MNEC Mlao amkaanga Tundu Lissu, asema ni mpotoshaji

JUMA JUMA

JF-Expert Member
Jan 5, 2013
666
835
MNEC MLAO AMKAANGA TUNDU LISSU, ASEMA NI MPOTOSHAJI.

Alhamisi, Jan 26, 2023.
Misungwi, Mwanza.

Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa Cde Ramadhani Mwinshehe Mlao (MNEC) amewasili Jijini Mwanza akitokea mkoani Shinyanga ambako amekuwa na muendelezo wa ziara Kanda ya ziwa kuelekea katika maadhimisho ya miaka 46 ya CCM na kupokelewa na wanachama wa chama cha mapinduzi katika ofisi za CCM mkoa wa Mwanza.

Katika ziara ameweza kufika wilayani Misungwi ambapo kupitia mkutano mkubwa wa Hadhara MNEC Mlao amempongeza sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa Kazi anayoendelea kufanya kuhakikisha watanzania wanapata maendeleo lakini pia amekemea vikali wanasiasa wanaopotoshaji na wanaosema uongo juu ya kazi kubwa inayofanywa na Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt Samia ambapo amesema;

"Yupo mtu mmoja jana kafanya mkutano wa hadhara pale Dar es Salaam na waziwazi amewadanganya watanzania kuwa bei ya kilo ya Nyama na Maharage ni sawa Tanzania kitu ambacho ni uongo sote tunajua bei ya nyama kilo ni Tsh 8000-9000 huku Maharage bei ni Tsh 3500-4000 hapo tunaona utofauti mkubwa hivyo mtu huyu anapaswa kupuuzwa kwa upotoshaji huo"

Aidha MNEC Mlao ameweza kushiriki katika zoezi la upandaji miti katika Hospital mpya ya wilaya ya Misungwi sambamba na kupandisha Bendera katika Shina namba tano kata ya Misungwi na kuzungumza na mwenyekiti wa shina Ndgu Juma Malangu ambapo amemshukuru sana MNEC Mlao kwa kuthamini na kutambua kazi kubwa ya chama inayofanywa kwenye mashina ya CCM.

Pia MNEC Mlao amesisitiza wanachama wa chama cha mapinduzi kuelekea maadhimisho ya miaka 46 ya CCM kuendelea kukijenga chama katika maeneo yao yote na kuwajuza kuwa uimara wa CCM utatokana na namna ambavyo tutaendelea kufanyakazi za chama kwa kujitolea vyema kuhakikisha idadi ya wanachama inazidi kukuwa sambamba nakufuatilia vyema utekelezaji wa ilani.

#MimiNiNyinyi

Imetolewa na:

JOSHUA KANDUMILA.

KATIBU WA UVCCM MKOA WA MWANZA.


 
Hawa Chadema malaghai sana, yaani yaliambiwa kilo ya nyama na maharage ni 9000, yakashangilia, halafu linaelekea nyumbani, linatoa 3000 kununua kilo ya maharage.

Linatembea linajisifu kama zuzu.

Mtu mwenye akili akikuambia suala la kijinga, wakati anajua una akili, huyo amekudharau
 
MNEC MLAO AMKAANGA TUNDU LISSU, ASEMA NI MPOTOSHAJI.

Alhamisi, Jan 26, 2023.
Misungwi, Mwanza.

Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa Cde Ramadhani Mwinshehe Mlao (MNEC) amewasili Jijini Mwanza akitokea mkoani Shinyanga ambako amekuwa na muendelezo wa ziara Kanda ya ziwa kuelekea katika maadhimisho ya miaka 46 ya CCM na kupokelewa na wanachama wa chama cha mapinduzi katika ofisi za CCM mkoa wa Mwanza.

Katika ziara ameweza kufika wilayani Misungwi ambapo kupitia mkutano mkubwa wa Hadhara MNEC Mlao amempongeza sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa Kazi anayoendelea kufanya kuhakikisha watanzania wanapata maendeleo lakini pia amekemea vikali wanasiasa wanaopotoshaji na wanaosema uongo juu ya kazi kubwa inayofanywa na Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt Samia ambapo amesema;

"Yupo mtu mmoja jana kafanya mkutano wa hadhara pale Dar es Salaam na waziwazi amewadanganya watanzania kuwa bei ya kilo ya Nyama na Maharage ni sawa Tanzania kitu ambacho ni uongo sote tunajua bei ya nyama kilo ni Tsh 8000-9000 huku Maharage bei ni Tsh 3500-4000 hapo tunaona utofauti mkubwa hivyo mtu huyu anapaswa kupuuzwa kwa upotoshaji huo"

Aidha MNEC Mlao ameweza kushiriki katika zoezi la upandaji miti katika Hospital mpya ya wilaya ya Misungwi sambamba na kupandisha Bendera katika Shina namba tano kata ya Misungwi na kuzungumza na mwenyekiti wa shina Ndgu Juma Malangu ambapo amemshukuru sana MNEC Mlao kwa kuthamini na kutambua kazi kubwa ya chama inayofanywa kwenye mashina ya CCM.

Pia MNEC Mlao amesisitiza wanachama wa chama cha mapinduzi kuelekea maadhimisho ya miaka 46 ya CCM kuendelea kukijenga chama katika maeneo yao yote na kuwajuza kuwa uimara wa CCM utatokana na namna ambavyo tutaendelea kufanyakazi za chama kwa kujitolea vyema kuhakikisha idadi ya wanachama inazidi kukuwa sambamba nakufuatilia vyema utekelezaji wa ilani.

