kbm
JF-Expert Member
- Oct 5, 2012
- 5,224
- 1,685
ppf tower inawaka moto asubuhi hii
"Ni JENGO LA ppf" LILOKO MAKUTANO YA MTAA WA OHIO NA GARDEN AVENUE katikati ya jiji la Dar es Salaam, mtaa wa Garden avenue linawaka moto mkali.
Kwa sasa moto unatoke kwa juu ya paa ya jengo hilo.
Gari la zima moto na wafanyakazi wa zimamoto wanahagaika kutafuta mbinu na jinsi ya kuweza kufika juu ya jengo, lakini kufuatana na vifaa duni wanapata shida jinsi yakuweza kufika eneo lenye moto.
Vijana wazimamoto wamejitahidi kupunguza kasi ya moto, lakini bado kuna dalili za moshi mzito upande wa kusini mwa jengo.
Hatimaye moto umezimwa eneo lote la jengo. Kwa sasa hakuna dalili zozote za moshi juu ya jengo.
"Ni JENGO LA ppf" LILOKO MAKUTANO YA MTAA WA OHIO NA GARDEN AVENUE katikati ya jiji la Dar es Salaam, mtaa wa Garden avenue linawaka moto mkali.
Kwa sasa moto unatoke kwa juu ya paa ya jengo hilo.
Gari la zima moto na wafanyakazi wa zimamoto wanahagaika kutafuta mbinu na jinsi ya kuweza kufika juu ya jengo, lakini kufuatana na vifaa duni wanapata shida jinsi yakuweza kufika eneo lenye moto.
Vijana wazimamoto wamejitahidi kupunguza kasi ya moto, lakini bado kuna dalili za moshi mzito upande wa kusini mwa jengo.
Hatimaye moto umezimwa eneo lote la jengo. Kwa sasa hakuna dalili zozote za moshi juu ya jengo.
Taarifa zinasema kuwa,hitilafu ya umeme iliyotokea kwenye mitambo ya mawasiliano iliyopo katika chumba cha 11, kilichopo juu, mwisho kabisa mwa jengo la minara ya PPF lililopo kwenye makutano ya Ohio/Garden Avenue, katikati ya jiji la Dar es Salaam ndiyo iliyosababisha moto asubuhi ya leo majira ya saa moja, na kusababisha jengo hilo ushika moto.
Imetaarifiwa kuwa walinzi wa jengo hilo walishuhudia moshi mzito ukitoka ndani ya jengo hilo la ghorofa, ndipo walipotoa taarifa kwa vikosi vya zima-moto.
Kikosi cha uokozi kilifika kwa wakati katika eneo husika na pamoja na kuweko nyenzo katika jengo hilo za kukwea hadi ghorofa ya kumi na moja, ufupi wa mipira ya zima-moto ili kufikisha maji kwenye chumba kinachowaka moto ulikwamisha jitihada za kuuzima moto huo. Hata na hivyo, juhudi zilizofanywa na kikosi hicho zimefanikiwa kuuzima moto huo kuzima kabisa mnamo mwendo wa saa tano kasoro za adhuhuri.
Polisi wapo katika eneo hilo ili kulinda mali zisiporwe au kuharibiwa na vibaka.
Hakuna madhara yoyote ya moja kwa moja kwa binadamu yaliyoripotiwa. Thamani ya hasara iliyosababishwa na moto huo nayo haijafahamika.