Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 152,998
- 453,891
- Thread starter
- #821
SEHEMU YA 74
Hilo likamfanya mke wake kuhisi kwamba mume wake alikuwa na stresi kwa sababu ya mtoto wake aliyekuwa kitandani akiugua. Moyo wa Violeth uliumia zaidi, ni kweli aliumia kuona mtoto wake akiwa kwenye hali hiyo lakini suala la Theo kuanza kunywa pombe kuondoa stresi ilimuumiza zaidi.
*** Daktari waliendelea kumfanyia matibabu Rachel, hakuonyesha nafuu yoyote ile kitu kilichowafanya kuitana na kuanza kuijadili afya yake.
Hakukuwa na dalili zozote za kupona na kurudi kwenye hali yake ya kawaida kitu kilichowafanya kuwasiliana na madaktari wa Hospitali ya Munich Medcal Centre ambayo ilikuwa na watalaamu wa magonjwa ya moyo na kuwataka Theo na mke wake wamuhamishie mtoto wao huko Ujerumani.
Iliwaumiza mno, kitendo cha madaktari wa India kushindwa kumtibu mtoto wao waliona kabisa kwa sehemu nyingine isingewezekana.
Waliambiwa kuhusu hospitali hiyo iliyokuwa jijini Munich nchini Ujerumani kwamba ilikuwa na watalaamu wengi lakini bado hawakutaka kuamini.
Kibali cha Rachel kupelekwa huko kikatolewa na watu hao walitakiwa kuondoka naye haraka sana kuelekea nchini huko.
Kichwa cha Theo hakikumuwaza mtoto wake wala safari hiyo, alichukua muda mwingi kumuwaza Iyanya, alitakiwa kumfuata na kuzungumza naye, alitakiwa kumwambia kila kitu kuhusu safari hiyo .
Hakujua angezungumza naye vipi kwani waliambiwa kwamba ni siku hiyohiyo ndiyo ambayo wangeondoka kuelekea nchini Ujerumani haraka iwezekanavyo.
“Ngoja niende chooni,” alimwambia mke wake.
Akainuka na kuelekea chooni, huko kama kawaida yake akapata nafasi ya kuzungumza na Iyanya, alimwambia kuhusu kile walichoambiwa na daktari hivyo msichana huyo kutakiwa kurudi Afrika Kusini.
“Kwa hiyo nirudi nyumbani?” aliuliza Iyanya.
“Ndiyo! Haina jinsi! Ila nitakukumbuka sana,” alisema Theo huku akionekana kuwa mnyonge mno.
“Na mtarudi lini?”
“Bado sijajua! Ila nadhani hivi karibuni.”
“Sawa. Kwa hiyo unaniachaje?” aliuliza msichana huyo.
“Nakutumia dola elfu tano kwenye akaunti yako mpenzi!” alisema Theo.
“Sawa. Nashukuru mpenzi!” alisema Iyanya na kukata simu.
Hilo likamfanya mke wake kuhisi kwamba mume wake alikuwa na stresi kwa sababu ya mtoto wake aliyekuwa kitandani akiugua. Moyo wa Violeth uliumia zaidi, ni kweli aliumia kuona mtoto wake akiwa kwenye hali hiyo lakini suala la Theo kuanza kunywa pombe kuondoa stresi ilimuumiza zaidi.
*** Daktari waliendelea kumfanyia matibabu Rachel, hakuonyesha nafuu yoyote ile kitu kilichowafanya kuitana na kuanza kuijadili afya yake.
Hakukuwa na dalili zozote za kupona na kurudi kwenye hali yake ya kawaida kitu kilichowafanya kuwasiliana na madaktari wa Hospitali ya Munich Medcal Centre ambayo ilikuwa na watalaamu wa magonjwa ya moyo na kuwataka Theo na mke wake wamuhamishie mtoto wao huko Ujerumani.
Iliwaumiza mno, kitendo cha madaktari wa India kushindwa kumtibu mtoto wao waliona kabisa kwa sehemu nyingine isingewezekana.
Waliambiwa kuhusu hospitali hiyo iliyokuwa jijini Munich nchini Ujerumani kwamba ilikuwa na watalaamu wengi lakini bado hawakutaka kuamini.
Kibali cha Rachel kupelekwa huko kikatolewa na watu hao walitakiwa kuondoka naye haraka sana kuelekea nchini huko.
Kichwa cha Theo hakikumuwaza mtoto wake wala safari hiyo, alichukua muda mwingi kumuwaza Iyanya, alitakiwa kumfuata na kuzungumza naye, alitakiwa kumwambia kila kitu kuhusu safari hiyo .
Hakujua angezungumza naye vipi kwani waliambiwa kwamba ni siku hiyohiyo ndiyo ambayo wangeondoka kuelekea nchini Ujerumani haraka iwezekanavyo.
“Ngoja niende chooni,” alimwambia mke wake.
Akainuka na kuelekea chooni, huko kama kawaida yake akapata nafasi ya kuzungumza na Iyanya, alimwambia kuhusu kile walichoambiwa na daktari hivyo msichana huyo kutakiwa kurudi Afrika Kusini.
“Kwa hiyo nirudi nyumbani?” aliuliza Iyanya.
“Ndiyo! Haina jinsi! Ila nitakukumbuka sana,” alisema Theo huku akionekana kuwa mnyonge mno.
“Na mtarudi lini?”
“Bado sijajua! Ila nadhani hivi karibuni.”
“Sawa. Kwa hiyo unaniachaje?” aliuliza msichana huyo.
“Nakutumia dola elfu tano kwenye akaunti yako mpenzi!” alisema Theo.
“Sawa. Nashukuru mpenzi!” alisema Iyanya na kukata simu.