More than serious nahitaji mume wandugu

More than serious nahitaji mume wandugu

Dada jena nimeshamwarifu Master detectie nae alikuwa anatafuta chumba mwenye vigezo kaa vyako kabisa.
Itakuwa ni vigelegele na vilegeleg na vificho hapa Jf
 
Wana JF, mimi ni mwanadada na leo nimeona nijitoe muhanga kabisa maana ninahitaji mume/mchumba. Niko tayari kupokea kukosolewa ila kwa yule aliyeko kwenye shinda kama yangu tafadhali ni PM.
Mimi ni Mkristo ninayempenda Mungu na ninahofu ya Mungu ndani yangu, tayari niko kwenye umri wa kati ya 30-33 na ninahitaji mume wa kati ya 33 na kuendelea. Awe na elimu ya kujitosheleza, mfanyakazi au aliyejiajiri. Kabila lolote Tanzania na pia awe Mkristo. Hili swala naomba tu mchukulie kwangu ni kitu halisi hapa sina utani na wala siko kwa ajili ya kumpotezea mtu muda. Na katika hili pia namshikirisha Mungu nikiamini mume/mke mwema anatoka kwa Bwana. Na pia kwa wale watakao nishauri na kunitia moyo kwenye hili nawashukuru. Kaka zangu popote pale ulipo na unajiona kweli unahitaji mke naomba uni PM lakini kama ni swala la mzaha au kujaribisha naomba usipoteze muda.


Tuwasiliane kwa maongezi zaidi naweza kupa huyu wangu ujaribu, ukishindwa unirudishie ukiweza ubaki nae.
 
Chapakazi;1728908]just a question...kwa nini unataka kuolewa kiasi hicho?

Swali: Kwa nini aendelee kusubili wakati mda, nafasi na utayari anao?
 
Dada wanaume wa JF hamna wa kuoa huku..Mtaani,kazini,kanisani kwako hujaona mtu aliyekuvutia. Ukisubiri utongozwe siku hizi utasuburi sana jitoe mhanga umvae yule umpendae ambae unaamini atakua mume bora kwako. Just relax,umri sio mkubwa sana. Wakati wa bwana ukifika utampata mume bora
 
mi nna vigezo vyote elim ya kutosha, kazi nzuri vitega uchumi bwerere, tatizo sasa kweny umri!!!!!!!!!!!!!!!!
kwani tatizo lipo wap ukiolewa na under30? hazalishi? au hafai kua mume? mbona mariah carey kaolewa na bwana mdogo nick na kamtia mimba mapacha
under 30 bado wananuka maziwa
 
Usihofu dadangu kuna watu wapo kimya nadhani wanafikiria wazo lako ili wakutafute. Mi naamini Mungu ni wa wote hivyo nafasi utapata ya kupata kipenzi cha nafsi yako. Am 35 years
 
Uzuri wako ulikuponza ukakataa waoaji kisa hawana mpunga!! Umejirusha na wala bata wenye wake zao, sasa muda umekutupa mkono umetukumbuka, pole na karibu na ukumbuke mchagua nazi hupata koroma. Hongera kwa kukata mshipa wa aibu na kujiweka wazi ksma ya mbuzi!!
 
Wana JF, mimi ni mwanadada na leo nimeona nijitoe muhanga kabisa maana ninahitaji mume/mchumba. Niko tayari kupokea kukosolewa ila kwa yule aliyeko kwenye shinda kama yangu tafadhali ni PM.
Mimi ni Mkristo ninayempenda Mungu na ninahofu ya Mungu ndani yangu, tayari niko kwenye umri wa kati ya 30-33 na ninahitaji mume wa kati ya 33 na kuendelea. Awe na elimu ya kujitosheleza, mfanyakazi au aliyejiajiri. Kabila lolote Tanzania na pia awe Mkristo. Hili swala naomba tu mchukulie kwangu ni kitu halisi hapa sina utani na wala siko kwa ajili ya kumpotezea mtu muda. Na katika hili pia namshikirisha Mungu nikiamini mume/mke mwema anatoka kwa Bwana. Na pia kwa wale watakao nishauri na kunitia moyo kwenye hili nawashukuru. Kaka zangu popote pale ulipo na unajiona kweli unahitaji mke naomba uni PM lakini kama ni swala la mzaha au kujaribisha naomba usipoteze muda.
USPATE SHIDA..
weka picha tuthaminishe...
usije ukawa umekongoroka afu uje kumfia mtu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom