Huu uzi ulinipita wapi sijui, ila nashukuru kwa kutambua, umama ni raha sana, dhana ya msalaba wala haipo. Na nguvu hii niliipata punde tu nilipoona product yangu mwenyewe, with my eyes, color and lips. Enzi hizo tunatumia nepi, sio hizi dispozabo diaper, maji na kwanga wakawa marafiki zangu, kamba zimefungwa kila mahali, uwii mvua ikinyesha nepi zinachelewa kukauka maan inabidi uanue. Nikajifungia kamba zangu ndani, watu woote wanalalama naharibu mwonekano, lakini i was so excited and so occupied na kijana wangu.
Sijawahi kuwa excited kiasi kile kwenye maisha yangu, not even when zombie proposed.
Kweli tupu, wababa tunawashukuru kwa kufanya ndoto zetu kuwa kweli. Afu sijui kama wanajua, yaani jamaa kila akisababisha kiumbe kuja duniani upendo unazidi. Sijui sababu na wao sura zao hubaki wa watoto? Wakati wa ujauzito ndio kabisa, ni mwendo wa 'mahaba niue', kuna siku nitafuata mtu kazini nikamsubirie:A S 13:
Na kwa wanaotafuta nawaombea wapate, ni furaha kuwa mama, sana sana.