Moto wawaka jengo la PPF Tower - Dar

Moto wawaka jengo la PPF Tower - Dar

Status
Not open for further replies.
dah. bahati mbaya uwezo wa vifaa vyetu vya zimamoto (public & private) ni kama ghorofa 7 tu. kwa hizo ghorofa 17 itabidi tusubiri moto ushuke ghorofa za chini ili tuonekane tumefanya kazi.

ANGALIZO: kwa wanaopanga kwenye majengo marefu hakikisha hauendi juu zaidi ya uwezo wa ZIMAMOTO zilizopo kwenye mji wako.
 
Hapa kuna kuchoma document ilikuficha ushaidi fulani na kubwa zaidi ni deal la insurance watu waendele kukaa mjini

V
SENGEREMA
 
ppf tower inawaka moto asubuhi hii
"Ni JENGO LA ppf" LILOKO MAKUTANO YA MTAA WA OHIO NA GARDEN AVENUE katikati ya jiji la Dar es Salaam, mtaa wa Garden avenue linawaka moto mkali.
Kwa sasa moto unatoke kwa juu ya paa ya jengo hilo.
Gari la zima moto na wafanyakazi wa zimamoto wanahagaika kutafuta mbinu na jinsi ya kuweza kufika juu ya jengo, lakini kufuatana na vifaa duni wanapata shida jinsi yakuweza kufika eneo lenye moto.

Vijana wazimamoto wamejitahidi kupunguza kasi ya moto, lakini bado kuna dalili za moshi mzito upande wa kusini mwa jengo.
Kwa majengo yetu marefu na uozo wa matayarisho wa kuzuia moto, nilijua hili litatokea siku moja and we will be powerless kuzuia au kuzima moto huo!

Hapo hakuna jinsi jengo litateketea tu!
 
janga la moto kwa tz ishakuwa kama wimbo yaan hv vikosi vya zima moto mpaka kero wakija wao hawakosagi visingizio ooooh mala ngaz hazifiki sasa walikujaje kama ngaz zao fup au ndo kuonesha na wenyewe walifika eneo la tukio?
 
Kwani Vodacom wameshahama ndani ya jengo hilo ? Siku nyingi sipo Dar ( sijui ) kama Vodacom hawajahama basi kuna kitu kinatafutwa hapo kufichwaa...

Hakuna jengo kubwa kama hilo hapa Tanzania ambalo halina miundombinu ya Uzimaji moto , Sema tu hao Zimamoto wetu hawataki kuuzima ! Kila jengo kubwa na la kisasa kama hilo lina Automatic sense za moshi tu na kufyatua maji kutoka juu ya dari, Achana na yela ma pipe mekundu kibao kila floor yaliyokitwa ukutani mwa jengo kwa ajili ya kuzima moto yenye maji kibao ni kuinyakua tu kutoka ukutani na kuweka switch on na kuachia maji !
 
Si liko mbele ya Wazara ya Mambo ya Ndani? Mabomu na marungu hamna?
 
Ikulu kulishaungua moto allegedly ulioanzia na pasi.

Tunajenga vipi mighorofa bila ya kuwa na mipango ya kuzima moto?

Nafikiri kama si Mwanakijiji basi kuna mwandishi mmoja wa Tanzania Daima au Mwananchi aliwahi kuandika makala akilichambua hili la kujengo majengo marefu lajini bila kutengeneza mfumo wa kudhibiti najanga ya mito.

Mwanakijiji yeye alukwenda mbali zaidi (sina uhakika ni katika makala hiyo hiyo au la, ila ninauhakika aliandika), akipendekeza kuletwa kwa magari yenye ngazi ndefu kuweza kupambana na moto katika maghorofa kwanu lile lilipo ngazi yake ni fupi ukilinganishwa na urefu wa yale yaliyojengwa na yanayojengwa. Kama haitoshi alipendekeza pawepo na vituo vya zimamoto zaidi ya kimoja kwa Dar, si kutegemea kile kilichopo Mwembetogwa (jina asilia la eneo la Fire).
 
Nasikia sasa hivi maombi makali yakiongoza na faya yanafanyika kuomba mvua kali inyeshe! Haya sisi tunasubiri tuone
 
wajinga utawasikia tu ati huo ni mpango wa FREEMASON hivi sasa hivi wanakalukuleti tarehe ya leo mwezi na mwaka na saa ilipoanza kuungua ili waje na data za kijinga na kihuni...kila kitu FREEMASON ,mtuache tupumue jaman kaah

Hayo ndo mawazo yako kwan unalazimishwa kuwasikiliza au unapenda mwenyewe
 
Akili fupi sana za wakuu wetu, mnatoa vibali vya magorofa mrefu ili hali hkuna vifaa vya kuzimia moto? Does this make sense to any one of ypu guys?
 
Kwani Vodacom wameshahama ndani ya jengo hilo ? Siku nyingi sipo Dar ( sijui ) kama Vodacom hawajahama basi kuna kitu kinatafutwa hapo kufichwaa...

Hakuna jengo kubwa kama hilo hapa Tanzania ambalo halina miundombinu ya Uzimaji moto , Sema tu hao Zimamoto wetu hawataki kuuzima ! Kila jengo kubwa na la kisasa kama hilo lina Automatic sense za moshi tu na kufyatua maji kutoka juu ya dari, Achana na yela ma pipe mekundu kibao kila floor yaliyokitwa ukutani mwa jengo kwa ajili ya kuzima moto yenye maji kibao ni kuinyakua tu kutoka ukutani na kuweka switch on na kuachia maji !

Kweli??
 
haya mambo ya kuungua ofisi weekend watu wwakiwwa hawapo kazini kunaleta utata sana
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom