Nianze kwa kuwapa pole wagonjwa wote waliolazwa katika hospitali ya rufaa ya Muhimbili.
Nilifika Muhimbili kwa mara ya kwanza siku ya Alhamis tarehe 13.09.2012, majira ya saa nne na nusu asubuhi. Baada ya kutoa maelezo kwa walinzi wakanishauri nisubiri hadi saa sita na nusu mchana ndiyo ningeruhusiwa kumwona mgonjwa niliyeenda kumjulia hali. Nikasubiri.
Muda huo ulipofika nikaingia na kuongoza moja kwa moja hadi wodi ya Mwaisela, namba 2. Hapo nikakutana na kikwazo. Walinzi wawili na muuguzi mmoja walikuwa wanahakiki watu wote wanaopita hilo lango la kuingia wodini. Ilani ikatolewa wenye chakula tu ndiyo wanaoruhusiwa kuingia.
Katika mchujo huo wote waliokuwa na juisi, maji, na matunda wakazuiliwa na hao walinzi. Kwangu mimi ambaye sikubeba chochote ilikuwa ni ngumu zaidi kueleweka. Akaja kijana mwingine aliyeonekana amevalia nguo nadhifu, mkononi kashika Biblia na kitabu cha maombi. Akasema amekuja muda huu kwa ajili ya kufanya maombi kwa Mungu kwa ajili ya mgonjwa wake aliyelazwa wodi hiyo. Akaambiwa "hakuna kuingia, huu ni muda wa chakula kwa wagonjwa, muda wa kuona wagonjwa ni saa kumi".
Baada ya msongamano kupungua nikamfuata Mzee mmoja aliyeonekana anasaidiana na walinzi. Nikamwambia: "baba nina dharula, nahitaji kumwona mgonjwa wangu muda huu ili nijue mahitaji yake, siishi mji huu (Dar) na ninahitaji kufahamu mahitaji yake mapema kabla ya saa kumi." Mzee yule akaniambia nimweleze yule kijana mlinzi aliyenizuia, tena niseme kwa hisia zile zile kama nilivyokuwa namweleza yeye. Nikamsogelea tena yule mlinzi na kumweleza. Yule kijana akaniambia: "nenda, halafu kata kulia". Nikaingia.
Nilipofika mlangoni nikaanza kuona wagonjwa waliolala chini, kwenye korido ya kuingia wodini. Nikasita kwa kudhani labda nimekosea. Nilipoenda mbele kidogo nikatokeza chumba cha kulaza wagonjwa. Wagonjwa walikuwa ni wengi sana. Wamejaa hadi wengine kulazwa chini. Nikaanza kuangaza huku na kule nikimtafuta mgonjwa wangu! Nikamkuta mahali akiwa amelala, chini. Vitanda vimejaa!
Akiwa katika siku ya nne toka afike alikuwa bado hajaelezwa kama atapatiwa matibabu lini. Yuko MOI. Sehemu ya wataalamu bingwa wanaotegemewa kuokoa maisha yake. Hapa hayuko peke yake. Wapo wagonjwa wenzake wengi. Na wengine walikuwa wanalia kwa maumivu makali.
Kwa nini nasema MGOMO BADO UNAENDELEA?
Ilipotimu saa nane kasoro dakika tano kengele ikalia ikiashilia muda wa kuwapa chakula wagonjwa umekwisha. Nikasubiri hadi dakika tano baadaye ndo nikainuka pale sakafuni nilipokuwa nimekaa. Nikaanza kutembea kurudi nilikotoka huku mawazo tele yameniandama.
