Mnyika anaandaliwa kumrithi Mbowe CHADEMA?

Msanii

Platinum Member
Jul 4, 2007
22,606
29,753
Kwanza nimpe kongole mdogo wangu John Mnyika kwa kuteuliwa kisha kupitishwa na Baraza Kuu Chadema kishika nafasi ya Ukatibu Mkuu Taifa wa chama hiko.

Anapokea kijiti kutoka kwa Vicent Mashinji ambaye alionekana ni mgeni kwenye Chama na siasa akitokea kwenye taaluma ya udaktari. Wadadisi wengi wa siasa walimuona Mashinji kama kijana wa aliyekuwa Mgombea Urais 2015 kupitia CHADEMA mhe. Lowassa ambaye sasa amerejea CCM.

Jina la John Mnyika halikupewa uzito sana katika nafasi hiyo ingawa watabiri wa siasa waliona uwezekano wa yeye kupokea kijiti kutoka kwa Mashinji ulikuwepo kidogo. Safari ya Mnyika kwenye siasa inaanzia tangu akiwa mwanafunzi Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam ambapo yeye na mwenzake Zitto walionekana ni vijana zao halisi la siasa wakilelewa na kuimarishwa upande wa Upinzani. Naweza kisema kwamba Mnyika ni mpinzani wa kweli kwa sababu hakuwahi kushiriki siasa za Chama cha CCM.

Wakati mwenzake Zitto akiungana na prof. Kitila Mkumbo na wenzake kutaka kumpindua Mbowe kwenye chaguzi za ndani CHADEMA, Mnyika hakuonekana kuunga mkono vuguvugu hilo huku akionyesha uaminifu wake kwa Mbowe na kundi lake.

John Mnyika anazifahamu siasa za upinzani, hivyo ni rahisi kwake kuimarisha ngome za CHADEMA katika kipindi chake cha Ukatibu Mkuu Taifa. Anajua kujenga hoja pia ni rahisi kwake kuwashawishi vijana kufuata mfano wake.

Nafasi aliyopewa, inamuweka karibu sana na Mbowe hivyo inawezekana CHADEMA wameona turufu ya Mnyika kuweza kuja kuwa kiongozi mkubwa wa CHADEMA siku za usoni.

Je una maoni gani kwenye hili la kumrithi Mbowe siku za usoni?
IMG_20191220_111357.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
..Dr.Mashinji alikuwa miongoni mwa wataalamu waliokuwa wakiishauri cdm wakati wakiandaa ilani yao ya uchaguzi.

..siyo kati ya waliojiunga na cdm kwa kusombwa na mafuriko ya Lowassa.

..Dr.Mashinji amefanya kazi kubwa ktk mazingira magumu. Nadhani amesaidia kuweka msingi kwa CDM kujiendesha kama taasisi.

..lingine ni kwamba amejitahidi ku-empower wanachama wengi zaidi, na hakujifanya kuwa mkubwa zaidi ya chama.
 
Ukimya wa John Mnyika hapo katikati uliwatia hofu sana wengi waliokuwa na matarajio makubwa kwake kabla ya ukimya ule.

Lakini, kwa vile ndani ya chama, wanaofahamu vizuri zaidi mienendo yake, na pengine sababu za ukimya ule bado wanaimani kubwa juu yake, hata walio nje inalazimu waunge mkono uteuzi huo.

Ni kijana mwenye kutia matumaini.
 
Sina shaka na uwezo wa Mnyika ila ukimya wake wa siku za karibuni haumfanyi kuvuta watu wengi. Nijuavyo mimi ili upate wafuasi lazima uwe active na sio ukimya. Kwangu mimi John Heche au Marcos Albanie walifaa sana kuliko Mnyika wa sasa. Iwapo Mnyika atarudi katika viwango vyake atakuwa katibu mkuu bora sana, lakini kwa ukimya wake wa sasa naona ni kama Mashinji karudi ofisini tena. Ngoja tuone.
 
..Dr.Mashinji alikuwa miongoni mwa wataalamu waliokuwa wakiishauri cdm wakati wakiandaa ilani yao ya uchaguzi.

..siyo kati ya waliojiunga na cdm kwa kusombwa na mafuriko ya Lowassa.

..Dr.Mashinji amefanya kazi kubwa ktk mazingira magumu. Nadhani amesaidia kuweka msingi kwa CDM kujiendesha kama taasisi.

