Mo Dewji nakuheshimu, ila unakoelekea sasa utaharibu na utaanza hata Kutukera na Sisi tunaokubali 'Kutukanwa' kwa ajili ya Kukutetea Mitandaoni

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,805
109,478
Mo Dewji leo utanisamehe sana Mimi GENTAMYCINE ambaye nina tabia ya kutopenda Unafiki, Kumnyenyekea Mtu, Kujipendekeza kwa Mtu au hata Kumuogopa Mtu hata kama ni Msomi sana su Tajiri mno na hata Wazazi wangu, Ndugu na Marafiki zangu wanalijua hili kwani ndivyo nilivyoumbwa na sitobadilka hadi Umauti wangu.

Mo Dewji Wewe ni Mwekezaji wa Klabu yetu ya Simba ila hujapewa Mamlaka ya Kumiliki ( Kuzimiliki ) Akili zetu ambao kuna wengine tunajua tuna Uwezo mkubwa wa Akili Kukuzidi ila labda ulichotuzidi ni Pesa, Mali ( Utajiri ) na bahati tu.

Mo Dewji ni Mimi huyu huyu GENTAMYCINE nilianzisha Uzi hapa JamiiForums kukutaka usijiingize kabisa katika Mtego wa Kujibizana na aliyekuwa Msemaji wetu Haji Manara na badala yake utuachie Sisi Mashabiki tutapambana nae kwani tunamjua na tunammudu.

Mo Dewji kwani Mchezaji Clatous Chota Chama akimpongeza 'Adui' yako wa sasa Haji Manara Wewe unapungukiwa na nini? Kwanini unapenda sana kutaka 'Kunyenyekewa' na wana Simba SC wote kana kwamba Wewe ni Mungu Mtu?

Mo Dewji hivi Matajiri wakubwa Wenzako kama akina Aliko Dangote, Patrice Motsepe, Moise Katumbwe Chapwe, Said Salim Bakhressa, Roman Ibrahimovic, Carlos Slim, Bill Gates na Roca Fella nao wana ' Utoto' huu kama wako?

Sasa leo hii Wewe Tajiri Mo Dewji ukianza kuwa na Uswahili wa Kujibizana na Haji Manara au wale 'wanaompenda' je, Sisi Mbayuwayu ( Masikini ) kama akina GENTAMYCINE tufanyeje? Nisikufiche Mo Dewji unaboa na umeniboa mno tu.

Mo Dewji hukupewa Dhamana ya Kuwekeza Simba SC ili utunyanyase, tukuogope, utupande Vichwani, utufanye utakavyo na tukuone Mungu Mtu sawa? Na usidhani ikitokea 'ukasusa' Simba SC na Kuondoka basi tutaabika mno kwani kwa 'Brand' ya Simba SC ya sasa hata ukijitoa leo wapo Matajiri wengine wakubwa tu Mwenyezi Mungu atatuletea na Simba SC yetu itaendelea vyema tu.

Mo Dewji Mwenyezi Mungu hakukupa huo Utajiri wako ili unyanyasie Watu, tukutukuze au tukulambe Miguu bali umepewa Utajiri huo mkubwa ili ushirikiane na Sisi Masikini ( Mbayuwayu ) akina GENTAMYCINE wenye Akili Kubwa kukuzidi ili kwa pamoja tushirikiane na tuipatie Mafanikio ya Uwanjani na nje ya Uwanja Simba SC yetu sawa?

Mo Dewji aliyekuwa Msemaji wa Simba SC Haji Manara alipokusema ( alipokunanga ) Wiki hii wengi ( GENTAMYCINE nikiwemo ) tulikataa Kumuamini ila kupitia huu Upuuzi wako kwa Mchezaji Clatous Chota Chama nami sasa niseme tu kuwa kwa 65% naanza Kuyaamini baadhi ya Madai ya Haji Manara juu yako.

