Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,076
- 463,977
- Thread starter
- #61
SEHEMU YA 16
Waliyauliza maswali yao, Violeth alijibu kwa umakini lakini Theo hakutaka kujibu kabisa kwani endapo angelazimishwa sana basi angetoa siri kuwa alimpenda msichana huyo na alikuwa tayari kwa lolote lile.
Baada ya waandishi kumaliza maswali yao, wawili hao wakaenda ndani ya magari yao na kuondoka mahali hapo.
Kichwa cha Theo kilichanganyikiwa, muda wote alikuwa akimfikiria Violeth, alikuwa msichana mrembo mno ambaye alikuwa tayari kufanya kila liwezekanalo kuhakikisha anamchukua na kuwa mke wa maisha yake.
Alipofika nyumbani, kwa kuwa alikuwa na namba ya msichana huyo, akampigia na kuanza kuzungumza naye.
Alikuwa na furaha mno, kwa jinsi Violeth alivyosikika kwenye simu, sauti yake ilivyokuwa nzuri hakika ilimchanganya na kuhisi kama alikuwa akizungumza na msichana mwenye sauti nzuri kuliko wote katika dunia hii.
“Violeth! Ninakupenda sana,” alisema Theo kwenye simu, alikuwa amelala, simu ilikuwa sikioni mwake.
“Ooh my God! (Oh Mungu wangu!) alijifanya kushangaa msichana huyo. “Kwa kipindi kirefu tulichokaa pamoja, nimejisikia tofauti sana, umeuteka moyo wangu kiasi kwamba sitaki kusikia lolote lile kuhusu wewe.
You’ve changed my world. Violeth! Ninakuhitaji, ninataka kuwa nawe katika maisha yangu yote,” alisema Theo kwa sauti ya chini kabisa ambayo aliamini ingemchanganya msichana huyo.
“Hapana! Si kwa sasa!”
“Kwa nini?”
“Moyo wangu una maumivu makali sana!”
“Najua! Ninahitaji nafasi ya kuyaondoa maumivu hayo, nitakufanya kuwa mwanamke mwenye furaha kuliko wote katika dunia hii,” alisema Theo.
“Theo....”
“Violeth! Tafadhali naomba nafasi,” alisema Theo.
Bado Violeth hakujiamini, alijiona kutokuwa tayari kuingia kwenye ulimwengu wa mapenzi na mwanaume yeyote yule, alijiwekea msimamo kwamba hatoingia kwenye uhusiano katika kipindi hicho.
Alimwambia hilo Theo, mwanaume huyo hakusikia, leo alipoambiwa hivyo, kesho asubuhi alimpigia simu na kuendelea kumsisitiza.
Baadaye Theo akagundua kwamba alikuwa akikosea kila alipompigia simu msichana huyo na kumsisitizia awe mpenzi wake bali alichotakiwa kufanya ni kumuonyeshea kwamba alikuwa akimpenda mno.
Waliyauliza maswali yao, Violeth alijibu kwa umakini lakini Theo hakutaka kujibu kabisa kwani endapo angelazimishwa sana basi angetoa siri kuwa alimpenda msichana huyo na alikuwa tayari kwa lolote lile.
Baada ya waandishi kumaliza maswali yao, wawili hao wakaenda ndani ya magari yao na kuondoka mahali hapo.
Kichwa cha Theo kilichanganyikiwa, muda wote alikuwa akimfikiria Violeth, alikuwa msichana mrembo mno ambaye alikuwa tayari kufanya kila liwezekanalo kuhakikisha anamchukua na kuwa mke wa maisha yake.
Alipofika nyumbani, kwa kuwa alikuwa na namba ya msichana huyo, akampigia na kuanza kuzungumza naye.
Alikuwa na furaha mno, kwa jinsi Violeth alivyosikika kwenye simu, sauti yake ilivyokuwa nzuri hakika ilimchanganya na kuhisi kama alikuwa akizungumza na msichana mwenye sauti nzuri kuliko wote katika dunia hii.
“Violeth! Ninakupenda sana,” alisema Theo kwenye simu, alikuwa amelala, simu ilikuwa sikioni mwake.
“Ooh my God! (Oh Mungu wangu!) alijifanya kushangaa msichana huyo. “Kwa kipindi kirefu tulichokaa pamoja, nimejisikia tofauti sana, umeuteka moyo wangu kiasi kwamba sitaki kusikia lolote lile kuhusu wewe.
You’ve changed my world. Violeth! Ninakuhitaji, ninataka kuwa nawe katika maisha yangu yote,” alisema Theo kwa sauti ya chini kabisa ambayo aliamini ingemchanganya msichana huyo.
“Hapana! Si kwa sasa!”
“Kwa nini?”
“Moyo wangu una maumivu makali sana!”
“Najua! Ninahitaji nafasi ya kuyaondoa maumivu hayo, nitakufanya kuwa mwanamke mwenye furaha kuliko wote katika dunia hii,” alisema Theo.
“Theo....”
“Violeth! Tafadhali naomba nafasi,” alisema Theo.
Bado Violeth hakujiamini, alijiona kutokuwa tayari kuingia kwenye ulimwengu wa mapenzi na mwanaume yeyote yule, alijiwekea msimamo kwamba hatoingia kwenye uhusiano katika kipindi hicho.
Alimwambia hilo Theo, mwanaume huyo hakusikia, leo alipoambiwa hivyo, kesho asubuhi alimpigia simu na kuendelea kumsisitiza.
Baadaye Theo akagundua kwamba alikuwa akikosea kila alipompigia simu msichana huyo na kumsisitizia awe mpenzi wake bali alichotakiwa kufanya ni kumuonyeshea kwamba alikuwa akimpenda mno.