Baada ya kufika geti la kutokea nikaona maandishi "OFISI YA MAONI/MALALAMIKO YA WATEJA". Nikashtuka! Nikawa nahaingaika moyoni kama niende kutoa maoni au nisiende. Baadaye nikaamua kwamba sitaenda kutoa maoni yangu kwenye kile kiofisi. Nikajiuliza kwani maoni yangu:
Nikafikia uamuzi. "JAMIIFORUMS.COM". Sikuwa na kompyuta siku ile, na simu yangu ndo hizi za bei poa. No intaneti. Nikaondoka na kuchukua dala dala kuelekea Ubungo. Kichwani mawazo tele! Huu mgomo nani anaujua? Hivi sakata lenyewe liliishaje? Dr. Ulimboka yuko wapi? Dr. Mkopi anaendeleaje na kesi yake? Je, ana mashahidi wa aina gani watakaowezesha asipatikane na hatia? Serikali nayo je, imeweza kudhibiti mgomo au imeuahirisha tu? Je, madhara ni yapi?
Lakini pia nikajiuliza hivi chakula hasa ni kitu gani? Je, Watanzania wanaelewa maana hasa ya chakula? FIKIRIA: maji tu, hapana. Machungwa mawili matatu, huingii wodini. Umebeba Juisi, No. Eti "NI KWA WALE WANAOPELEKA CHAKULA TU". Nikawafikiria pia viongozi wa kiroho ambao wanatumia Biblia. Imeandikwa kwamba neno la MUNGU ni CHAKULA cha uzima.
Nikiwa wodini, hata hivyo, wagonjwa na ndugu zao wengi walikuwa wanawalaumu madaktari. Wagonjwa wengine walikuwa wanawalaumu ndugu zao ambao wameshindwa kuchangia HONGO ili wafanyiwe upasuaji kwa wakati. Kwa kweli neno serikali sikulisikia. Pia Mungu alikuwa ametawala kwenye vinywa vya wengi. Nami naungana nao kwa kumwomba Mungu awatie nguvu ya kuvumilia machungu yote wanayoyapata, huku wakitumaini wokovu wake. AMEEN!
Nilifika Muhimbili kwa mara ya kwanza siku ya Alhamis tarehe 13.09.2012, majira ya saa nne na nusu asubuhi. Baada ya kutoa maelezo kwa walinzi wakanishauri nisubiri hadi saa sita na nusu mchana ndiyo ningeruhusiwa kumwona mgonjwa niliyeenda kumjulia hali. Nikasubiri.
Muda huo ulipofika nikaingia na kuongoza moja kwa moja hadi wodi ya Mwaisela, namba 2. Hapo nikakutana na kikwazo. Walinzi wawili na muuguzi mmoja walikuwa wanahakiki watu wote wanaopita hilo lango la kuingia wodini. Ilani ikatolewa wenye chakula tu ndiyo wanaoruhusiwa kuingia.
Katika mchujo huo wote waliokuwa na juisi, maji, na matunda wakazuiliwa na hao walinzi. Kwangu mimi ambaye sikubeba chochote ilikuwa ni ngumu zaidi kueleweka. Akaja kijana mwingine aliyeonekana amevalia nguo nadhifu, mkononi kashika Biblia na kitabu cha maombi. Akasema amekuja muda huu kwa ajili ya kufanya maombi kwa Mungu kwa ajili ya mgonjwa wake aliyelazwa wodi hiyo. Akaambiwa "hakuna kuingia, huu ni muda wa chakula kwa wagonjwa, muda wa kuona wagonjwa ni saa kumi".
Baada ya msongamano kupungua nikamfuata Mzee mmoja aliyeonekana anasaidiana na walinzi. Nikamwambia: "baba nina dharula, nahitaji kumwona mgonjwa wangu muda huu ili nijue mahitaji yake, siishi mji huu (Dar) na ninahitaji kufahamu mahitaji yake mapema kabla ya saa kumi." Mzee yule akaniambia nimweleze yule kijana mlinzi aliyenizuia, tena niseme kwa hisia zile zile kama nilivyokuwa namweleza yeye. Nikamsogelea tena yule mlinzi na kumweleza. Yule kijana akaniambia: "nenda, halafu kata kulia". Nikaingia.
