Mnara wa Babeli unaanguka

Ne Mbwitu

JF-Expert Member
Joined
Aug 23, 2020
Posts
275
Reaction score
803
1.Ukipita kwenye magroup ya wanavyuo yamepamba moto.
2.Ukipita kwenye magroup ya wafanyakazi kimewaka
3. Ukipita kwenye magroup ya kijani kupo jiii kumepoa kama kiporo cha uji
4. Ukipita magroup ya upinzani, kimesanuka
5. Ukipita magroup ya wafanyabiashara, ni motoo
6. Ukipita magroup ya kitaa, hali ni tete.

Kuna kila dalili mnara wa babeli unaanguka uchaguzi huu.
 
Umetusahau sisi huku vijijini, pia nako kumepamba moto. HATUDANGANYIKA TENA
 
Mvumilie pale matokeo yatakapokuwa yanatangazwa kama yanavyowafikia. Na hakuna mahali popote mnaweza kuyapinga.
 
Ukifuata yanayoongelewa kwenye mitandao, unaweza ukadhani sasa Chadema wamechukua nchi. Hakuna kipindi ambacho watu walidhani CCM ingeanguka kama 2015. Mitandao ilipamba moto lakini matokeo yalivyoanza kutangazwa watu walikimbia siyo Facebook, tweeter, instragram na humu JF. Hata humu, haya mapambio mwisho wake itakua tarehe 29 na 30 Oktoba, 2020.
 
Hii ni ishara ya uvivu hata Rais awe kiumbe gani watu aina ya mleta mada wataendelea kulalamika tu,

Haiwezekani mtu anayejali muda na kuzalisha akawa member wa watsapp group zaidi ya sita, hizo ni chache tu alizotetea mleta mada ukiacha na zile za kiutuuzima ambazo mleta mada naye ni member.
 
Magufuli yupo mpaka 2030
 
Chief umeamua kuzama na Meli yako😂😂
 
Yaani ubabe wa maccm kwa miaka takriban minne umezimwa na TUNDU LISSU kwa week tatu tu
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…