Mnyika is the most brilliant lawmaker!

Mnyika is the most brilliant lawmaker!

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
52,153
Reaction score
162,570
Naomba niseme tu, Mh.Mnyika, ni mbunge bora katika utungaji wa sheria katika bunge letu.

Tuna mawaziri na wabunge wasomi lakini Mnyika japo hana elimu kama wao, ame-prove to be the best lawmaker.

Huyu Mh. ana uwezo mkubwa wa kujenga hoja na kutetea hoja zake katika upitishaji wa vifungu vya sheri ila wingi wa wabunge wa CCM ndio kikwazo cha nchi hii kupata sheria bora.

Kwakweli he is very impressive awapo ndani ya Bunge.

Ningekuwa na uwezo, huyu Mh.ningemzawadia gari "brand new".

Tujenge utamaduni wa ku-pick the best legislator na kuwapa tuzo ili kuwatia moyo wabunge wanaotambua wajibu wao kwa umma.

Kwa wanaofuatulia Bunge, wataukubaliana na mimi ila kwa wale wenye wivu, wataleta hapa kejeli na siasa tu and nothing else.
 
Kweli mkuu na Kinacholiangusha Taifa ni Ushabik wa kinafk has kweny haya Maswal ya Msing watu hawatak kukubaliana na Ukweli....
 
siku tukiweka ushabiki wa kisiasa pembeni tutasonga mbele...ila kwa sasa tutaendelea kusikia michango na mapendekezo mazuri ambayo yatakuwa yana bezwa na walioko madarakani
 
Yaani umezungumza kitu kilichotulia sana, Mnyika ni mmoja ya wabunge wachache wa bunge hili wanaojua wajibu wa mbunge haswa. Sio mara moja au mbili namuona akipambana kwenye vifungu vya sheria na huwa anapambana mpaka dakiki ya mwisho na huwa anajenga hoja zenye mantiki. Huwa anashindwa kwa ule wingi wa ndioo na sio hoja.

Kwa uwezo huo wa Mnyika umenifanya mimi na wenzangu waelewa kuangalia uwezo wa mtu na sio elimu yake ya darasani. Kwa mfano hebu tuangalie tu watu wenye elimu ya degree pale bungeni wenye uwezo wa kujenga hoja kama Mnyika achia mbali hao MaDr na Maprof. kwahiyo elimu kwetu haina tija kwa kiwango kile bali ni sifa mojawapo tu ya mmbunge, ila uongozi kwetu ni uwezo. Nakushukuru mleta mada kwa kuliona hilo.
 
Nadhani ungeanza na Zitto Kabwe maana ni mbunge pekee katika bunge linaloendelea aliyepeleka hoja nyingi bungeni zenye masilahi kwa taifa na kupelekea mawaziri na viongozi kadhaa kujiuzuru kwa nyakati tofauti katika kipindi chake cha miaka 10 bungeni.

Hata suala la ESCROW ambalo CDM wamelitumia sana kujiuza kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa, Mnyika alikuwa wapi wakati Kafulira na Zitto wanahangaika nalo na CAG! CDM walikuja kudandia na kutaka eti kutoka bungeni baada ya kuona hiyo issue inaweza kuwa boost kisiasa!
 
Watunga sheria wanaitwa learned brothers and Sisters huyo mnyika hata degree hana.Acha kudhalilisha fani ya wanasheria.
 
Anamzidi mpaka AG kweli the man is very serious leo nimemkubali zaidi japo hakuwa na msaada ila kaonesha yuko sawa, pia kuna siku msigwa alisema kuna 20%ya wabunge hawapaswi kuwepo mjengoni ni kweli tena niwale wa ndiyoooooooooo
 
Simply brilliant! Man I can not agree more with you! single handedly JM anaiwakilisha kambi ya upinzani kwa weledi mkubwa; save for what is called "the irony of big numbers"; wabunge wote wa CCM kuu na CCM B wenzao kwao ni business as usual!! kulinda status quo; kuhakikisha wanajihami wasiwajibishwe kwa madudu yao; lakini wakae wakijua kuna siku kutakucha; haiwezekani usiku ukabaki usiku tu; hata kule Iceland msimu wa usiku mrefu huwa unakwisha kunakucha; na hapa kutakucha tu. Well done John Mnyika; Nchi hii ina deni kubwa sana kwako kwa juhudi zako, your efforts will never be in vain.
 

Beyond any reasonable doubt...

Watanzania watumie fursa adhimu ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, kuchagua wabunge wengi zaidi watakaotimiza wajibu na majukumu yao inavyotakiwa kama wanavyofanya wabunge wengi wa CHADEMA na upinzani kwa ujumla hasa kupitia UKAWA.

Wajibu huo uende mbali kwa kuhakikisha tunaiondoa CCM madarakani ili hatimaye tuweke madarakani uongozi ambao utazingatia kuwa mchakato wa kutunga sheria (fair laws) unapaswa kuwa kwa ajili ya manufaa ya wananchi na nchi, kuanzia miswada inapoanza kuandaliwa na kupitia hatua takriban 8 ikiwemo kwenye Baraza la Mawaziri (chini ya rais), mjadala Bungeni na kisha kwa Rais kwa ajili ya assent.
 
Nadhani ungeanza na Zitto Kabwe maana ni mbunge pekee katika bunge linaloendelea aliyepeleka hoja nyingi bungeni zenye masilahi kwa taifa na kupelekea mawaziri na viongozi kadhaa kujiuzuru kwa nyakati tofauti katika kipindi chake cha miaka 10 bungeni.

Hata suala la ESCROW ambalo CDM wamelitumia sana kujiuza kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa, Mnyika alikuwa wapi wakati Kafulira na Zitto wanahangaika nalo na CAG! CDM walikuja kudandia na kutaka eti kutoka bungeni baada ya kuona hiyo issue inaweza kuwa boost kisiasa!

Mkuu...unaweza kuwa tayari tukuwekee nakala ya hotuba ya Waziri Kivuli wa Nishati na Madini John Mnyika, bajeti ya mwaka 2014/2015? Kama huwa hauoni soni kuaibika kwa kusema uongo!
 
Watunga sheria wanaitwa learned brothers and Sisters huyo mnyika hata degree hana.Acha kudhalilisha fani ya wanasheria.

Si sahihi ili uwe mtunga sheria lazima uwe na degree na hata wewe kama mwanasheria hujui kigezo cha kikatiba cha mtunga sheria kinasemaje ili apate sifa ya kuwa mtunga sheria. Tuache ushabiki kwenye jema lazima tupongezane .
 
Watunga sheria wanaitwa learned brothers and Sisters huyo mnyika hata degree hana.Acha kudhalilisha fani ya wanasheria.

Alas! What a low comment. Mkuu East African Eagle, unajua majukumu ya mihimili ya serikali kweli? Somo hili linafundishwa ngazi ya shule ya msingi. Naomba kuamini kuwa umepitiwa tu mkuu, vinginevyo huu mjadala utakuwa unakuzidi kimo kabisa na unahitaji kueleweshwa zaidi ili uwe mchangiaji mzuri hata kama unapinga kilichoandikwa na mwanzisha thread.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu...unaweza kuwa tayari tukuwekee nakala ya hotuba ya Waziri Kivuli wa Nishati na Madini John Mnyika, bajeti ya mwaka 2014/2015? Kama huwa hauoni soni kuaibika kwa kusema uongo!

Hotuba unaweza kuipata kwenye website ya bunge, labda ulitaka kusema nini, why can't you be straight?
 
Back
Top Bottom