Moyo Ulioonja Maumivu

Moyo Ulioonja Maumivu

Asante shunie. Theo atakuja kujuta. Watu wa hivyo wapo wakishajiona wanao, wanaueneza makusudi
 
SEHEMU YA 71

Theo aliendelea kumfikiria Iyanya, kwake hakukuwa na mwanamke aliyekuwa mzuri kama msichana huyo. Kichwani mwake kulipita warembo wengi, aliokuwa amelala nao kwa kipindi kirefu lakini kwa Iyanya, kwake alikuwa kila kitu.

Alimuacha mke wake akiugulia peke yake, hakuwa na moyo wa huruma, kila alipokuwa akimwangalia, hakuona kama alikuwa na mapenzi yoyote yale moyoni mwake kwa mke wake huyo.

Baada ya kupita siku kadhaa, Iyanya akampigia simu na kumwambia kwamba alikuwa tayari kusafiri na kwenda nchini India kuungana naye.

Theo akafurahi, hakuamini kama msichana huyo mrembo sasa alikuwa tayari kwenda huko. Haraka sana akamwambia amfuate kwani alikuwa akimsubiri kwa mahaba yote.

Msichana huyo akaondoka nchini Afrika Kusini na kuelekea India. Ndani ya ndege alimfikiria mwanaume huyo, alimpenda lakini tamaa yake ya kutaka kuwa na maisha mazuri, pesa ilimfanya kulala na wanaume wengi.

Siku alipoingia, alipokea ujumbe kwamba tayari hoteli iliandaliwa kwa ajili yake, akaondoka na kuelekea huko na kulala usiku kucha huku akichati na marafiki zake na kuwaambia aliokota embe chini ya muarobaini, alibahatika kutembea na mwanaume maarufu kuliko wote Afrika.

“Unataka kusema ni Theo?’ aliuliza rafiki yake aliyekuwa upande wa pili.
“Ndiyo! Mwanaume anajua sana kupenda,” alisema Iyanya.

“Sasa si ndiyo utulie!”
“Ana mke! Nitatuliaje na mume wa mtu!”
“Basi mchune vya kutosha kama ndiyo hivyo! Ila kuwa makini, hao mastaa huwa wanakuwa na mademu wengi sana,” alisema rafiki yake huyo.

Aliwaambia wote hao kuhusu mpenzi wake huyo, kila mmoja alimsifia na kumwambia kwamba alistahili kuwa na mwanaume huyo kutokana na uzuri aliokuwanao.
Siku hiyo ambayo aliingia na kwenda hotelini, Kwa Theo hali ilikuwa ni balaa.

Alikuwa na hamu ya kuondoka na kumuacha mke wake hospitalini lakini hakujua ni kwa namna gani angeweza kuondoka mahali hapo.
 
SEHEMU YA 72

Hakukaa na kutulia, muda mwingi alikuwa akisimama na kutembea huku na kule, alionekana kufikiria mambo mengi na kitu pekee ambacho alihisi mke wake ni kwamba mume wake huyo alikuwa akiifikiria hali ya mtoto wao kumbe haikuwa hivyo kabisa.

“Iyanya! Haiwezekani! Leo ni lazima nije kulala na wewe,’ alijisemea Theo akiwa ndani ya chumba alicholazwa mtoto wake.

Muda mwingine alikuwa akikisogelea kitanda kile na kumwangalia mtoto wake, alikuwa akipitia kwenye matatizo makubwa lakini kutokana na kuwa na tamaa ya kulala na mwanamke ambaye alihisi kuwa na uzuri kuliko wote katika dunia hii, hakutaka kujali kabisa.

Mtoto Rachel aliendelea kuwa vilevile, hakuongea kitu, hakutingishika, hakulia wala kufanya kitu chochote kile. Mke wake, Violeth alikuwa akilia tu, kila alipomwangalia mtoto wake kitandani pale aliumia kupita kawaida.

“Mke wangu! Hutakiwi kulia, hiyo ni kumchulia mtoto,” alisema Theo huku akimwangalia mke wake.