Mo Dewji hivi hujifunzi tu hata kwa Msanii Nasib Abdul ( Diamond Platinumz ) ambaye kutwa ananangwa ( anasemwa ) vibaya tena hadi 'Kudhalilishwa' na akina Mwinjaku lakini Kijana wa Watu ( Diamond ) hajathubutu hata Kujibizana nae Mitandaoni na katika Vyombo vya Habari. Ina maana hata Diamond Platinumz anakushinda Uvumilivu na Uungwana dhidi ya Maadui ( Enemies ) na Watesi ( Critics ) wako?

Mo Dewji nakuheshimu mno ila kwa hili ulilolifanya nisamehe sana ila niseme tu umekosea zaidi na sidhani kama Tajiri wa Mfano wako anatakiwa kuwa na 'Vijitabia' vya Utoto Utoto, Ukike Kike na Uswahili pamoja na Ushambenga kama unavyoanza kutuonyesha.

Bado hujachelewa Kubadilika na bado GENTAMYCINE sijakata Tamaa juu yako na Kukuheshimu ila nakuomba tu Jitathmini na fanyia Kazi haya niliyokusema na Kukushangaa nayo hapa. Ni kweli wana Simba SC tunakupenda na Kukuhitaji kwa Mafanikio makubwa yaliyotokana na Uwekezaji wako mkubwa ila hatutaki utunyanyase, utupelekeshe utakavyo na utufanye tukuone Wewe ni Mungu wakati Mimi najua Mungu ni Mmoja tena Yule wa Ibrahim, Isaka na Yakobo kwa Sisi Wakristo.

ID yangu hii Dawa ya GENTAMYCINE ( ANTIBIOTIC ) inayotibu Matatizo Sugu ya Mwilini hivyo naamini kwa haya niliyokuambia hapa yatakuponya nawe pia na utabadilika na uanze kuishi Kiustaarabu kama Matajiri wakubwa Wenzako duniani.

Hakuna aliye juu ya 'Klabu' hii ya Simba.
 
Huyu Mo si anyamaze huu upepo mchafu upite mbalimbali Mambo yaendelee maana sasa anajizalilisha na kuonyesha true color yake Hadi Manara anaonekana yuko sahihi, kanisikitisha sasa kwa hii tabia yake anakua ka wanawake wa uswahili bwana, no classy at all. Hii issue ni yeye anaikuza si atulie huu upepo utulie ndo afanye yake.
 
Alichofanya mo waweza sema ni mahaba ya moyo wake na simba lakin kiuhalisia wote wanapaswa kujihoji kati ya mo na ccc
 
Kila penye jumuiya uongozi ni kitu muhimu uongozi wa kiafrika ni pesa na umaarufu inasikitisha sana kuona simba hawakuwa na maandalizi ya wacho kianzisha si viongozi wanachama shabiki hata wachezaji kila mtu ana lake
 
Mo ni mswahili tu
hata wakati ametekwa ni halali kabisa
coz hatuwezijua na nao waliomteka aliwafanyia nini kibaya!
Wachezaji ni watu wa kupita tu Leo yupo hapa na kesho yupo kule!
Unamuuliza mchezaji eti Manara alilipa hela ya uhamisho wako?
Yaani nawaza hata kwenye kampuni yake
Kwa mwenendo huu
Je hao wafanyakazi si wana shida sana?
Wakati fulani watu wanaficha makucha yao
Ila kamwe hawawezi kuyaficha milele
Huwa ni swala tu la muda, ataonesha tabia yake halisi!

Hii ni baada ya ile check ya 20B!!
ana nguvu sasa!
Basi wengi wataamini kuwa ni kweli simu ya kumzuia Diamond ilipigwa!
Simba sc ni chama kubwa kwa sasa hadi nje matajiri wameiona!
Hivyo hata wakiambiwa waje wawekeze basi watakimbizana kuja hadi simba sc waseme baaaaasiii!
Hata akina Roman Abro wa Chelsea sc hajawahi kuingilia maisha binafsi ya mchezaji!
Hasa anapoongelea mambo yake binafsi na watu wake au marafiki!
Fatilia mishahara ya wafanyakazi wa Mo. Hasa viwandani na madereva wa magari yake utaelewa Mwamedi ni mtu wa aina gani. We fatilia mishahara ndio utaelewa vizuri.
 
Back
Top Bottom