Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 98,035
- 142,943
SEHEMU YA 61
“She won’t die....she won’t die...” (hatokufa....hatokufa...) alisema Theo huku akiwa amemkumbatia mke wake.
Walikaa kwenye hali hiyo kama dakika tano huku kila mmoja akilia. Walipomaliza, Theo akaanza kupiga hatua kumfuata Rachel kitandani pale, alipomfikia na kumwangalia, moyo wake ukazidi kuuma zaidi.
Mtoto huyo mdogo alitia huruma, alikuwa kimya kitandani huku akipumulia mtungi wa gesi iliyokuwa pembeni yake. Baada ya dakika kadhaa daktari akaingia na kuwaomba kutoka kwani walihitaji kuendelea na matibabu.
Wakatoka chumbani humo na kuelekea kwenye korido ambapo hapo wakawakuta waandishi wa habari ambao nao walijifanya kama wagonjwa na kuanza kuwapiga picha pamoja.
Muda wote huo Theo alikuwa akiumia, alijiona kuwa mkosaji kwamba yeye ndiye aliyesababisha hayo yote kwani kama angetulia nyumbani aliamini kwamba angemsaidia mke wake muda wote mpaka kufika hapo hospitalini.
“Ungenipigia simu mke wangu....” alisema Theo kwa sauti ya chini.
“Nilishindwa...nilichanganyikiwa mume wangu....” alisema Theo.
Wakauomba uongozi wa hospitali uwaondoe waandishi hao mahali hapo, wakafanya hivyo na kubaki peke yao na baadhi ya wagonjwa waliokuwa hapohapo.
Siku hiyo haikuwa ya kuondoka tena kurudi nyumbani, walitakiwa kuendelea kubaki hapohapo mpaka pale ambapo daktari angewaeleza kulikuwa na tatizo gani. Kwa sababu familia ilikuwa kwenye hayo matatizo, Theo akaahidi kupambana nayo mpaka mwisho, hata Iyanya, akapanga kumsahau.
|
|
|
|
JE, nini kitaendelea?
Ngabu bwana hili swali unaniuliza mara ya pili ujue na mwanzo nilishakujibu
Nazitoa kwa nyemo zao la shigongo ndio mtunzi wa hizi story
Oh samahani kama nimekukera. Uzee tu unanisumbua.
Nasahau sahau sana. Nisamehe tu.
Ahsante kwa kujibu.
anawakilisha vyema lkn mkuu wanaume kweny ubora wenu hahahaha
Yah anaitendea haki nafasi ya wenye vipaji hivyo......ila kwa sisi wengine tuliotulia, tunaona anaharibu tu tafsiri harisi ya neno mwanaume.anawakilisha vyema lkn mkuu wanaume kweny ubora wenu hahahaha
Hahahaha nakuja pm tafadhali nipokeeSema kweli
Lini uliniomba eti
Toba!!!!Sema kweli
Lini uliniomba eti
Omba tuToba!!!!
Sijui na mimi niombe??? (Oooh sorry, nimejikuta nikiwaza kwa sauti).
Sent using Jamii Forums mobile app
Aisee majibu yako yamenichekesha. Halafu umejibu kistaarabu kabisaOh samahani kama nimekukera. Uzee tu unanisumbua.
Nasahau sahau sana. Nisamehe tu.
Ahsante kwa kujibu.
Aisee majibu yako yamenichekesha. Halafu umejibu kistaarabu kabisa
nakwako pia kipenzi,uje nakupenda mieNna hasira nae mimi[emoji38][emoji38] yooo
Heri ya mwaka mpya mpnz.
Sent using Jamii Forums mobile app
Ujue me nakupenda wewe,wish ningekuwa hata karibu[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] happy new year mama k wangu [emoji8] kivuruge wangu mm
Theo mjalaana,hawezi kumsahau iyanyaSEHEMU YA 61
“She won’t die....she won’t die...” (hatokufa....hatokufa...) alisema Theo huku akiwa amemkumbatia mke wake.
Walikaa kwenye hali hiyo kama dakika tano huku kila mmoja akilia. Walipomaliza, Theo akaanza kupiga hatua kumfuata Rachel kitandani pale, alipomfikia na kumwangalia, moyo wake ukazidi kuuma zaidi.
Mtoto huyo mdogo alitia huruma, alikuwa kimya kitandani huku akipumulia mtungi wa gesi iliyokuwa pembeni yake. Baada ya dakika kadhaa daktari akaingia na kuwaomba kutoka kwani walihitaji kuendelea na matibabu.
Wakatoka chumbani humo na kuelekea kwenye korido ambapo hapo wakawakuta waandishi wa habari ambao nao walijifanya kama wagonjwa na kuanza kuwapiga picha pamoja.
Muda wote huo Theo alikuwa akiumia, alijiona kuwa mkosaji kwamba yeye ndiye aliyesababisha hayo yote kwani kama angetulia nyumbani aliamini kwamba angemsaidia mke wake muda wote mpaka kufika hapo hospitalini.
“Ungenipigia simu mke wangu....” alisema Theo kwa sauti ya chini.
“Nilishindwa...nilichanganyikiwa mume wangu....” alisema Theo.
Wakauomba uongozi wa hospitali uwaondoe waandishi hao mahali hapo, wakafanya hivyo na kubaki peke yao na baadhi ya wagonjwa waliokuwa hapohapo.
Siku hiyo haikuwa ya kuondoka tena kurudi nyumbani, walitakiwa kuendelea kubaki hapohapo mpaka pale ambapo daktari angewaeleza kulikuwa na tatizo gani. Kwa sababu familia ilikuwa kwenye hayo matatizo, Theo akaahidi kupambana nayo mpaka mwisho, hata Iyanya, akapanga kumsahau.
|
|
|
|
JE, nini kitaendelea?