#MimiNiNyinyi

Imetolewa na:

JOSHUA KANDUMILA.

KATIBU WA UVCCM MKOA WA MWANZA.

View attachment 2496588
View attachment 2496589
Kwa hiyo kasikiliza hotuba nzima ya TAL akaona hoja ni maharage kufananishwa na nyama hadi akaandaa na hotuba ya maharage na nyama kuwa na utofauti wa bei? Hivi kweli hawa chawa ndivyo waliyokubaliana kukomaa na vitu vya kitoto namna hii?
 
MNEC MLAO AMKAANGA TUNDU LISSU, ASEMA NI MPOTOSHAJI.

Alhamisi, Jan 26, 2023.
Misungwi, Mwanza.

Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa Cde Ramadhani Mwinshehe Mlao (MNEC) amewasili Jijini Mwanza akitokea mkoani Shinyanga ambako amekuwa na muendelezo wa ziara Kanda ya ziwa kuelekea katika maadhimisho ya miaka 46 ya CCM na kupokelewa na wanachama wa chama cha mapinduzi katika ofisi za CCM mkoa wa Mwanza.

Katika ziara ameweza kufika wilayani Misungwi ambapo kupitia mkutano mkubwa wa Hadhara MNEC Mlao amempongeza sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa Kazi anayoendelea kufanya kuhakikisha watanzania wanapata maendeleo lakini pia amekemea vikali wanasiasa wanaopotoshaji na wanaosema uongo juu ya kazi kubwa inayofanywa na Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt Samia ambapo amesema;

"Yupo mtu mmoja jana kafanya mkutano wa hadhara pale Dar es Salaam na waziwazi amewadanganya watanzania kuwa bei ya kilo ya Nyama na Maharage ni sawa Tanzania kitu ambacho ni uongo sote tunajua bei ya nyama kilo ni Tsh 8000-9000 huku Maharage bei ni Tsh 3500-4000 hapo tunaona utofauti mkubwa hivyo mtu huyu anapaswa kupuuzwa kwa upotoshaji huo"

Aidha MNEC Mlao ameweza kushiriki katika zoezi la upandaji miti katika Hospital mpya ya wilaya ya Misungwi sambamba na kupandisha Bendera katika Shina namba tano kata ya Misungwi na kuzungumza na mwenyekiti wa shina Ndgu Juma Malangu ambapo amemshukuru sana MNEC Mlao kwa kuthamini na kutambua kazi kubwa ya chama inayofanywa kwenye mashina ya CCM.

Pia MNEC Mlao amesisitiza wanachama wa chama cha mapinduzi kuelekea maadhimisho ya miaka 46 ya CCM kuendelea kukijenga chama katika maeneo yao yote na kuwajuza kuwa uimara wa CCM utatokana na namna ambavyo tutaendelea kufanyakazi za chama kwa kujitolea vyema kuhakikisha idadi ya wanachama inazidi kukuwa sambamba nakufuatilia vyema utekelezaji wa ilani.

#MimiNiNyinyi

Imetolewa na:

JOSHUA KANDUMILA.

KATIBU WA UVCCM MKOA WA MWANZA.

View attachment 2496588
View attachment 2496589
Kwa hili nitasimama na Lissu!

Suala sio utofauti wa bei,kati ya nyama na Maharage!

Hoja kubwa ni kwa nini bei za bidhaa hizo ambazo kimsingi,hazitokei Ukraine .

Ng'ombe wamejazana Tanzania, halafu kilo moja inakuwaje 9,000/=. ...why!

Maharage yanalimwa Tanzania , lakimi kilo imefikia kilo shilingi 4,000/= kwa nimi?

Samia ndie alikuwa wa kwanza kushawishi,upandaji wa bei holela,kupitia hotuba zake kadhaa,alipokuwa akitetea Tozo!

Msituone watanzania woye ni makabwela tusiojitambua.

Unapofungua mipaka ya mchi,ili kuwafurahisha baadhi ya watu na kutafuta Political Mileage.

Madhara yanapotokea muwe mnajua mlipokosea na kutoa ufafanuzi!

Leo hii mnatembea mkiwadanganya hao wavaa kijani,na kusubiria Posho,lakini wapiga kura suo hao pekee!

Mkipigwa chini baadae msije kushtuka,kwa sasa endeleeni kukamua buyu la asali.
 
Kama data za uchumi zinawavuruga, hamjui bei za bidhaa, ndio mnataka mkabidhiwe nchi........nimekaaa paleeeee.....
Nyie ndio mliovuruga. Tuna ng'ombe wengi, hivyo bei ya nyama ilitakiwa iwe kilo 1 ni tsh.4000. Hamjamsoma Lisu vizuri, hapo mnaingia kwenye ile 18 alioitaka ili abutue mpita vizuri. Sasa hiyo iliyotakiwa kuwa bei ya nyama ndio bei ya maharage mpo apo. Hii bei ya tsh.9000 mpaka 10,000 siyo bei halali, bali ni ulanguzi. Nayo mnataka kusingizia vita ya Ukraine na Urusi? Wakati mifugo tunayo. Pia mtafakari vizuri point anazotoa mwamba! Hakurupuki, ukimsoma kama kachemka Ukamshambulia! ujue unakuja kuchemshwa wewe. Endeleeni kusema anadanganya ili afafanue vizuri hii oja mtanikumbuka.
 
Back
Top Bottom