“Moyo wangu unauma mume wangu!” “Najua! Ngoja nikakutafutie chakula,” alisema Theo, alifanya hivyo kwa kuwa alihitaji kuondoka hapo hospitalini na kwenda kumuona Iyanya hotelini.
“Hapana! Sijisikii kula.

Naomba ubaki nami, nitakula kesho asubuhi,” alisema mke wake maneno ambayo yalimuumiza mno kwani alitamani sana kuondoka, hakutaka kubaki mahali hapo hata kidogo.

“Hapana mke wangu! Ni lazima ule kwa afya yako, hata kama hujisikii njaa,” alisema Theo huku akimwangalia mke wake.

Hakutaka kubaki hapo hospitalini, alimwambia mke wake kwamba ni lazima aondoke mahali hapo na kwenda kumtafutia chakula. Japokuwa Violeth alikataa lakini hakuwa na jinsi na kwa sababu mume wake aling’ang’ania, hakuwa na jinsi.

Theo akaondoka, njiani alikuwa akikimbia. Hoteli ambayo alimchukulia chumba Iyanya haukuwa mbali kutoka hapo alipokuwa. Alitamani kuwa na kasi zaidi na muda mwingine alitamani hata kupaa.

Mhemko wa kuwa na Iyanya ulimshika mno, hakutaka kusikia la mtu yeyote yule na aliuahidi moyo wake kwamba siku hiyo ingekuwa ni ya hatari, ilikuwa ni lazima Iyanya ajutie uamuzi wake wa kwenda India.
 
SEHEMU YA 73

Hakuchukua dakika nyingi, akafika, alikuwa akitokwa na jasho, alipandisha ngazi harakaharaka kwani alihisi kama angechukua ngazi angechelewa kufika.

Alipofika katika chumba alichokuwa Iyanya, akagonga na msichana huyo kufungua. Alipogonganisha naye macho tu, hapohapo akamsukumia ndani kimahaba na kisha kumkumbatia.

Alihisi damu yake ikizunguka kwa kasi kubwa, alichanganyikiwa mno, alikuwa na kiu na mtu pekee ambaye angeweza kuikata kiu hiyo alikuwa ni Iyanya tu.

“Ninakupenda mpenzi, niikukumbuka sana,” alisema Theo huku akimwangalia msichana huyo kwa macho yaliyoonekana kuhitaji mapenzi yote.
“Nakupenda pia, nilikukumbuka sana,” alisema Iyanya.

Wakabebana mpaka bafuni, wakaoga na kusuguana migongo na baada ya huko wakaelekea chumbani ambapo huko wakaanza kufanya mapenzi bila kinga kama kawaida yao.

Siku hiyo Theo alifanyia komesha, alimkumbuka mpenzi wake huyo, alimtamani sana na alimuona kama mpya vile. Alimfanya alivyotaka.

Walikaa huko kwa saa tatu ndipo walimaliza na Theo kuondoka huku akimwambia msichana huyo kwamba angemuona siku inayofuata asubuhi.

Alikuwa na hofu kwamba mke wake angekuwa na wasiwasi kuhusu yeye, alimwambia kwamba alifuata chakula lakini mpaka muda huo hakuwa amerudi hospitalini.

Hakuwa na sababu ila alichokifanya ni kwenda katika kituo cha polisi na kumchukua mmoja na kupanga naye dili kwamba alitakiwa kumpeleka hospitalini ambapo huko angemwambia mke wake kwamba alimchukua kutoka baa alipokuwa akinywa, na kwa jinsi alivyoonekana, alikuwa na mawazo mno.

Polisi huyo akakubali, akapita katika duka la pombe na kuchukua chupa moja ya pombe kali, akaiingiza mdomoni na kusukutua kisha kuelekea huko.

Walipofika hospitalini, Violeth alishangaa alipoambiwa kwamba mume wake huyo alikutwa baa akiwa anakunywa, alilewa na kwa jinsi alivyoonekana tu, alikuwa na stresi mno.

“Mume wangu! Tatizo nini?” aliuliza Violeth huku akimwangalia mume wake.
“Rachel....Rachel...” aliliita jina la mtoto wake.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom