Moses Machali amtaka Zitto kuwa na nidhamu

Moses Machali amtaka Zitto kuwa na nidhamu

Status
Not open for further replies.

saidi kindole

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2012
Posts
311
Reaction score
796
machali.png

Mbunge wa Kasulu Mjini, Moses Machali kufuatia kauli ya Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe kufuatia kauli yake kuwa kuwa ili wabunge wanane wa majimbo ya Mkoa wa Kigoma waweze kushinda katika uchaguzi Mkuu ujao lazima wajiunge na chama hicho kipya.

"Zitto anapaswa kuwa na nidhamu na angeelekeza nguvu zake katika kujenga umoja wa wapinzani. Kwanza sijui anatoa kauli hii kwa kutumia msingi upi? Mwaka 2010 alipita jimboni kwangu kuwapigia debe wagombea wa CHADEMA lakini nilishinda," alisema Machali.

Machali aliendelea kusema "Nilipata ubunge siyo kwa sababu ya Zitto, walionipa ubunge ni wananchi. Zitto hana msaada wowote kwangu na asidhani kwamba yeye ni maarufu kuliko wabunge wengine, asitushushe."
 
UKAWA wengi vichwa maji wamesahau kuhusu CCM sasa wana pambana na mtu makini Zitto kabwe..

CCM itatawala milele..
 
Kuna haja gani ya kupambana na CCM alihali CCM ina jimaliza yenyewe??? By d way sion kama ZZK umaarufu wake unabadili uelewa wa watu zaid ya watu kuendelea kumtambu true color yake
Unapotoa kauli angalia effect kwanza siyo kama huyu kibaraka anavyofanya mpaka anaharibu kazi yake ya CCM aliyotumwa

Ila kama ni lengo pia kuharibu kazi aliyotumwa kwa manufaa ya upinzan ni sawa tunaomba kila siku atoe kauli zake
 
UKAWA wengi vichwa maji wamesahau kuhusu CCM sasa wana pambana na mtu makini Zitto kabwe..

CCM itatawala milele..

Hauoni kuwa yeye na hicho chama ndicho kinapambana na Upinzani halisi

Chama kilichoundwa na kinachofadhiliwa na CCM ili kuudhoofisha Upinzani wa UKAWA

Chama ambacho katika ajenda zake namba moja ni kuibomoa chadema
 
Sio peke yake Machali

Kwa upande wa kafulila alisema "Kauli ya Zito ni ya kawaida kutolewa na wanasiasa.Leo hii hakuna chama kitakachojitangaza kuwa kitashindwa uchaguzi.Ni sawa na anayeuza dawa hata kama haimponyi yeye atainadi tu"

Kafulila ambaye kwa muda mrefu amekuwa na urafiki na zito alisema ushindi wake katika uchaguzi mkuu hautegemei uwapo wa act "Nimeshinda ubunge nikiwa NCCR na nitaendelea kushinda nikiwa na chama hiki.Wanaonipigia kura ni wananchi na ushindi uko palepale" alisema

Obama ambaye ni mwenyekiti wa wabunge wa kigoma alisema kauli ya Zito inalenga kujipatia "ujiko" kwa wananchi

Source ;Mwananchi Tar 10,April 2015 Ukurasa wa 7
 
Zitto Kabwe, abakishe na maneno ya kesho kwa sababu aliwahi kujinadi anaenda kufundisha chuo na kuachana na siasa leo yupo kupambana na wabunge wa upinzani.

kawatisha Mdee, Mnyika sasa anaenda kuwatikisa wabunge wa upinzani Kigoma. najua kule ambaye wataelewana Tumbili
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom