Moshi: Vijana watatu wa familia moja wauliwa na wanakijiji kwa tuhuma ya wizi wa pikipiki

Vijana watatu wa familia moja katika kijiji cha Manushi kati wilaya ya moshi vijijini wamechomwa moto hadi kufa na wanakijiji wenye hasira kali baada ya kuiba pikipiki kutoka machame.

Vijana hao wajulikanao kama ombeni kasamu, Anorld kasamu, na Marius kasamu wamechomwa moto nyumbani kwao manushi kati na wanakijiji kutoka machame baada ya kuiba piki pikipiki moja huko machame.

Wanakijiji kutoka machame waliwatafuta vijana hao na kwa kushirikiana na wenyeji wa kijiji hicho waliwatoa ndani ya nyumba na kuwachoma moto vijana wawili kati ya watatu ambao ni wa familia moja.,na baadae wenyeji wa kijiji wakamchukua na mdogo wao na. Kuanza kumkata kata mapanga hadi kufariki.

Tukio hilo limeleta furaha kijijini hapo baada ya wananchi kuchoshwa na ujambazi wa vijana hao hapo kijijini.

Tukio hilo limetokea jana kijijini hapo na polisi walipewa taarifa na kuja kuchukua miili ya marehemu hao na Kupelekwa kwenye nyumba ya kuhifadhia maiti moshi mjini.

Hadi sasa haijajulikana miili hiyo itazikwa lini

Hakuna Mwanakijiji yoyote aliyekamtwa kutokana na tukio hilo.

Update
Mazishi ya vijana hao ni kesho jumamosi,
Habari zaidi nitazisogeza hapa
Watu tuna roho mbaya sana. Hata kama umeibiwa why do you kill? Utakuta kati ya walioua wengi ni wezi serikalini, wengine wanaiba wake za watu n.k.

Tusiyachekelee mauaji kama haya, mtu yeyote naweza kuwa victim wakati wowote. Mauaji kama haya yamesababisha watu wasio na makosa/hatia wauawe.

Binamu ya wife aliuwawa mkoa fulani nyanda za juu alipokuwa akifanya kazi serikalini, huku akitoa mikopo midogo isiyo rasmi ili kuongeza kipato.

Siku moja alienda kwa wadeni waliokuwa wakimsumbua kijijini pembeni ya mji. Wakopwaji waliwaambia wanakijiji wenzao kuwa huyo mkopeshaji ndio mhalifu wa tukio la kupotea mtoto pale kijijini siku za karibuni, hivyo wakapiga yote kuitana na kisha kumwua. Haki hadi leo haijapatikana.

From nowhere mbaya wako anaweza kukufanya uuawe na kundi la watu.
 
Matukio ya wizi wa Pikipiki na ukwapuaji wa simu Moshi yameongezeka mno, ndio maana wananchi wamejaa hasira vichwani mwao. Juzi kati tu chalii wa 20 Years alipigwa na Rungu kichwani wakamchukulia pikipiki yake na kusababisha kifo chake.
 
Ukitaka kuishi kwa amani bila hiana na mtu, heshimu vitu vya watu.

Kujichukulia sheria mkononi kuna visababishi, hasa "wenye hasira" wakipima sheria inavyowakandamiza wenye haki na kupewa ushindi waporaji.

Tuna maumivu ya kifikra kusikia mauaji ya kiholela kama haya yanayoongelewa sasa yakifanyika, lakini dunia ya wastaarabika tusimame kati kuhubiri amani na siyo kuegemea upande, mfano wa kauli za kwamba pikipiki ya mtu ni uchafu, yaani mali ya mtu ni uchafu, nimestaajabishwa sana na kauli hii!

Vaa uhusika wa kuporwa mali kijambazi uone maumivu ya kisaikolijia yatakavyokuandama!

Jambo hili limekwishatokea, tuliobaki tujifunze kutendeana mema na wa kwanza kutenda wema ni wewe.

Mob justice hawafanyiwi watu wema, bali hufanywa kwa wahalifu, bakia na akiba hiyo kichwani mwako.
Anasema pikipiki ni uchafu. Hajui kwamba wezi kabla ya kuondoka na pikipiki wanamnyonga kwanza mwenye pikipiki kwa waya au wanamtoboa na bisibisi shingoni. Jamaa mjinga sana huyu.
 
Watu tuna roho mbaya sana. Hata kama umeibiwa why do you kill? Utakuta kati ya walioua wengi ni wezi serikalini, wengine wanaiba wake za watu n.k.

Tusiyachekelee mauaji kama haya, mtu yeyote naweza kuwa victim wakati wowote. Mauaji kama haya yamesababisha watu wasio na makosa/hatia wauawe.

Binamu ya wife aliuwawa mkoa fulani nyanda za juu alipokuwa akifanya kazi serikalini, huku akitoa mikopo midogo isiyo rasmi ili kuongeza kipato.

Siku moja alienda kwa wadeni waliokuwa wakimsumbua kijijini pembeni ya mji. Wakopwaji waliwaambia wanakijiji wenzao kuwa huyo mkopeshaji ndio mhalifu wa tukio la kupotea mtoto pale kijijini siku za karibuni, hivyo wakapiga yote kuitana na kisha kumwua. Haki hadi leo haijapatikana.

From nowhere mbaya wako anaweza kukufanya uuawe na kundi la watu.
Tulia hapohapo. Hao wauwaji wa jamaa yako ndiyo sawa na hao wezi wa pikipiki. Unataka kuwatetea si ndiyo?
 
Shida ya wezi ukiingia kwenye 18 zao hautoki mzima na ukitoka mzima lazima wakuachie kovu au kilema.
Shida nyingine watu hawaoji wakifika wanapiga tu kuna case nyingi za mauaji kwa watu wasio na hatia kwa kusingiziwa ni wezi.
 
Back
Top Bottom