MOSHI: Serikali yaifunga bar maarufu ya Meku's Bistro

MOSHI: Serikali yaifunga bar maarufu ya Meku's Bistro

Hivi punde

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2017
Posts
2,554
Reaction score
8,606
Halmashauri ya Manispaa ya Moshi imempa mfanyabiashara anayemiliki klabu mashuhuri ya Meku’s Bistro Bar & Restaurant muda wa saa 24 kuifunga klabu hiyo kwa kukiuka sheria za nchi.

Klabu hiyo ambayo ni moja kati ya klabu mashuhuri mjini Moshi, inadaiwa kukiuka sheria ya mazingira ya mwaka 2004 kwa kupiga muziki kwa sauti kubwa na kuwa kero kwa majirani.

Barua ya halmashauri hiyo ya Machi 8, 2018 iliyotiwa saini na Danford Kamenya kwa niaba ya mkurugenzi wa manispaa, imesisitiza klabu hiyo kufungwa ndani ya saa 24 baada ya kupokea barua hiyo.

“Pamoja na ushauri wa mara kwa mara kuhusu kuzingatia masharti bado juhudi zetu zimekwama. Aidha imebainika biashara yako ya baa na mgahawa iko eneo hatarishi ambalo ni kituo cha mafuta.

“Kulingana na aina ya biashara unayoifanya kukusanya watu wengi na kuhitaji eneo kubwa zaidi unashauriwa kutafuta eneo linalofaa kwa shughuli hiyo.
“Unatahadharishwa kuwa kukaidi kutekeleza amri hii kunailazimisha ofisi kuchukua hatua kali za kisheria dhidi yako bila kukupa onyo lingine lolote pamoja na kukufikisha mahakamani,” imesema.

Mkurugenzi wa manispaa hiyo, Michael Mwandezi alipoulizwa na MCL Digital leo, amekiri ofisi yake kutoa amri hiyo na kwamba hiyo ni baada ya njia zote za kidiplomasia kushindikana.

Mwandezi alisema halmashauri ilikuwa haina jinsi nyingine ya kufanya kwa kuwa mmiliki wake alishapewa onyo mara kadhaa na hata kutozwa faini, lakini hakutaka kujirekebisha.
 
Ngoja nitaangalia mwezi wa kumi na mbili nikienda
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Aisee nisehemu amazing sana nakumbuka December nilikua hapo, sijui nn shida ila niliona mambo yalienda vizuri tu.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Maskini meku....yule baby wake atamuhongaa nini???manake kwa kumspoil yule kijana hajambo sasa sijui atamuhonga nini mumewe .....mdomo koma

Juzi kwenye kili wakina perer more walipiga show kabambe na ilijaza pa kukanyga hakuna dats why wanasema watu walijaaa sana kuliko eneo lilivyo kwa tuliokuwepo riadhani mtaniambiaaa yaan nyomi la haja
 
Kati ya bar na kituo cha mafuta, nani aliyeanza biashara? Kwahiyo anatakiwa kufunga kwa sababu ya mazingira hatarishi si kwa sababu ya kelele.
 
Sad news, kijiwe changu hiki Japo kipo eneo hatarishi kwa maana ya barabarani na sheli
 
Kati ya bar na kituo cha mafuta, nani aliyeanza biashara? Kwahiyo anatakiwa kufunga kwa sababu ya mazingira hatarishi si kwa sababu ya kelele.
Kwani mmiliki wake ni nani
 
Figisu kivipi ndugu hebu funguka Ina maana hayo madai siyo ya kweli hata moja......!!!?
Usimshangae...huyo ni mpinzani....kishajenga hoja hpo ndio anaipeleka ikajadiliwe na kikao cha juu cha chama chake ili kesho waite wanahabari kulaani....
Angekuwa na akili singekimbilia kusema figisu....kwenye jambo lenye athari kwa wengi
 
Back
Top Bottom