More than serious nahitaji mume wandugu

Una miaka "33 - 43" ndio nini hicho, unaficha nini, au ni kibibi kimepigika?

Kama "mke mme mwema anatoka kwa Mungu," kwa nini unakuja kutafuta mume mitandaoni, kwani Mungu hajui kwamba unatafuta akushushie mume?

Kama unataka mtu wakuwa nae "kwa raha na tabu," kwa nini hutaki mtu mwenye tabu ya ukimwi? Kama hupendi mtu ambae hajamaliza starehe za dunia za kupenda wanawake kwa sababu "kuna janga la ukimwi," vipi ambae anajua kujikinga na ukimwi lakini anapenda wanawake? Na ukimwi si una dawa?

Mchumba awe "walau elimu ya chini awe na diploma angalau awe na kabachela." Hueleweki, diploma ndio nini na "kabachela" ndio nini?

Awe ameajiriwa kwenye "shirika au serikalini." Vipi kama ana mahekari ya mashamba ya kahawa na ng'ombe wa maziwa na nyama na maduka ya kubadilisha hela ambayo sio "shirika"? Unajua unachokiandika?

Hutaki mtu anaetaka "kujaribisha," well, mtu una mvua 43 usawa huu, nitajuaje bado unashika mimba wewe kama sijajaribisha kwanza?

Wife advertisement yako haijaenda shule.

Kiongozi invisible alikupa kazi ya kusahihisha advertisements? hongera
 
mtarajiwa wako unataka awe na umri gani? wowote? jaribu kufafanua kidogo dada yangu
 
Dada yangu Almight God yupo karibu na sisi na anajibu maombi. Nikushauri kitu kimoja, mbuzi hula urefu wa kamba yake jitahidi kuomba mtu ambaye ni eneo lako ili ujiridhishe na mambo mengi kutoka kwake. Umesema una 33 - 43 je una mtoto? Anyway kwa sababu sina interest sina haja ya kukuhoji kama upo kwa pilato lakini kama kweli una hofu ya Mungu omba Mungu atakupa mume mwema kabisa japokuwa umechelewa hadi kwani assume una 33 na umri mzuri wa kuzaa ni safe ni < 35 sasa hadi mchumba umpate na kuoana nakadiria 35 itakuwa inaaproach hivyo itamlazimisha mumeo akikuoa tu na ndoa isichelewe kujibu. Na katika kipindi kigumu kwa wanaume ni wake zao wanapokuwa wajawazito na wakishajifungua! Mumeo kweli inabidi awe amemaliza starehe za dunia japokuwa si rahisi sana.
 
mtarajiwa wako unataka awe na umri gani? wowote? jaribu kufafanua kidogo dada yangu
Sema dada yangu alikuwa busy kukemea mizaha akasahau mambo madogo madogo kama haya lakini yana matter sana katika kutoa maamuzi.
 
Kumbe hujaelewa maana.

Wewe ni mwanamke uliyejitangaza kuwa unatafuta mume, umetangaza kwamba mke anapatikana, "wife advertisement"! Sasa ghafla watoka mapovu ya nini binti, si umesema unataka mtu "muwazi"?

Anheuser
Again, take sometime to read na kutafakari before jumping into meaningless_____________________anayetafuta mume is "Jena", and I am Nemo, ie we are two different persons. Sasa basi If you failed to realize such a simple fact , what does that say re:your comments and/or great thinking??............Just curious:A S embarassed:!

Jena
My apologies again for filling your thread with...................
 
Ta
Anheuser
Again, take sometime to read na kutafakari before jumping into meaningless_____________________anayetafuta mume is "Jena", and I am Nemo, ie we are two different persons. Sasa basi If you failed to realize such a simple fact , what does that say re:your comments and/or great thinking??............Just curious:A S embarassed:!.
Unatoka nje ya mada. Wewe ndio mnakuwadiana na huyo mwingine, for all I know nyinyi wamoja katika kutafuta mume, ambacho sio jinai. Tatizo, tangazo lako limepinda mno, huwezi kusema una umri kati ya 33 na 43. That's a decade long gap! Demu wa miaka 33 na shangazi lenye 43 ni binadamu wawili tofauti. Taja una umri gani ijulikane kama bado unazalishika.
 
Duh Anheuser "demu na shangazi" eee!

Hahaha sijui huwa mnafikiri nini!
 
TaUnatoka nje ya mada. Wewe ndio mnakuwadiana na huyo mwingine, for all I know nyinyi wamoja katika kutafuta mume, ambacho sio jinai. Tatizo, tangazo lako limepinda mno, huwezi kusema una umri kati ya 33 na 43. That's a decade long gap! Demu wa miaka 33 na shangazi lenye 43 ni binadamu wawili tofauti. Taja una umri gani ijulikane kama bado unazalishika.
Anheuser
I'm not going to waste my braincells dignifying this with an _______________Its not serving any purpose to this lady's thread,
but waste of space. In anycase you what they say, "never argue with a ____________cause people might not know the difference", so Im out!!!
 
Duh Anheuser "demu na shangazi" eee!

Hahaha sijui huwa mnafikiri nini!
I mean, come on Gaijin, jimama la 43 kitaani haliitwi demu tena, unamvunjia heshima, hilo ni "auntie" la nguvu, and again, umri si jinai, tatizo maa mdogo anaficha kati ya 33 na 43 hasemi kala chumvi kiasi gani hapo, I mean lazima watu wajue concetration ya chumvi wanazoenda ku deal nazo, uongo dadaangu?
 
I mean, come on Gaijin, jimama la 43 kitaani haliitwi demu tena, unamvunjia heshima, hilo ni "auntie" la nguvu, and again, umri si jinai, tatizo maa mdogo anaficha kati ya 33 na 43 hasemi kala chumvi kiasi gani hapo, I mean lazima watu wajue concetration ya chumvi wanazoenda ku deal nazo, uongo dadaangu?

Hahaha....i can't.

Lkn when all is said and done, una point ya msingi. Kiwango cha chumvi lazima kijuulikane awali kabla ya yote; manake mpishi kutujia na kiwango cha chumvi ni gunia zima au kijiko kimoja kunatia mushkeil kwa mlaji
 
Kila la heri, hata mtandaoni wanapatikana waume/wake wa maana tu usikate tamaa kutafuta kile unachokitaka, ila tu uwe muangalifu kuhakikisha watakaojibu ombi lako hawafanyi hivyo kwa kukupotezea muda wako.
 
Mbona nyie mnabishana humu wakati mwayego ameshapata pm. Kadhaa ndiyo maana kakaa kimya ila kwa ushauri wa bure tu dada yangu vuta pumzi na ujipange na kuna njia za kutafuta mume ambazo utawapata wengi na kujichagulia unayempenda kulingana na vigezo vyako ila hapa unaweza kupata makanjanja na wapigaji tu na watakupotezea muda na kukutumia na wanaume wanaijua sanaa vizuri na wanaweza pia kujiweka kwenye sifa unazotaka na wakakupitia na kukuacha uwanjani peke yako.

Ni pm. Kama utapenda nikuelekeze ili upate the right person.
 
Re: ADVERTISMENT

More than serious nahitaji mume wandugu


Wana JF, mimi ni mwanadada na leo nimeona nijitoe muhanga kabisa maana ninahitaji mume/mchumba. Niko tayari kupokea kukosolewa ila kwa yule aliyeko kwenye shinda kama yangu tafadhali ni PM.
Mimi ni Mkristo ninayempenda Mungu na ninahofu ya Mungu ndani yangu, tayari niko kwenye umri wa miaka 33 - 43. Ninatafuta/ Ninahitaji mume mwenye hekima, busara na upendo wa dhati na anaejua definition ya mke nini. Pia kama hajamaliza starehe za dunia za kupenda wanawake asiniandikie - kuna janga la ukmwi sitaki, nataka mtu wa kutulia ili tujenge maisha kwa raha na tabu.

Napenda awe Mkristo aliye na hofu ya Mungu ndani yake. Awe amesoma walau elimu ya chini awe na diploma angalau awe na kabachela hivi kwa umri huo. Awe muajiriwa eidha katika shirika au serikalini kama ana mtoto mmoja sio mbaya wasizidi. Awe tayari kupima ukimwi zaidi ya mara 3. Awe muwazi.


Mimi ni muajiriwa katika shirika

Hili swala naomba tu mchukulie kwangu ni kitu halisi hapa sina utani na wala siko kwa ajili ya kumpotezea mtu muda. Na katika hili pia namshikirisha Mungu nikiamini mume/mke mwema anatoka kwa Bwana. Na pia kwa wale watakao nishauri na kunitia moyo kwenye hili nawashukuru. Kaka zangu popote pale ulipo na unajiona kweli unahitaji mke naomba uni PM lakini kama ni swala la mzaha au kujaribisha naomba usipoteze muda.

Inaonekana Mungu ni mtu!!!!
wewe unatafuta mme, halafu unashirikisha Mungu. Kwani Mungu hawezi kukutafutia? Inawezekana Imani yako ya Kikristo, siyo imara, ndo wale wa bora liende. Kama unamshirikisha Mungu, kwa nini uweke masharti? Mungu akikupatia mlevi, malaya, mbinafsi si utagoma?

Kama unamshirikisha Mungu, toa masharti ili yeyote atakayekuja umkubali. Yawezekana ni kupitia kwako huyo mwanamme ataokoka. Soma kitabu cha hosea, utaona jinsi nabii wa Mungu alivyopewa mke CHANGUDOA, ambaye kila mtu anamjua lakini alioa. P[ia soma vitabu vya wakoritho, waefeso na timotheo, kuna mafundisho yatakuinua kuhusu ndoa.
 
Haya tena, vidume shupavu changamkieni tenda hiyooooooooooooo! Huko mbele isije ikawa tena ooooooooooh mwanamke gani kwanza ulijilengesha publicly......
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom