PreGE2025 Mnyika: Msajili aseme amempa Siku ngapi Makalla madai ya CHADEMA kununua Virusi vya Ebola

PreGE2025 Mnyika: Msajili aseme amempa Siku ngapi Makalla madai ya CHADEMA kununua Virusi vya Ebola

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
4,783
Reaction score
14,975
John Mnyika, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) amemtaka Msajili wa Vyama vya Siasa kusema hatua alizochukua dhidi ya Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Amos Makalla aliyedai CHADEMA inachangisha fedha kwenda kununua Virusi vya Ebola na Epox

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Soma Pia: Makalla: CHADEMA wanataka kuingiza Ebola Tanzania ili wazuie uchaguzi!

Amesema hayo wakati akifungua mafunzo ya Uongozi kwa Viongozi wa BAWACHA na BAVICHA kutoka Kanda ya Kusini yanayofanyika Masasi, ambapo amembatana na Mkurugenzi wa Mafunzo, Oganaizesheni na Uchaguzi, John Pambalu.
 
Bunge pia limekuwa ni Rubber Stamp na Ofisi ya Msajili pia ni Rubber Stamp, CCM wameua taasisi zote na kuzifanya Taasisi Chawa wa Mama.
 
Ukitafuta chimbuko la haya mambo utagundua Mwalimu Nyerere ndo alituchoma
Hapana. Wewe utakuwa hukuelewa aliyo kuwa akiyasimamia; siyo haya yanayo fanyika leo hii.
Inanikumbusha Mwalimu Nyerere kwenye kitabu chaTujisahihishe.

Ukurasa wa 5
Huo ukurasa wa 5 unasemaje mkuu, labda hayo yange msaidia huyu mkuu 'chief04' kuelewa tofauti kubwa iliyopo sasa kati ya CCM hii na hiyo ya wakati wa Mwalimu Nyerere.
 
"Mambo haya yanafanyika ili kuitoa CHADEMA katika agenda ya Taifa ya NO REFORMS NO ELECTION": Mnyika
 
John Mnyika, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) amemtaka Msajili wa Vyama vya Siasa kusema hatua alizochukua dhidi ya Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Amos Makalla aliyedai CHADEMA inachangisha fedha kwenda kununua Virusi vya Ebola na Epox

Amesema hayo wakati akifungua mafunzo ya Uongozi kwa Viongozi wa BAWACHA na BAVICHA kutoka Kanda ya Kusini yanayofanyika Masasi, ambapo amembatana na Mkurugenzi wa Mafunzo, Oganaizesheni na Uchaguzi, John Pambalu.
😅😅hahah
 
Mnyika siku hizi kachangamka sana,nafikiri chairman aliyetoka alimnyima nafasi ya kua huru kushambulia kama wa sasa amemuacha aifanye kazi yake kwa uhuru kabisa.
Bila shaka Dr.Slaa atakua tayari kumpa uzoefu zaid Ili awe moto kama enzi zake
 

View: https://youtu.be/DIC_ozvSnF0?si=_mnodMkKoiaxJMuU
➡Ofisi ya Msajili wa vyama siasa imeendelea kujaribu kuendelea kuichokonoa CHADEMA kwa kumtaka katibu mkuu kujibu hoja za yule mwanachama wa CHADEMA aliyelelamika kwamba kikao cha Baraza Kuu kilichothibitisha uteuzi wa katibu mkuu, manaibu katibu mkuu (Tanganyika na Zanzibar) na wajumbe wateule wa kamati kuu uliofanywa na Mwenyekiti Tundu Lissu hakikuwa na akidi inayotakiwa ya 75% ya wajumbe wote na hivyo katibu, manaibu makatibu hao na wajumbe wateule hao wa kamati kuu ni batili, si halali....

➡Katibu mkuu wa CHADEMA John Mnyika ktk video hiyo anamjibu mwanachama huyo na msajili wa vyama vya siasa kupitia vgombo vya habari kwa kuwa yeye msajili naye katoa madai yake hayo kupitia njia hiyo hiyo...

➡Aidha Katibu Mkuu John Mnyika, amemtaka MsajilI wa vyama vya siasa aeleze umma wa Watanzania amechukua hatua gani kwa CCM ambacho kimevunja katiba yake waziwazi huku wanachama wake wakilalamika kwa kitendo hicho cha kumpitisha Bi Samia Suluhu Hassan kuwa mgombea u - Rais 2025 na Dr Emmanuel Nchimbi kuwa mgombea mwenza wake kinyume cha taratibu na katiba yao....

➡Na mwisho, amemtaka Msajili wa vyama vya siasa aueleze umma wa Watanzania hatua alizomchukulia Katibu wa itikadi na uenezi wa CCM Amosi Makalla kwa kitendo chake cha kuropoka uongo hadharani kuwa CHADEMA kupitia kampeni yake ya TONE TONE ina mpango wa kutumia fedha hizo kwenda kununua virusi vya Ebola na M- POX na kuviingiza nchini....

➡Amesema, kauli hii ya Amos Makalla ni uongo wa kijinga, kipuuzi na unahatarisha usalama wa taifa kwa sababu umezua taharuki kwa wananchi na kwa wageni wanaingia nchini kwetu kwa shughuli mbalimbali ikiwemo utalii, biashara nk

➡Mwisho, Katibu Mkuu John Mnyika amewataka wanachama na wana CHADEMA na wapigania mabadiliko kutokukubali kuondolewa na kuhamishwa kutoka kwenye focus ya mapambano ya kupigania mabadiliko ya mifumo ya uchaguzi kupitia katiba, sheria na kanuni ili kuhakikisha nchi inakuwa na katiba, sheria na kanuni bora na za haki kwa watu wote ktk kuhakikisha tunakuwa na chaguzi za WAZI, HAKI, HURU na za KUAMINIKA ili kila mwanachi aone kura yake ina thamani, inahesabikia na inahesabiwa ktk kuchagua viongozi wao...

Mtazame na msikilize ☝🏻☝🏻☝🏻
 
Bunge pia limekuwa ni Rubber Stamp na Ofisi ya Msajili pia ni Rubber Stamp, CCM wameua taasisi zote na kuzifanya Taasisi Chawa wa Mama.

Imagine, nchi inaongozwa na Karani wa Masijala, Waziri Mkuu mwalimu grade A na Naibu Waziri Mkuu naye Mwalimu Grade A. No wonder .... Mpango kaamua kuachia ngazi.
 
Back
Top Bottom