More than serious nahitaji mume wandugu

Kila la heri Dada Jena. Endelea kusali na kuomba, na Mungu Atakujalia. Umefanya vizuri kuamini kuwa mume anatoka kwa Mungu. Ukiwa na imani hiyo, ninakushauri pia katika maombi yako uzingatie mume aliye na heri na wewe zaidi kuliko sifa ulizotaja tu.
 
Umesema umri kuanzia 33 nakuendelea, mimi nina umri 69 years vp?:bange: utanikubali?
 
Midhali uko tayari kukusolewa, kushauriwa uwe tayari zaidi. Mi si mkristo sitarajii kuku PM. Imenenwa "mpendelee nduguyako lile ambalo unalipenda wewe nafsini mwako". Tafuta contacts za Dr W Slaa (mgombea urais Tz 2010). Huyu anakidhi karibu vigezo vyako vingi na ana shida, Inasemekana amefikia hadi kuazima au kupora wake za watu jinsi alivyo na shida ya mke.

1 Anapenda na ana uwezo wa kukosoa, katika ndoa yenu uta enjoy na hilo, 2 umri wake ni zaidi ya miaka 33. 3 ni Mkristo, ni padri mpenda bwana hata katika Uchaguzi mkuu wakristo wengi waliridhika nae. 4 ana elimu ya kujitosheleza naamini hakusoma shule za Memkwa wala UPE, 5 kajiajiri kisiasa zaidi, posho yake siijui kwa siku ni kiasi gani lakini matanuzi anayo, usishangae posa za awali na pete vinaweza kuletwa kwa helikopta kama kwenu hakuna barabara, wakati wa ndoa yenu mnaweza mkajinunulia gari la kwendea msalani na lingine sokoni n k.

Sikufatilia kabila lake halisi kama ni mtusi au mmasai ila dalili za ubantu na uhutu hana. any way midhali kigezo kwako si tatizo naamini utamtafuta.

Hii isije ikafikirika namfagilia Slaa peke yake ila na wewe pia nataka ukipate unachotafuta

upupu a.k.a pumba.
 
karibu sana jukwaani dada Jena......nakuhakikishia hapa JF utapata mume mwema.....ila ujiandae kwa masihara lakini usikate tamaa....wapo walio single na wana heshima zao....nakutakia kila la kheri na Mungu akubariki katika jambo hili
PretA naona unawapigia chapuo wakaka wa humu JF. mtieni moyo mdada huyu na pia kuweni makini na kumlinda ktk mjadala huu hapa JF kuna watu humu mwezi mchanga hawakawii kuharibu nia safi ya mgeni wetu aliyetujia na shida yake tena anahitaji kuanzisha familia na mwanaJF mwezetu, tumsupport hadi atakapofanikiwa. Pia jena baada ya mafanikio usisite kutupa taarifa ili HARUSI hiyo ifanikishwe na wana JF pia.
 
What a coincedence! Wana Jf heshima kwenu, ni mara yangu ya kwanza kuchangia humu jamvini lakini nakutana na habari njema za mchumba, ki ukweli niko single na ninahitaji mchumba umri miaka 34, nafanya kazi serikalini lakini nina hofu kweli na namna hii ya kupata mchumba ni kweli naweza kupata mtu anayefaa kweli kimaisha? Jamani.. "we are talking about life here! Let's be more than serious!

Anaehitaji mchumba ni JENA sisi tunasaidia kufanikisha shida yake sasa kama kweli wewe nawe ni muhitaji wasilianeni ktk private Massage (PM) Kujua kama yuko serious au vp utapowasiliana nae mkapanga kuonana mkaongea ndipo utakapo jua kama anakufaa au laa, watu wanatafuta wachumba magazetini, facebook hata mtu akikosea simu na kupiga namba ya mwenzake mtu anapandia hapohapo na mwisho wanaweka mambo sawa. Kumbuka hakuna formula ya kukutana na binti au kijana atakayekuwa mume au mke wako mwaweza kutana popote na bado ndoa ikawa nzuri kwenu na kubarikiwa na MUNGU
 
re; pia awe Mkristo.

even me I am dead serious, lakini tatizo naona ni hilo sharti la dini. kama unadhani dini inaongeleka waweza ni PM.
 
Kila la heri Dada Jena. Endelea kusali na kuomba, na Mungu Atakujalia. Umefanya vizuri kuamini kuwa mume anatoka kwa Mungu. Ukiwa na imani hiyo, ninakushauri pia katika maombi yako uzingatie mume aliye na heri na wewe zaidi kuliko sifa ulizotaja tu.

Asante sana na maombi yako ni muhimu zaidi
 
Naendelea kutoa shukrani zangu za dhati kwenu bado nahitaji maombi yenu na Mungu anisaidie nifanikishe
 
Ok sisy zidi kuuomba muweza wa yote atakufanyia njia pasipo na njia, atakupa mume pale utakapoona hakuna mume. lkn let me share with u this experience u'll hardly find ur future husband with at least 70% qualities u desire but once u find 1 with more than 50% of qualities ur desiring opt him owing the fact he/u will adjust to fit the remaining portion as u live together, another quotion is that be aware of liers who may may do anything to win ur body after that they will turn their back from u im with u through prayers once u succeed let us know
 
Mambo Jena, hivi bado haujafanikiwa? pole sana maana uliniahidi utanijulisha ukipata. Ila usijali kama hapa haujapata utapata tu. nakutakiam kila la heri.
 
Hongera sister kwa kuweka vigizo vyako wazi. VIJANA MLIO SINGLE JITOKEZENI. kuwa makini na vijana waleo watataka kuonja na kukutupa watajifanya kama wanahitaji kuoa kumbe wanayao mengine kuwa makini sana
 
wana jf, mimi ni mwanadada na leo nimeona nijitoe muhanga kabisa maana ninahitaji mume/mchumba. Niko tayari kupokea kukosolewa ila kwa yule aliyeko kwenye shinda kama yangu tafadhali ni pm.
Mimi ni mkristo ninayempenda mungu na ninahofu ya mungu ndani yangu, tayari niko kwenye umri wa kati ya 30-33 na ninahitaji mume wa kati ya 33 na kuendelea. Awe na elimu ya kujitosheleza, mfanyakazi au aliyejiajiri. Kabila lolote tanzania na pia awe mkristo. Hili swala naomba tu mchukulie kwangu ni kitu halisi hapa sina utani na wala siko kwa ajili ya kumpotezea mtu muda. Na katika hili pia namshikirisha mungu nikiamini mume/mke mwema anatoka kwa bwana. Na pia kwa wale watakao nishauri na kunitia moyo kwenye hili nawashukuru. Kaka zangu popote pale ulipo na unajiona kweli unahitaji mke naomba uni pm lakini kama ni swala la mzaha au kujaribisha naomba usipoteze muda.


safi sana, naomba mungu akupe hitaji la moyo wako,
naomba ukifanikiwa utujulishe basi wana jf wenzako,
kutoka ndani ya moyo wangu nakupa hongera sana kwa ujasiri uliouchukua, siyo wanawake woote wenye uwezo na ujasiri wa kueleza mahitaji yao na hasa kama linahusiana na mahusiano,
wengi wanakufa /tunakufa na tai shingoni.
 
Wana JF, mimi ni mwanadada na leo nimeona nijitoe muhanga kabisa maana ninahitaji mume/mchumba. Niko tayari kupokea kukosolewa ila kwa yule aliyeko kwenye shinda kama yangu tafadhali ni PM.
Mimi ni Mkristo ninayempenda Mungu na ninahofu ya Mungu ndani yangu, tayari niko kwenye umri wa kati ya 30-33 na ninahitaji mume wa kati ya 33 na kuendelea. Awe na elimu ya kujitosheleza, mfanyakazi au aliyejiajiri. Kabila lolote Tanzania na pia awe Mkristo. Hili swala naomba tu mchukulie kwangu ni kitu halisi hapa sina utani na wala siko kwa ajili ya kumpotezea mtu muda. Na katika hili pia namshikirisha Mungu nikiamini mume/mke mwema anatoka kwa Bwana. Na pia kwa wale watakao nishauri na kunitia moyo kwenye hili nawashukuru. Kaka zangu popote pale ulipo na unajiona kweli unahitaji mke naomba uni PM lakini kama ni swala la mzaha au kujaribisha naomba usipoteze muda.

Nipo apa tayari please,Nangoja ugeuke
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom