Mo-TOWN
JF-Expert Member
- Oct 11, 2010
- 1,721
- 515
Wana JF, mimi ni mwanadada na leo nimeona nijitoe muhanga kabisa maana ninahitaji mume/mchumba. Niko tayari kupokea kukosolewa ila kwa yule aliyeko kwenye shinda kama yangu tafadhali ni PM.
Mimi ni Mkristo ninayempenda Mungu na ninahofu ya Mungu ndani yangu, tayari niko kwenye umri wa kati ya 30-33 na ninahitaji mume wa kati ya 33 na kuendelea. Awe na elimu ya kujitosheleza, mfanyakazi au aliyejiajiri. Kabila lolote Tanzania na pia awe Mkristo. Hili swala naomba tu mchukulie kwangu ni kitu halisi hapa sina utani na wala siko kwa ajili ya kumpotezea mtu muda. Na katika hili pia namshikirisha Mungu nikiamini mume/mke mwema anatoka kwa Bwana. Na pia kwa wale watakao nishauri na kunitia moyo kwenye hili nawashukuru. Kaka zangu popote pale ulipo na unajiona kweli unahitaji mke naomba uni PM lakini kama ni swala la mzaha au kujaribisha naomba usipoteze muda.
Nimekupata dada nina imani kuwa kweli una hilo hitaji la mume. Na ni vizuri kuwa unamshirikisha Mungu ktk hili.
Ushauri wangu kwako ni kama ifuatavyo.
Kwanza forum hii inaweza kukusaidia kimawazo zaidi kutokana uzoefu wa watu mbalimbali kumpata mtu sahihi kwa maana ya mume.
Kwa vigezo ulivyotoa kwa kweli kabisa ni wazi utapata kwa haraka sana mwanaume si mume?
Swala la mume linahitaji zaidi kuishirikisha roho kuliko nafsi. Hapa namaanisha kuangalia zaidi maswala ya upendo zaidi kuliko muonekano wa nje!
Umesema juu ya awe na kazi elimu ya kutosha etc hivi vyote ni material. Kwa hayo machache nakushauri na nawaomba wadau wengine kutoa ushauri wa kuweza kujua ni yupi atakufaa kama mume na si mwanaume. Naamini kuwa roho mtakatifu amekuwa akikufunulia lakini kwa namna moja au nyingine ujaweza kutambua. Ni wazi kwa umri wako umekutana na vijana wa kiume ambao baadhi walionyesha nia lakini wengine hawakuonyesha. Hapa JF utapa ushauri ikiwa ni pamoja na jinsi gani ya kutambua mapenzi ya kweli. Sikushauri kwa vigezo ulivyoainisha kama viwe ndio ilani yako. Naamini umeshawaona vijana wengi wa aina hiyo lakini kwa namna moja umewaona hawakufai.