Mpaka wa bahari watikisa Muungano

Status
Not open for further replies.

Kakke

JF-Expert Member
Dec 4, 2010
1,883
1,482
[h=1][/h]Written by amini // 19/01/2012 // Habari // No comments

DSC047671-564x272.jpg
na Mauwa Mohammed, Zanzibar
WAJUMBE wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar wamehoji hatua ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupeleka maombi Umoja wa Mataifa (UN) kuomba kuongezewa ukubwa wa eneo la bahari.
Kauli hiyo imewasilishwa na Mwakilishi wa Mji Mkongwe (CUF), Ismail Jussa Ladhu na kutaka kutoa hoja ili baraza hilo lijadili katika kikao kinachoendelea mjini Zanzibar.
Alisema hatua hiyo ya Serikali ya Muungano ni nzito inayogusa wananchi kwa hiyo, ilitakiwa kuangaliwa vema kwani waathirika wakuu huenda wakawa ni Wazanzibari.
Jussa alifahamisha kuwa kwa mujibu wa taarifa iliyotoka ndani ya vyombo vya habari ombi hilo linawasilishwa leo katika ofisi za Umoja huo New York, Marekani.
Spika wa Baraza la Wawakilishi, Pandu Ameir Kificho, alitumia busara kubwa na kuwataka wajumbe wasubiri na kuiagiza Serikali kulifuatilia suala hilo kikamilifu ili wananchi wa Zanzibar wajue lengo la hatua hiyo kwa Tanzania.
Alitoa agizo kwa serikali kutoa maelezo juu ya upande mmoja wa Muungano kupeleka maombi hayo kwa Umoja wa Mataifa bila kuushirikisha upande wa pili.
Aliitaka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kufuatilia jambo hilo kabla ya maamuzi ya Umoja wa Mataifa hayajatolewa kuhusiana na suala hilo.
Naye Mwakilishi wa Kuteuliwa, Ali Mzee Ali, alisema kuwa ingekuwa jambo la maana suala kama hilo likapigiwa kura kutokana na umuhimu wake kitaifa.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, anayedaiwa kusimamia na kuwasilisha hoja hiyo UN, hakuweza kupatikana kutoa maelezo ya jambo hilo.
Jitihada za Tanzania Daima kuonana na Tibaijuka ofisini kwake zilikwama baada ya kupewa maelezo kuwa waziri huyo alikuwa nje ya ofisi kwa shughuli za kikazi na kwamba asingeweza kurudi. Aidha, simu yake ya mkononi iliita mara nyingi bila kupokewa.
chanzo Tanzania Daima
 
We jusa acha kiherehere
usijifanye unajua kila kitu, kwanza
we si mzawa.
 
Written by amini // 19/01/2012 // Habari // No comments

DSC047671-564x272.jpg
na Mauwa Mohammed, Zanzibar
WAJUMBE wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar wamehoji hatua ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupeleka maombi Umoja wa Mataifa (UN) kuomba kuongezewa ukubwa wa eneo la bahari.
Kauli hiyo imewasilishwa na Mwakilishi wa Mji Mkongwe (CUF), Ismail Jussa Ladhu na kutaka kutoa hoja ili baraza hilo lijadili katika kikao kinachoendelea mjini Zanzibar.
Alisema hatua hiyo ya Serikali ya Muungano ni nzito inayogusa wananchi kwa hiyo, ilitakiwa kuangaliwa vema kwani waathirika wakuu huenda wakawa ni Wazanzibari.
Jussa alifahamisha kuwa kwa mujibu wa taarifa iliyotoka ndani ya vyombo vya habari ombi hilo linawasilishwa leo katika ofisi za Umoja huo New York, Marekani.
Spika wa Baraza la Wawakilishi, Pandu Ameir Kificho, alitumia busara kubwa na kuwataka wajumbe wasubiri na kuiagiza Serikali kulifuatilia suala hilo kikamilifu ili wananchi wa Zanzibar wajue lengo la hatua hiyo kwa Tanzania.
Alitoa agizo kwa serikali kutoa maelezo juu ya upande mmoja wa Muungano kupeleka maombi hayo kwa Umoja wa Mataifa bila kuushirikisha upande wa pili.
Aliitaka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kufuatilia jambo hilo kabla ya maamuzi ya Umoja wa Mataifa hayajatolewa kuhusiana na suala hilo.
Naye Mwakilishi wa Kuteuliwa, Ali Mzee Ali, alisema kuwa ingekuwa jambo la maana suala kama hilo likapigiwa kura kutokana na umuhimu wake kitaifa.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, anayedaiwa kusimamia na kuwasilisha hoja hiyo UN, hakuweza kupatikana kutoa maelezo ya jambo hilo.
Jitihada za Tanzania Daima kuonana na Tibaijuka ofisini kwake zilikwama baada ya kupewa maelezo kuwa waziri huyo alikuwa nje ya ofisi kwa shughuli za kikazi na kwamba asingeweza kurudi. Aidha, simu yake ya mkononi iliita mara nyingi bila kupokewa.
chanzo Tanzania Daima


Hongera sana Ismail Jussa.

Kwani huo ni uvunjifu wa Katiba zote mbili ya Muungano na ile ya Znz. Ni lazima kieleweke hapo na kumjuza Prof Tibaijuka kuwa Znz ni nchi anapaswa kuiheshimu kwa dhati kabisa.

Hongera sana mwakilishi wangu.
 
Ndo maana kama katiba mpya itachezewa basi tujue kuwa CCM na CUF waweza kufarakana wakati wowote huko zanzibar na majibu yake yakamwangusha vibaya kikwete ndani na nje
 
Kwani wakati wanapeleka hilo ombi la kuongeza eneo la bahari kulikuwa hakuna mawasiliano na SMZ? Mbona jambo hili linaleta utata. Mi nilifikiri SMZ ingefurahia jambo hilo?
 
ukweli uelezwe kwa kujibu swali la kwanini wanataka kufanya hivyo? huenda kunasababu za msingi kitaifa, anaye jua sababu naomba anijuze ndo nisapoti au nikanushe.
 
Ndugu Wazanzibari, jambo hili si la waziri wa ardhi peke yake bali limepata baraka za baraza la mawaziri ambalo miongoni mwa wajumbe wake ni Rais wa Zanzibar, Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye ni Mzanzibari na wazanzibari wengine ambao ni mawaziri karika SMT. Sasa mnataka mshirikishwe namna gani? Jussa kama hujui haya hufai kuwa mwakilishi!
 
Hatutuna sababu ya kukubaliana katika hilo, kwani hata tukiamua sasa muungano ukavunjika, Zanzibar haiwezi kutambulia kama nchi mpaka sisi tukubali, kwa umbali ambao Zanzibar ipo, Sheria za Kimataifa za mipaka ya bahari haiitambui zanznibari kama nchi.
Hivyo achaneni na ndoto za mchana, hilo lingewezekana ingeanza Taiwan kutambuliwa kama nchi.
Sema ujinga wa viongozi wetu ndiyo unawapa kichwa na kuwajazeni ujinga, ila endeleeni kulalamika bila ya kuona, mwisho haitukuwa mzuri kwenu.
 
Haya tusubiri tuone. Inashangaza kuona mambo hayaendi au kuna upinzani kwenye mambo ambayo ni ya nchi moja japo serikali mbili. Nilidhani faida itakuwa kwa ajili ya watz wote kumbe kuna wengine ambao hawahusiki. Basi itakuwa shida na maendeleo yetu yatakuwa yanasuasua kama sisi wenyewe tutakuwa tunalumbana kwenye vitu ambavyo tungeweza tu tukaelezana mezani. Mungu ibariki Tanzania!
 
Hongera sana Ismail Jussa.

Kwani huo ni uvunjifu wa Katiba zote mbili ya Muungano na ile ya Znz. Ni lazima kieleweke hapo na kumjuza Prof Tibaijuka kuwa Znz ni nchi anapaswa kuiheshimu kwa dhati kabisa.

Hongera sana mwakilishi wangu.

Jussa hajui,na hajui anaozungumza nao-hata wananchi wake wengi hawana uwezo wa kupambanua maswala kama haya
somam hapa,upate kuelewa
https://www.jamiiforums.com/hoja-nzito/209835-kwanini-jussa-anawajaza-ujinga-wazanzibari-wenzie.html


Kwani wakati wanapeleka hilo ombi la kuongeza eneo la bahari kulikuwa hakuna mawasiliano na SMZ? Mbona jambo hili linaleta utata. Mi nilifikiri SMZ ingefurahia jambo hilo?
hawana mawasilaino pale serikali ya tz inapokuwa inafanya mambo ya watanganyika,ambao ndo wengi,ni kama vile viongozi wameshuka kidogo wakaona wao ni watanganyika-bora wafanye maswala ya taifa lao.
hii ikipita swala la mafuta halitapigiwa kelele na wazanzibar,maana lazima yawe ya share au ya tanganyika
soma hapa
https://www.jamiiforums.com/hoja-nzito/209835-kwanini-jussa-anawajaza-ujinga-wazanzibari-wenzie.html
 
Hongera sana Ismail Jussa.

