MO haidai Simba hata shilingi moja, inamdai yeye

MO haidai Simba hata shilingi moja, inamdai yeye

Bila MO simba ni sawa na Maji Maji
Sio mo anaisaidia Simba na Simba inamsaidia mo pia (symbiosis). Yanga alitoka Abbas Gulamali akaja Manji Yusuf na Manji aliondoka akaja GSM. Hata mo akiondoka atakuja tajiri mwingine, usihofu aloo. Shida inaweza kuwepo kwa muda mfupi tu kabla ya kumpata kibopa mwingine msua zaidi.
 
Jidanganye.
Sio kwamba Rage aliropoka tu kuwaita mbumbumbu mashabiki wa Simba. Kuna mashabiki wa Simba wanadhani mo kaitoa mbali Simba, Simba ilikuwepo tangu 1936. Ni Simba iliyomtoa mbali mo na familia yake.

Mo pia kashajua kuwa mashabiki wa Simba kuna mbumbumbu wengi, ndiyo maana kila pesa anayotoa anahesabu kuwa anaikopesha Simba na anataka mkopo huo uidhinishwe na club ya Simba. Yaani ni sawa na mtu amenunua keki na kuila imeisha kisha anadai keki yake kwa muuzaji.

Mkataba wa Simba na Mo ni yeye kutoa fedha bila idadi na Simba imtangaze mo bila idadi (reciprocal). Yaani kama mfadhili atatoa fedha zaidi kwenye kusajili wachezaji wazuri, mishahara mizuri na bonus zaidi na Simba itamtangaza zaidi mo ndani na nje ya nchi. Mo alifanya kazi yake ya kutoa pesa na simba ilifanya kazi yake ya kutangaza bidhaa za mo Tanzania, CECAFA, CAF mpaka FIFA mpaka Simba ikamleta Rais wa FIFA hapa akashikana nae mkono. Hii maana yake mo hadai kwa simba na Simba hadai kitu kwa mo. Kama wakiachana kila mtu ataondoka kwa amani bila kudaiana kitu.

Elimu kama hii inayo Rage tu na watu wachache sana pale Simba. Akina Kisugu na mhindi wa Simba hawana elimu kama hii, wanadhani mo anaidai sana Simba na akiondolewa pale Simba lazima irudishe hela ya mo aliyotoa utadhani kuwa Simba haikumtangaza mo hadi kwenye makalio ya mashabiki wao. Yaani ni sawa na kusema na Mo arudishe Simba alivyotangazwa Tz, CECAFA, CAF na FIFA.
 
Haiishi tu Mo kuidai simba billions of shilings! Yeye na familia yake ndiyo wamiliki halali wa timu ya simba. Kama huamini muulize Mangungu.
Mo ana 49%, Gsm ana 100% Yanga na Mwenyekiti kawapa awasaidie, Na kiwanja ana 50% kwa mkataba wa milele Amina.
 
Back
Top Bottom