Mnasema mmesoma elimu yenu imetufikisha wapi?

Mnasema mmesoma elimu yenu imetufikisha wapi?

mwanaharakatihalisi1

Senior Member
Joined
Apr 26, 2013
Posts
107
Reaction score
25
Nikiiangazia kuanzia pembe ya Africa mpaka mwisho kusini mwake tokea uhuru viongozi wengi ni wakristo na asilimia kubwa ya watendaji ni wakristo na wao ndio wanadai wamesoma.
Swali langu ni Elimu yao na usomi wao umetufikisha wapi? Mbona tunazidi kuwa masikini na mafisadi wanaongezeka?
Mataifa ya nje yanazidi kuifanya africa shamba la bibi.. mnashindwa vipi kutumia elimu yenu ambayo mnajisifia kila siku?
Tujadili bila jazba wala kuumiza hisia za watu
 
Naona mmeanza,hivi huu udini ndiyo wimbo kila siku??
 
Heshima natanguliza Salamu mbele,
Elimu ni mwangaza (light/nuru)
Elimu bila utu ni kama nyumba bila wakazi ndani.
Elimu haina mwisho.
Elimu ni manufaa.
hizo kuta nne hujengwa kama nyumba na elimu, Lakini ikiingia Dharau,Bweteka,Faraguwo,kiburi. Basi nyumba husambaratika na ELIMU kuwa bila maendeleo wala mafanikio...Hatimaye elimu huwa kama moshi hewani.
kwa mtazamo wangu tu.
 
hapa tulipo na tunakoelekea.
ki ukweli hoja yako ni nzuri kama ingesimama bila dini kwa kuwazungumzia wasomi kwa ujumla wametufikisha wapi ingekuwa na mashiko zaidi harafu hili la dini lingejadiliwa ndani kwa ndani.
swala la nchi linatuuma wote na linatukela kwelikweli sijui inakuwaje/
hao wasomi wenyewe wamekuwa vilaza kila siku mawazo yao ni kujikita kujibu maswali rahisi (waibe wakagombee ubunge ) na matokeo yake wanatoka maeneo ya maana ya kuijenga nchi.
daktari mbunge -afya bora tunaipata wapi
mwandisi mbunge tatizo la maji na upangaji miji litaishaje
mwalimu pekee ndiye aliyebaki kwenye taaluma yake unategemea nini.

lakini paliko na ukweli lazima tukubali wakristo wengi tumepoteza maadili ya dini yetu na hapa tusiwe wabishi wengi wetu hatufanyi kwa ajili ya wengine tumekuwa warafi wezi wdhurumaji wenye tamaa ya mali na fedha bila kujali uhalali wake.
inauma lakin huu ndio ukweli wenyewe.
mikataba mingi yanchi kudhurumiwa imesimamiwa na viongozi wakristo kwa kujua walichokuwa wanafanya au kutokujua na kubwa zaidi ni ubinafsi wetu tu.
tubadilike hata waliotuletea shule hawakutegemea tungekuwa katika hali hii.
tubadilike tuikomboe nchi yetu inaliwa na mchwa wenye ukubwa wa simba.
 
Nikiiangazia kuanzia pembe ya Africa mpaka mwisho kusini mwake tokea uhuru viongozi wengi ni wakristo na asilimia kubwa ya watendaji ni wakristo na wao ndio wanadai wamesoma.
Swali langu ni Elimu yao na usomi wao umetufikisha wapi? Mbona tunazidi kuwa masikini na mafisadi wanaongezeka?
Mataifa ya nje yanazidi kuifanya africa shamba la bibi.. mnashindwa vipi kutumia elimu yenu ambayo mnajisifia kila siku?
Tujadili bila jazba wala kuumiza hisia za watu

nimeshtuki inshu hapa huu uzi ni wa udini
 
Nafkiri Mods wanatakiwa kuifuta hii mada ili isiendelee kupata wachangiaji! Nasema hivyo kwa sababu inaonyesha mtoa mada anataka kuendeleza mijadala ya udini ambayo kwa kiasi kikubwa inaendelea kuleta mpasuko kwenye jamii ya Watanzania. Pia mada imekosa mashiko kwa sababu zifuatazo

1. Mtoa uzi katumia mawazo yake binafsi katika kutoa mada yenye ujumla kwa nchi za Kiafrika.
2. Si kweli kwamba nchi za kiafrika, ikiwemo Tanzania zina viongozi wengi wa kikristo kuliko waislam. Siamin kama kuna tafiti zilizofanyika kuhusu idadi ya viongozi na dini zao katika nchi zetu.
3. Suala la maendeleo si suala la wakristo au waislam peke yako! Ni suala mtambuka, linahusisha watu wa kila aina, jinsia zote! Hata kama wakristo wako kwenye nafasi ya kutunga sera na kusimamia, halaf waislam wako kwenye utekelezaji, wote wanawajibika kwa ajili ya kuleta maendeleo.
4. Dhana ya kwamba wakristo wamesoma kuliko waislam haina mashiko. Ni maneno ya mitaani tu!

Nimemaliza!

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Nikiiangazia kuanzia pembe ya Africa mpaka mwisho kusini mwake tokea uhuru viongozi wengi ni wakristo na asilimia kubwa ya watendaji ni wakristo na wao ndio wanadai wamesoma.
Swali langu ni Elimu yao na usomi wao umetufikisha wapi? Mbona tunazidi kuwa masikini na mafisadi wanaongezeka?
Mataifa ya nje yanazidi kuifanya africa shamba la bibi.. mnashindwa vipi kutumia elimu yenu ambayo mnajisifia kila siku?
Tujadili bila jazba wala kuumiza hisia za watu

Mkuu, ni kweli kikwazo kikubwa cha maendeleo kimekuwa ni magaidi, maharamia, mafisadi, wauza bangi, wauza unga, watumia madawa, watoro wa shule, vibaka nk, ambao tumejaribu sana kuwarekebisha na hata kuwaweka kizuizini.

Ila nakuomba pia ufanye utafiti kwamba wengi wa hawa wahalifu wanaozuia maendeleo yetu ni Wakristo au Waislamu ili tuamue kwamba sote tuwe Wakristo au Waislamu maana inaonekana kuna upande ambao angalau kuna maadili. Hii itaongeza kasi ya maendeleo yetu.

Deal?
 
Nikiiangazia kuanzia pembe ya Africa mpaka mwisho kusini mwake tokea uhuru viongozi wengi ni wakristo na asilimia kubwa ya watendaji ni wakristo na wao ndio wanadai wamesoma.
Swali langu ni Elimu yao na usomi wao umetufikisha wapi? Mbona tunazidi kuwa masikini na mafisadi wanaongezeka?
Mataifa ya nje yanazidi kuifanya africa shamba la bibi.. mnashindwa vipi kutumia elimu yenu ambayo mnajisifia kila siku?
Tujadili bila jazba wala kuumiza hisia za watu


Na wewe tuambie, somalia, syria, sudan, jordan, afghanistan, tunisia, morocco, misri, zimefikishwa hapo zilipo na akina nan???

Kwa kukusaidia tu, Elimu inaanza kwanza na kukusaidia mwenyewe. Wewe kalia majungu tu na sumu za ponda wenu
 
Elimu na Ufisadi ni vitu viwili tofauti,unaweza kupata elimu na ukawa fisadi,kinachotakiwa ni nia ya viongozi
 
somalia, syria afghanistan, misri libya .........uislam umezifikisha wapi? utasema nchi za magharibi inamaana nchi za magharibi zinauwezo zaidi ya Mungu wenu.
 
hapa tulipo na tunakoelekea.
ki ukweli hoja yako ni nzuri kama ingesimama bila dini kwa kuwazungumzia wasomi kwa ujumla wametufikisha wapi ingekuwa na mashiko zaidi harafu hili la dini lingejadiliwa ndani kwa ndani.
swala la nchi linatuuma wote na linatukela kwelikweli sijui inakuwaje/
hao wasomi wenyewe wamekuwa vilaza kila siku mawazo yao ni kujikita kujibu maswali rahisi (waibe wakagombee ubunge ) na matokeo yake wanatoka maeneo ya maana ya kuijenga nchi.
daktari mbunge -afya bora tunaipata wapi
mwandisi mbunge tatizo la maji na upangaji miji litaishaje
mwalimu pekee ndiye aliyebaki kwenye taaluma yake unategemea nini.

lakini paliko na ukweli lazima tukubali wakristo wengi tumepoteza maadili ya dini yetu na hapa tusiwe wabishi wengi wetu hatufanyi kwa ajili ya wengine tumekuwa warafi wezi wdhurumaji wenye tamaa ya mali na fedha bila kujali uhalali wake.
inauma lakin huu ndio ukweli wenyewe.
mikataba mingi yanchi kudhurumiwa imesimamiwa na viongozi wakristo kwa kujua walichokuwa wanafanya au kutokujua na kubwa zaidi ni ubinafsi wetu tu.
tubadilike hata waliotuletea shule hawakutegemea tungekuwa katika hali hii.
tubadilike tuikomboe nchi yetu inaliwa na mchwa wenye ukubwa wa simba.

tatizo unaongea bila fact huna na information za kutosha,kwaiyo unataka kuniambia wakristo na mafisadi nchi hii?
 
Kweli wewe ni mwanaharakati wa kidini,tatizo umechanganya mbili kwenye moja,swala la elimu na udini,sawasawa na maendeleo.wapi hiyo? Jipange vizuri.
 
Sijawahi kusoma post ya kijinga kama hii...amakweli JF imeingiliwa!unataka kutueleza kwamba umaskini wa Afrika umeletwa na maraisi wakristo?Nadhani una uelewa mdogo sana wa Historia,siasa na muingiliano wa ki-uchumi wa dunia.
 
Mkuu, ni kweli kikwazo kikubwa cha maendeleo kimekuwa ni magaidi, maharamia, mafisadi, wauza bangi, wauza unga, watumia madawa, watoro wa shule, vibaka nk, ambao tumejaribu sana kuwarekebisha na hata kuwaweka kizuizini.

Ila nakuomba pia ufanye utafiti kwamba wengi wa hawa wahalifu wanaozuia maendeleo yetu ni Wakristo au Waislamu ili tuamue kwamba sote tuwe Wakristo au Waislamu maana inaonekana kuna upande ambao angalau kuna maadili. Hii itaongeza kasi ya maendeleo yetu.

Deal?

Naji quote;

Majina ya wanaohusika na madawa ya kulevya; ili kuelewa nilichosema hapo juu, hii list hapa chini inakuambia nini?
wauza+unga+tanzania2.png
 
Muache tabia ya kutembea na ndizi kwenye kanzu...
 
tatizo unaongea bila fact huna na information za kutosha,kwaiyo unataka kuniambia wakristo na mafisadi nchi hii?
usiogope!
cha kwanza elewa kuwa mimi ni mkristo pia. unataka information gani tena za kuthibitisha mapungufu? lazima tujifunze kusema ukweli ili tujiweke huru sina maana dini nyingine ni wakamilifu hapana lakini na sisi tumekuwa wabinafsi na wezi japo si wamoja kwa moja kwa kuwa tunatumia taaluma zaidi lakini mwisho wa siku nasisi ni wezi tu.
kuwa muungwana kubali! mabadiliko ya maana huanza kwako
 
Back
Top Bottom