Kwani huo ni uvunjifu wa Katiba zote mbili ya Muungano na ile ya Znz. Ni lazima kieleweke hapo na kumjuza Prof Tibaijuka kuwa Znz ni nchi anapaswa kuiheshimu kwa dhati kabisa.

Hongera sana mwakilishi wangu.


Kaka wewe si ulisema sio Mtanzania.......na ukaniambia kuwa uliwahi kuishi tu kisha ukarudi kwenu sasa Jusa mwakilishi wako kivipi? Au unalengo la kurudi baada ya zenj kujitenga? Mie huwa sikuelewi ndugu wewe ni Mzenj? Mwarabu wa Oman....au wewe wa wapi hasa? Kuna athread moja ulitumia maneno ya kujiondoa kuwa mtz uliposema taifa lenu....nchi yenu......wewe ukajiondoa sasa unawakilishwa vipi na Jussa. Kama wewe mzamiaji then acha usokorokwinyo
 
Spika wa Baraza la Wawakilishi, Pandu Ameir Kificho, alitumia busara kubwa na kuwataka wajumbe wasubiri na kuiagiza Serikali kulifuatilia suala hilo kikamilifu ili wananchi wa Zanzibar wajue lengo la hatua hiyo kwa Tanzania.
Alitoa agizo kwa serikali kutoa maelezo juu ya upande mmoja wa Muungano kupeleka maombi hayo kwa Umoja wa Mataifa bila kuushirikisha upande wa pili.
Aliitaka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kufuatilia jambo hilo kabla ya maamuzi ya Umoja wa Mataifa hayajatolewa kuhusiana na suala hilo.

Kwa haraka sana nilifikiri Watanzania wa Wazanzibar wangefurahia hoja ya kuomba kuongezewa eneo jambo ambalo lingewaweza pia hata wao (Wanzania waishio zanzibar )kujitanua kiuchumi katika shughuli za baharini.

Halafu hii kauli ya "Upande mmoja wa Muungano" sijaielewa. Hawa watanzania wa Zanzibar wanataka kutuaminisha Kuwa JMT ni serikali ya Tanganyika.
 
Hivi barua ya maombi ya Wazanzibari waliowakilisha UN kwa Ban Ki Moon kujitenga imeshajibiwa?

Itabidi Serikali ya JMT ifanye robbing kubwa kwa kutumia influence za Prof. Tibaijuka (former boss UN Habita)
na Asha Rose Migiro (Deputy UN Secretary), ili hili jambo la mipaka ya bahari lipite haraka, na pia kwa
kutumia token hiyo hiyo, serikali ya JMT iwatumie watu hao influencial kwenye Siasa za UN kuhakikisha
ombi la Zanzibar kujitenga na Tanganyika lina gonga mwamba kama unachama wa Zanzibar FIFA!
 
Hongera sana Ismail Jussa.

Kwani huo ni uvunjifu wa Katiba zote mbili ya Muungano na ile ya Znz. Ni lazima kieleweke hapo na kumjuza Prof Tibaijuka kuwa Znz ni nchi anapaswa kuiheshimu kwa dhati kabisa.

Hongera sana mwakilishi wangu.

Vifungu vipi vya katiba vilivyovunjwa!
Btw: UN walitoa muda kwa nchi zinazotaka kuongezewa eneo toka ile sehemu ya kimataifa na deadline imefika huyo Jussa alikuwa wapi kutoa maoni yake?
 
Watanganyika bado mnaendelea kuwacheyea WaZANZIBARI? Subiri muone kali yao, sio wale mambumbumbu tena. Yangu macho.
 
Hongera sana Ismail Jussa.

Kwani huo ni uvunjifu wa Katiba zote mbili ya Muungano na ile ya Znz. Ni lazima kieleweke hapo na kumjuza Prof Tibaijuka kuwa Znz ni nchi anapaswa kuiheshimu kwa dhati kabisa.

Hongera sana mwakilishi wangu.

Usipojipongeza mwenyewe unamsubiri nani akupongeze.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom