Rocky City
JF-Expert Member
- Nov 22, 2017
- 982
- 749
Hata ningekuwa mm ningemsahau vp sasa,,umesikia mtoto ana chura balaaaa kwa mujib wa mwandishi.
Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app

Nimejaa tele mpenziKumbe upo bibie..?
Ooohooo acha nisikitike tu mimiHata ningekuwa mm ningemsahau vp sasa,,umesikia mtoto ana chura balaaaa kwa mujib wa mwandishi.
Sent using Jamii Forums mobile app
AuntieSEHEMU YA 62
Huo ulikuwa ni muda wa majonzi mazito, Theo alikuwa na maumivu makali moyoni mwake, kila alipokuwa akimwangalia mke wake, alisikia maumivu makali mno.
Alikaa na mkewe ndani ya chumba alicholazwa mtoto wao, mioyo yao ilikuwa na maumivu makali, kile kilichotokea kiliuma kupita kawaida. Baada ya saa kadhaa, wakaitwa ndani ya chumba cha daktari na kuambiwa kilichokuwa kikiendelea kwa mtoto wao.
Kwa Rachel jambo hilo lilionekana kuwa jipya, lilimuuma mno lakini kwa Theo halikuwa jipya, alilifahamu kwa kuwa aliambiwa kabla ila hakutaka kumwambia mke wake kwa kuwa aliamini angekuwa na majonzi zaidi.
“Niliambiwa hivyo na daktari,” alisema Theo maneno yaliyomfanya Violeth kushtuka kwani hakuamini kama mume wake alilifahamu hilo ila hakutaka kumwambia.
“Ulilifahamu? Kwa nini hukuniambia?” aliuliza Violeth huku akionekana kukasirishwa na kile alichokisema Theo.
Hakutaka kumficha, alimwambia ukweli kwamba hakufanya hivyo kwa kuwa alikubaliana na daktari anyamaze kwani endapo angemwambia kila kitu basi asingeweza kuvumilia kutokana na kile kilichotokea kwa mtoto mwingine.
Violeth hakutaka kuelewa, kwake aliona kama alisalitiwa lakini Theo alimwambia kila kitu, na alifanya vile kwa ajili yake kwani endapo angemwambia basi angeharibu kila kitu.
“Ni ushauri kutoka kwa daktari kwani hata mimi nilitamani sana kukwambia,” alisema Theo, alijitetea sana.
“Kwa hiyo hukutaka kuniambia kabisa!”
“Nilifuata ushauri wa daktari! Mke wangu, huu si muda wa lawama tenaa tunatakiwa kuungana kwa ajili ya afya ya mtoto wetu,” alisema Theo huku akimwangalia mke wake huyo.
Violeth hakutakiwa kulalamika kwa lolote lile, kile kilichofanyika kilikuwa ni kwa ajili yake hivyo kutakiwa kusahau na kuangalia afya ya Rachel tu.
Daktari huyo akawaambia kwamba matibabu juu ya misuli ya moyo wa Rachel yalitakiwa kufanyika nchini India, kwa nchi kama Tanzania ambayo ilikuwa na wataalamu wadogo ingekuwa vigumu sana kufanyika.

tunateseka wanao jmn kwani ulikua wapi.?SEHEMU YA 65
Baada ya kumaliza kila kitu, akatoka chooni na kuungana na mke wake. Ilikuwa ni vigumu kwa Violeth kugundua kilichokuwa kikiendelea, mwanaume huyo alijua kuigiza, alijua kumuonyesha ni kwa jinsi gani alikuwa na majonzi tele juu ya hali ya mtoto wao.
Violeth hakugundua kama mwanaume huyo alikuwa na mwanamke mwingine, hivyo akaendelea kuhuzunika huku akiamini Theo naye alikuwa kama yeye.
Mule ndani ya chumba lilipokusanyika jopo la madaktari wale, wakakubaliana matibabu yaanze mara moja, kwa kuwa Rachel alikuwa mdogo, mishipa yake haikuwa imekomaa, alitakiwa kupewa dawa maalumu za kuiweka sawa mishipa hiyo kwa ajili ya matibabu.
Walikubaliana, na kila kitu ambacho walikubaliana huko wakaenda kuzungumza na wazazi wake, waliwaambia kila kitu kwamba alitakiwa kupewa dawa kabla ya kuanza kufanyiwa upasuaji huo.
“Hakuna shida,” alisema Theo.
Hapo India walichukua chumba maalumu katika hoteli moja ya nyota tano na kukaa huko. Usiku hakukuwa na mtu aliyeonekana kuwa na furaha, Violeth alibaki akimfikiria mtoto wake lakini Theo alikuwa akimfikiria mpenzi wake, Iyanya ambaye alimwambia ni lazima afike nchini India kwa lengo la kula bata pamoja naye.
|
|
|
Je, nini kitaendelea?


najikaribisha arostoni.Nina mengi acha tuNakupenda pia mama k wanguungekuwa karibu ungenifanyaje eti babe.
![]()
Theo mbwa mkubwa wewe shetani wa miguu 7 mfyuuySEHEMU YA 64
Walichukua dakika kadhaa, wakafika na kupelekwa ndani ya chumba cha upasuaji. Kitu cha kwanza kabisa kabla ya wote ni jopo la madaktari kumi kukutana na kuanza kuipitia ripoti kutoka katika hospitali aliyotoka nchini Tanzania, wasingeweza kufanya kitu chochote kile pasipo kuipitia ripoti hiyo ambayo ingewapa mwanga wa wapi pa kuanzia.
Wakati madaktari wakiendelea kujadili kuhusu hali ya mgonjwa ndipo Theo akarudiwa na wazo kuhusu Iyanya.
Alishtuka, alimuacha msichana huyo hotelini, hakujua ni kitu gani kilitokea baada ya yeye kuondoka chumbani na kuelekea hospitalini.
Alitakiwa kuwasiliana naye na kumwambia kila kitu ili kama ingewezekana basi afunge safari na kuelekea nchini India kumfuata.
Haraka sana akamuaga mke wake kwamba alikuwa akienda chooni ambapo huko akampigia simu kwa WhatsApp na kuanza kuongea naye.
Kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kumuomba msamaha kwa kilichotokea, alimwambia alikuwa akipitia kwenye matatizo na familia yake hivyo angeomba sana amuonee huruma lakini penzi lao lilikuwa kama lilivyokuwa kipindi cha nyuma.
“When will you come back?” (utarudi lini?) aliuliza msichana huyo.
“I don’t know! I just want you to come here!” (sijui! Ninataka uje huku) alisema Theo.
“India?”
“Yaap!”
“Why?” (kwa nini?)
“I want to spend the time together. I really miss you my baby! Please, I want to see you,” (ninataka nitumie muda mwingi pamoja. Nimekukumbuka mno mpenzi! Nitaka kukuona, tafadhali) alisema Theo huku akionekana kumuhitaji mno mwanamke huyo.
“I got nothing in my pockets,” (sina kitu mfukoni)
“That’s not a problem!” (hilo si tatizo) alisema Theo.
Ilikuwa ni lazima kujitoa kwa mwanamke huyo, alimpenda kuliko hata mke wake, kwake, alimthamini na alikuwa tayari kufanya jambo lolote lile lakini mwisho wa siku aweze kuwa naye.
Alikuwa tajiri mkubwa, alikuwa na pesa, kwake, kumtumia pesa mwanamke huyo halikuwa tatizo hata kidogo hivyo haraka sana akafanya muamala na kumtumia kiasi cha milioni kumi kwenye akaunti yake.