Ismail Jussa Ladhu na kutaka kutoa hoja ili baraza hilo lijadili katika kikao kinachoendelea mjini Zanzibar.
Alisema hatua hiyo ya Serikali ya Muungano ni nzito inayogusa wananchi kwa hiyo, ilitakiwa kuangaliwa vema kwani waathirika wakuu huenda wakawa ni Wazanzibari.
Jussa alifahamisha kuwa kwa mujibu wa taarifa iliyotoka ndani ya vyombo vya habari ombi hilo linawasilishwa leo katika ofisi za Umoja huo New York, Marekani.
Spika wa Baraza la Wawakilishi, Pandu Ameir Kificho, alitumia busara kubwa na kuwataka wajumbe wasubiri na kuiagiza Serikali kulifuatilia suala hilo kikamilifu ili wananchi wa Zanzibar wajue lengo la hatua hiyo kwa Tanzania.
Alitoa agizo kwa serikali kutoa maelezo juu ya upande mmoja wa Muungano kupeleka maombi hayo kwa Umoja wa Mataifa bila kuushirikisha upande wa pili.
Aliitaka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kufuatilia jambo hilo kabla ya maamuzi ya Umoja wa Mataifa hayajatolewa kuhusiana na suala hilo.
Naye Mwakilishi wa Kuteuliwa, Ali Mzee Ali, alisema kuwa ingekuwa jambo la maana suala kama hilo likapigiwa kura kutokana na umuhimu wake kitaifa.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, anayedaiwa kusimamia na kuwasilisha hoja hiyo UN, hakuweza kupatikana kutoa maelezo ya jambo hilo.
Jitihada za Tanzania Daima kuonana na Tibaijuka ofisini kwake zilikwama baada ya kupewa maelezo kuwa waziri huyo alikuwa nje ya ofisi kwa shughuli za kikazi na kwamba asingeweza kurudi. Aidha, simu yake ya mkononi iliita mara nyingi bila kupokewa.
chanzo Tanzania Daima