Nilipofika mlangoni nikaanza kuona wagonjwa waliolala chini, kwenye korido ya kuingia wodini. Nikasita kwa kudhani labda nimekosea. Nilipoenda mbele kidogo nikatokeza chumba cha kulaza wagonjwa. Wagonjwa walikuwa ni wengi sana. Wamejaa hadi wengine kulazwa chini. Nikaanza kuangaza huku na kule nikimtafuta mgonjwa wangu! Nikamkuta mahali akiwa amelala, chini. Vitanda vimejaa!
Akiwa katika siku ya nne toka afike alikuwa bado hajaelezwa kama atapatiwa matibabu lini. Yuko MOI. Sehemu ya wataalamu bingwa wanaotegemewa kuokoa maisha yake. Hapa hayuko peke yake. Wapo wagonjwa wenzake wengi. Na wengine walikuwa wanalia kwa maumivu makali.
Kwa nini nasema MGOMO BADO UNAENDELEA?
- Wagonjwa wameongezeka na kufikia hatua ya kulala hadi kwenye korido. Kasi ya kuwatibu ni ndogo.
- Wale wanaoweza kutoa rushwa wanalazimika kulipia operation kwa siri. Unaweza kulipia shilingi ngapi, lini, kwa nani ndicho kigezo kwa sasa. Siwasingizii madaktari.
Ilipotimu saa nane kasoro dakika tano kengele ikalia ikiashilia muda wa kuwapa chakula wagonjwa umekwisha. Nikasubiri hadi dakika tano baadaye ndo nikainuka pale sakafuni nilipokuwa nimekaa. Nikaanza kutembea kurudi nilikotoka huku mawazo tele yameniandama.
Baada ya kufika geti la kutokea nikaona maandishi "OFISI YA MAONI/MALALAMIKO YA WATEJA". Nikashtuka! Nikawa nahaingaika moyoni kama niende kutoa maoni au nisiende. Baadaye nikaamua kwamba sitaenda kutoa maoni yangu kwenye kile kiofisi. Nikajiuliza kwani maoni yangu:
- atakayeyapokea ni nani?
- atakayeyachambua ni nani?
- atakayeandaa ripoti ni nani?
- atakayepokea ripoti ni nani?
- atakayefanyia kazi mapendekezo ya ripoti ni nani?
Nikafikia uamuzi. "JAMIIFORUMS.COM". Sikuwa na kompyuta siku ile, na simu yangu ndo hizi za bei poa. No intaneti. Nikaondoka na kuchukua dala dala kuelekea Ubungo. Kichwani mawazo tele! Huu mgomo nani anaujua? Hivi sakata lenyewe liliishaje? Dr. Ulimboka yuko wapi? Dr. Mkopi anaendeleaje na kesi yake? Je, ana mashahidi wa aina gani watakaowezesha asipatikane na hatia? Serikali nayo je, imeweza kudhibiti mgomo au imeuahirisha tu? Je, madhara ni yapi?
Lakini pia nikajiuliza hivi chakula hasa ni kitu gani? Je, Watanzania wanaelewa maana hasa ya chakula? FIKIRIA: maji tu, hapana. Machungwa mawili matatu, huingii wodini. Umebeba Juisi, No. Eti "NI KWA WALE WANAOPELEKA CHAKULA TU". Nikawafikiria pia viongozi wa kiroho ambao wanatumia Biblia. Imeandikwa kwamba neno la MUNGU ni CHAKULA cha uzima.
Nikiwa wodini, hata hivyo, wagonjwa na ndugu zao wengi walikuwa wanawalaumu madaktari. Wagonjwa wengine walikuwa wanawalaumu ndugu zao ambao wameshindwa kuchangia HONGO ili wafanyiwe upasuaji kwa wakati. Kwa kweli neno serikali sikulisikia. Pia Mungu alikuwa ametawala kwenye vinywa vya wengi. Nami naungana nao kwa kumwomba Mungu awatie nguvu ya kuvumilia machungu yote wanayoyapata, huku wakitumaini wokovu wake. AMEEN!