..lingine ni kwamba amejitahidi ku-empower wanachama wengi zaidi, na hakujifanya kuwa mkubwa zaidi ya chama.
Lakini kuna watu hawatakuelewa kwenye hii hoja yako, watataka picha, au ueleze ni kivipi Dr.Mashinji amefanya kazi kubwa.

Lakini licha ya sifa nyingi ulizo zieleza, nimeshangaa kwamba sikuona kama kapata cheo au nafasi nyingine chamani. Je, hii nikwamba wameona hakufanya kitu chochote hiyo miaka mitano aliyotumika kama katibu mkuu? au kaomba kupumzika afanye mambo mengine ki maisha hasa kwenye taaluma yake? au Chama kimemtosa hivyo?
 
Mwanzoni nilihisi Bwana H.e.c.he atachukua hiyo nafasi ila baada ya kubwagwa na yule mh shosti kwenye uchaguzi wa kanda ikabaki story
 
Sina shaka na uwezo wa Mnyika ila ukimya wake wa siku za karibuni haumfanyi kuvuta watu wengi. Nijuavyo mimi ili upate wafuasi lazima uwe active na sio ukimya. Kwangu mimi John Heche au Marcos Albanie walifaa sana kuliko Mnyika wa sasa. Iwapo Mnyika atarudi katika viwango vyake atakuwa katibu mkuu bora sana, lakini kwa ukimya wake wa sasa naona ni kama Mashinji karudi ofisini tena. Ngoja tuone.
Kila jambo na wakati wake.
 
Sina shaka na uwezo wa Mnyika ila ukimya wake wa siku za karibuni haumfanyi kuvuta watu wengi. Nijuavyo mimi ili upate wafuasi lazima uwe active na sio ukimya. Kwangu mimi John Heche au Marcos Albanie walifaa sana kuliko Mnyika wa sasa. Iwapo Mnyika atarudi katika viwango vyake atakuwa katibu mkuu bora sana, lakini kwa ukimya wake wa sasa naona ni kama Mashinji karudi ofisini tena. Ngoja tuone.
Mnyika atarudi kwenye ubora wake.Kilichomnyima raha Mnyika ni uwepo wa Akina Lowassa na genge lake.Mnyika alikuwa ni mwanafunzi mwaminifu wa Dr Slaa.Ujio wa Akina Lowassa lilikuwa ni pigo kubwa kwake.Naamini kwa Sasa hivi atarudi kwenye viwango vyake baada ya mamluki wote kuwekwa pembeni.Chadema isirudie Tena ujinga wa 2015 mwaka 2020

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Lakini kuna watu hawatakuelewa kwenye hii hoja yako, watataka picha, au ueleze ni kivipi Dr.Mashinji amefanya kazi kubwa.

Lakini licha ya sifa nyingi ulizo zieleza, nimeshangaa kwamba sikuona kama kapata cheo au nafasi nyingine chamani. Je, hii nikwamba wameona hakufanya kitu chochote hiyo miaka mitano aliyotumika kama katibu mkuu? au kaomba kupumzika afanye mambo mengine ki maisha hasa kwenye taaluma yake? au Chama kimemtosa hivyo?

..Katibu Mkuu ni nafasi ya kuteuliwa na Mwenyekiti.

..sasa inawezekana Mwenyekiti anataka chama kichukue muelekeo ambao utahitaji Katibu Mkuu mwenye sifa tofauti na Dr.Mashinji.

..nadhani, baada ya Dr.Slaa kuondoka, CDM ilihitaji Katibu Mkuu ambaye hangekuwa mkubwa kuliko chama, na mwenye kuweza ku-decentralize chama ktk kanda zake.
 
Msanii,
Binafsi namuona mnyika kama kijana ambaye anaenda rudisha Chama katika uimara zaidi kwa kushirikiana na Mwenyekiti wake na viongozi wengine Mashinji ni mpole ila yule jamaa si na nafikilia anaweza akawa amepewa mahalum kuelekea 2020. Sijawai kua na chama ila mungu akinisaidia bahada ya uchaguzi 2020 nitajiunga na chama chochote ambacho nitapenda ila nimeami kuanzia juzi kwamba kweli tunachama dola ccm na nakubali kina mizizi ila pia chadema si chama cha mzezo mchezo kabisa ilipofika chadema haitaji propaganda za kwenye mitandao kuikabili bali kuikabili inaitaji akili kubwa,nguvu kidogo,na umakin wa hali juu.inaitaji kuijibu kwa hoja zaidi .Binafsi kwa jicho lingine naiyona tz kwa sasa ina vyama viwili vilivyo imarika yahani ccm na chadema
 
Back
Top Bottom