Mohammed Dewji kwanini haendi bungeni?

Mohammed Dewji kwanini haendi bungeni?

Nyie mnatunga katiba yenu, sasa yeye inamhusu nini? mwacheni bana aendelee na biashara zake!! hizi chokochoko za nini wakati waliomchagua wapo kimya.
 
yupo kwenye biashara zake.ubunge ni kwa ajili ya kufacilitate biashara zake.
 
Ukiona mbunge anajiamlia tu kutokwenda bungeni na hakuna hatua yeyote inachukuliwa na ofisi ya bunge ujue yeye ni zaidi ya bunge, hebu jaribu wewe usiende kazini siku moja tu bila taarifa yoyote uone kitakachotokea.
 
Kwenye wabunge wote umemwona Mohammed dewji tu?
Kama kuna kitu unataka akufanyie sema tu ili
nikupe kontakti zake.

Wee Dewji alikufanyia nini? hebu tupatie elimu kidogo
 
Umekuwa ni utaratibu wake kutohudhuria,

kufika bungeni kusalimia wenzake na kukimbia kwenye vikao vya kawaida vya Bunge, sasa na Bunge la Katiba haendi, kama anaona biashara zake ni za maana zaidi kwanini aligombea Ubunge? Wananchi wake wanawakilishwa vipi katika masuala ya muhimu?

Yawezekana huyu ni mbunge mzigo kuliko wengine. na hata asipoenda, siku anapoenda huko akigawa kidogo hata vigogo wa Bunge wanaufyata.

ifike mahali watanzania wajue hili

Labda kwakuwa yeye hahitaji posho.. na hana cha kuchangia.
 
atakuwa ame mtuma Ndassa au Proxy wake aka mwakilishe, yeye anaingiza mamilioni , hawezi kuziacha kufuata laki 3 ya Ndassa
 
Mwenzake alivyoona amepata alichohitaji akaziita siasa uchwala na sasa ameingia kwenye orodha ya Forbes, na huyu anapigania miaka isiyozidi miwili aingie huko. We na mimi tuendelee tu kukaa kwenye keyboards lakini tusisahau kuwa 'wajinga ndio waliwao'.
 
Nani anawawakilisha wananchi wake katika chombo cha kutunga sheria, kuishauri serikali na kuihoji?
kuna post moja kutoka Kawe ilisema kazi ya mbuge ni pamoja na roby miladi ya maendeleo na kuipeleka eneo lako huyu jamaa kwa kutumia mipesa yake anaweza sana kuroby maendeleo ya sehemu zingine na kuhamishia Singida na wanasingida wakafurahi mpaka gego la mwisho wakiamini mbunge wao kafanya yote hayo kwa pesa zake kumbe ni kodi zetu!!!!!
 
hako kajamaa kana jibu jibu utumbo kanafikiri wote wanashida kama yeye mpaka kapewa namba asambaze?,,
kama mtu haendi mjengoni alafu asisemwe yee nani?,JK mwenye mpini wa2 wanamsema sembuse yeye.
kama hela tunazo sio wewe mpaka utoe hiyo tigo <no yake>ndo upate pesa.bwa mdogo usirudie
 
sioni kama kuna tatizo kama matatizo ya wananchi wake anayatatua. ila kama wananchi anaowawakilisha hawa benefit chochote hapo ndo kuna shida kubwa ya yeye kuonekana mzigo tena wamisumari na chama chake kinatakiwa kumuambia
Anatakiwa awawakilishe wananchi waliomchagua bungeni na si vinginevyo.
Alichaguliwa awe muwakilishi sio muhisani.
Wabunge wote wakisema wanatatua matatizo ya wananchi wao bila kufika bungeni unafikiri itakuwaje?
 
Back
Top Bottom