Mnyika Akalia Kuti Kavu

Bunge letu kwa sasa limekuwa la hovyo sana. Na hii inachangiwa kwa kiasi kikubwa na upendeleo wa wazi unaofanywa na hao wanaokalia kiti cha spika cha kuwakandamiza wapinzani kiasi kwamba kimewafanya wapinzani kuwa na hasira wawapo bungeni. Nilimwona Lisu alivyokasirika pale aliponyimwa nafasi alipoomba mwongozo wa mwenyekiti/spika wakati Sugu alipotakiwa kuwataja Janjaweed. Nafikiri kuna umuhimu wa katiba mpya kutaka Spika kuwa mtu asiyekuwa na chama ili kutoa usawa kwa wabunge wa vyama vyote.
 

hakika umetumwa, kwa jinsi ulivyo anza, kama huna cha kutuambia ni ten times better ukakaa kimya,magamba mna hali ngumu, pole sana
 
Najiuliza!
Je, yawezekana vipi Mwigulu kijana wa juzi tu, aliyeingia kwenye active politics mwishoni mwa 2000 aweze kupewa nafasi nzito ya Mweka Hazina wa CCM Taifa wakati hana miaka mitano kwenye active politics?
Just curious....
 

Ebu tufahamishe Nchemba alikuwa na cheo gani hapo BoT wakati wa sakata la EPA?
 

Hatukushangai bila shaka wewe ni mfuasi wa chadema na kawaida ya vijana wa chadema na viongozi wao ni dharau,matusi,kejeli na ni waropokaji wasiokuwa na data sasa wataona kitakachomkuta Mnyika,namshauri Mh Nchemba usimuache huyu mtu akishindwa kuthibitisha achukuliwe atua kali ili kulinda heshima ya bunge na utulivu wa nchi yetu ujue hawa jamaa wamezidi kuropoka!
 
Last edited by a moderator:
Wewe na Michembe mwenzako nina wasi wasi na shule zenu! Ebu twambie Ur edc.lvl kwanza! Coz sidhan kama unaweza kulopoka ujinga wako ndan ya Jm,kama shle inakutosha! Tambua Mnyika ana shule ya kutosha,yuko makini,na anajiamin kwa kila anachokiongea! Atuitaji kujua michembe aliingia Bot lini,,mwambie asubili moto wake 6days to come!! Ulitumwa nini??
 

Panadol nadhani unawasha washa mtu kuwa mfuasi kijana wa chadema ni kifungu kipi cha katiba nimekivunja tunasema Mwigulu nNchemba ni nut hafafnani na kisomo chake anashusha hadhi ya chama chako CCM kama wengine walivyokishusha kama akina Jakaya
 
hakika umetumwa, kwa jinsi ulivyo anza, kama huna cha kutuambia ni ten times better ukakaa kimya,magamba mna hali ngumu, pole sana

Nimetumwa na Slaa, daktari wetu.
 

Utajuaje huyu hana chama manake watu wanajificha kwenye vivuli fulani mwisho wa siku tunakuja gundua kuwa na mpenzi wa chama fulani na hii imedhihirishwa na wabunge wengi wa chadema mfano Tundu Lissu,Mama Kaihura hawa walijificha kwenye kivuli cha uanaharakati wakiikemea serikali kwa mambo mengi kumbe ni wafuasi wa chadema na ata huyu Dr Ulimboka nae inajulikana wazi ni mfuasi wa chadema kazi yao ni kuishambulia serikali ionekane haifahi kwa watu lengo lao ni kuhghohoficha upendo wa watanzania kwa serikali yao na chama cha CCM kwa ujumla na kuimarisha upinzani hasa chadema ewe mtanzania mzalendo kataa chadema ili kulinda Amani,Umoja na Mshikamano wetu hawa chadema wanafanya hayo yote ikiwamo na uchochezi wa migomo hapa nchini kwa sababu ya uroho na urafi wa madaraka!
 
Kwani Rais si dhaifu? Acha hizo. Mnyika alisema ukweli. Rais wako nchi imemshinda kwa nini tusiseme ukweli?
 
Kuna mmoja alirudisha bilioni 50, sio yeye kweli, hii ilikuwa baada ya 2006. Take care eeee. Halafu serikali inaruhusu wezi kuridisha pesa za uizi. Au walikopa?
 
ohooooo!! huyu Mnyika mbona hivi tena? anakurupuka bila data! Hivi adhabu ya mbunge anayeshindwa kuthibisha huwa ni ipi? maana ni dhahiri shairi kwamba hapa Mnyika atashindwa kuthibitisha.

Itakuwa tu sawa na swala la uthibitisho wa Lema kuhusu waziri mkuu kulidanganya bunge
 
Sawa kama mchemba aliingia BOT 2006 je na kina jpatel,waliingia Bot mwaka gani vile?
 
ohooooo!! huyu Mnyika mbona hivi tena? anakurupuka bila data! Hivi adhabu ya mbunge anayeshindwa kuthibisha huwa ni ipi? maana ni dhahiri shairi kwamba hapa Mnyika atashindwa kuthibitisha.

Mi sioni umuhimu wowote wa kuthibitisha kauli kwani uzoefu umeonyesha hata pale shutuma zinapothibitishwa haziwekwi hadharani na hakuna hatua zinazochukuliwa. Ni mbinu za Spika na wanaoitwa wenyeviti wa vikao kuulinda na kuutetea udhaifu wa viongozi na serikali yao dhaifu.
 
Ebu tufahamishe Nchemba alikuwa na cheo gani hapo BoT wakati wa sakata la EPA?

Kwani we Ritzi, unajua mtoaji na mpokeaji, nani anapona katika rushwa. Kigulu wakati huu hakupokea?
 
[h=6]KWA HILI KIJANA WETU JOHN MNYIKA UMEPOTOKA..................NA UNAPASWA KUMUOMBA RADHI MWIGULU NCHEMBA KUONYESHA UUNGWANA WAKO!!!!!!!! 2004, MWIGULU NCHEMBA a.k.a CHIEF alikuwa THIRD YEAR UDSM-UCHUMI............2005, ALIKUWA ANAFANYA SHAHADA YA UZAMILI (MASTERS) MWAKA WA KWANZA..........OCTOBA 2006 NDIO ALIJIUNGA BOT-BANK OF TANZANIA!!!!!!!!! WAKATI SAKATA LA EPA LILITOKEA 2005!!!!! SEMA UKWELI NA UWONGO UWE MWIKO!!!!!!!! ALUTA CONTINUA!!![/h]
 
Mnyika ni mtu makini sana, hawezi kukurupuka na kusema bila kuwa na vielelezo; ngojeni athibitishe halafu nyie magamba mfiche ushahidi kama mlivyofanya kwa Lema!! Chadema NOMA hawawezekani!!

CCM na washirika wao wamepata kizunguzungu. Kwenye ofisi wala viti hapakaliki. Hii ni kwa sababu hali ya nchi imebadilika. Kwa bahati mbaya wanasoma report za kila mara za usalama wa Taifa(usalama wa viongozi na walala heri). Maana wale jamaa wa usalama wamegawanyika. Wapo wa ukweli na wale feki. Sasa kwa kuwa hizi report zinatoa taarifa halisi na sio zile za kuchakachuwa,zinawaonyesha ukweli halisi wa jinsi wananchi walivyoitosa CCM,hii inawapa wazimu zaidi. Ukitaka kujuwa ona namna akina Mwigulu Nchemba,Nape,Mukama, wanavyopauka hovyo hovyo
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…