Tujikumbushe Mfalme Nimrod wa mnara wa Babeli

zitto junior

JF-Expert Member
Oct 7, 2013
19,039
28,688
image-20170321-5408-12bnkph.jpg

Habari za jioni wakuu moja kwa moja niende kwenye mada husika za kukumbushana kuhusu watu wa kale waliofanya makubwa leo ningependa tumgusie Nimrod aliyetawala Babylon ya kale huko mashariki ya kati. Kwa ufalme wa sumeria alifahamika kwa jina la Mfalme Enmer-kar alipata kuishi hapa duniani takribani miaka 5000 iliopita.

Kwa tafsiri za biblia na maandiko ya kiislam na kiyahudi (dini kuu 3 za mashariki ya kati) Nimrod alikuwa kitukuu wa Nuhu na mjukuu wa Ham...

Mwanzo 10
8 Kushi akamzaa Nimrodi, akaanza kuwa mtu hodari katika nchi.
9 Alikuwa hodari kuwinda wanyama mbele za BWANA. Kwa hiyo watu hunena, Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda wanyama mbele za BWANA.
10 Mwanzo wa ufalme wake ulikuwa Babeli na Ereku, na Akadi, na Kalne, katika nchi ya Shinari.
11 Akatoka katika nchi ile akaenda mpaka Ashuru, akajenga Ninawi, na Rehoboth-iri, na Kala;
12 na Reseni, kati ya Ninawi na Kala, nao ni mji mkubwa.


UMAARUFU WAKE
1.Inaelezwa kwenye simulizi za kale kuwa mfalme Nimrod/enmer kar baada ya kusimuliwa kuwa mababu zake waliuawa na YHWH/MUNGU/ALLAH kwenye gharika kuu, aliamua kujenga mnara mkubwa ili kumfikia Mungu ili aweze kulipa kisasi kwa "unyama" waliofanyiwa mababu zake. Simulizi zinaeleza aliweza kukusanya watu wengi wa ulimwengu takribani laki 7 na kwakuwa alikuwa mfalme wa himaya kubwa na ya kwanza duniani aliweza kuwakusanya wengi kumfanyia hiyo kazi ya kujenga mnara wa kumfikia Mungu. Mradi huo wa kujenga mnara huo wenye umbo kama pyramid za misri kuanzia ramani kuchorwa,vifaa kuungwa na mnara kukamilika kwa 80% ulichukia takribani miaka 20 hatimaye Mungu alipoona Nia yao ni ovu akawachanganya lugha na baadae kuleta tetemeko lilioangusha mnara huo

NB: Mnara haukuwa wa kumfikia Mungu kimwili yaani mawinguni bali ilikuwa ni kufanya matambiko ya kutengeneza kma GETI la kiroho kuwapeleka mbinguni na simulizi zinasema walipoona GETI hilo limetokea wakaanza kurusha mishale ambayo haikuzaa matunda na baada ya hapo wakatawanywa
Ancient_ziggurat_at_Ali_Air_Base_Iraq_2005.jpg

Mfano wa mnara wa babeli ulivyokuwa

2. Nimrod anaelezwa kwamba ndio mfalme wa Kwanza hapa Duniani na alikuwa ndio wa kwanza kujenga Himaya duniani yaani babeli/sumerian empire... Inaelezwa mifumo mingi ya ujenzi,vita,utawala,jeshi,serikali n.k vilianzia kwake hivyo alikuwa na ushawishi sana kiasi kwamba alitawala koo zote za shem ham na japhet na hata mataifa mengi kutoka pande zote za dunia kufuatana na kitabu cha Jasher walikuwa wanakuja babeli kumuinamia!!!

3. Inaelezwa pia ndio alijenga jiji la kwanza duniani ambao ulikuwa mji mkubwa sana Babylon/babeli... Miji mikubwa na maarufu kwenye historia ya biblia kama shinar,babeli,Ninawi na ashuru na yote ilijengwa na Nimrod huko mashariki ya kati hii pia ilimjengea umaarufu sana nimrod.
images (2).jpg

babylon-006.jpg

4. Kufuatana na kitabu cha jasher zile familia tatu yaani shem japhet na ham ziliingia kwenye vita kubwa sana na Nimrod aliongoza majeshi ya familia ya HAM na kuwatandika ndugu zao hao na toka siku hiyo akawaweka chini ya utawala wake hili pia lilimpa umaarufu sana Nimrod kipindi chake.

5. Ikumbukwe baada ya gharika wanadamu wote yaani familia ya Nuhu na vizazi vyake walikuwa wakimuabudu MUNGU/ALLAH ila alipokuja Nimrod ndio akarudisha ibada za masanamu,matambiko,uchawi hivyo hii dini yake ambayo sanamu lake ndio liliabudiwa nalo ilimpa umaarufu na alipata wafuasi wengi sana maana ndio alileta dini ya kwanza kabisa baada ya gharika tofauti na ile ya asili ya kumuabudu Mungu pekee.

FREEMASONRY
Nimrod pia anahusishwa na kuweka misingi ya Freemasonry na kuna baadhi ya lodge na baadhi vitabu na majarida yao wanamtambua Kama Grand master wao wa kwanza kabisa..... Hata leo hii ukiwa mwanachama wa Freemasons kwenye baadhi ya lodge inatakiwa ule kiapo kwa Nimrod inaitwa NIMROD's OATH..... Pia miongozo,sheria,viapo,taratibu nyingi za freemasons wamezicopy kutoka kwa chama cha kwanza cha giza (secret society)alichokianzisha nimrod cha wajenzi wa mji wa NINAWI, hivyo yote yanayofanywa na freemasons leo na dini zote za kipagani misingi yake iliwekwa na Nimrod

ALIPATAJE USHAWISHI
Simulizi za vitabu kadhaa hasa Book of jasher (kinatambuliwa na baadhi ya waandishi wa biblia) vinaeleza alipata hizo nguvu kutoka Vazi ambalo Mungu alimfanyia Adam kipindi alipojiona yupo uchi baada ya dhambi ya bustani ya edeni.

Mwanzo 3
21 BWANA Mungu akawafanyia Adamu na mkewe mavazi ya ngozi, akawavika

Vazi lile alimrithisha mwanaye - Seth naye likazunguka hadi kufikia kwa nuhu ila Ham aliiba vazi hilo kutoka kwenye safina na likarithishwa kwa cush ambaye alikuwa mwanaye wa kwanza naye akamrithisha Nimrod. Ukisoma the first book of adam and eve,adam alionyesha hofu alipotimuliwa bustanini kuwa Wanyama wakali watamla ila Mungu alimwambia hilo vazi litamlinda na wanyama wote wakali yaani wakimuona tu wanamuinamia na hii ilimfanya Nimrod pia kutetemekewa na wanyama kila alipowaona na ndio maana biblia inasema;

mwanzo 10:9
Alikuwa hodari kuwinda wanyama mbele za BWANA. Kwa hiyo watu hunena, Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda wanyama mbele za BWANA.

Pia inadaiwa uwezo huu wa wanyama kumuogopa ulifanya hata wanadamu wa kawaida wampe heshima ya UUNGU fulani bila kujua siri ya nguvu zake..... Hivyo alipata nguvu za ajabu za kuwatawala watu na kujenga ushawishi sana enzi zake.

ANGUKO LAKE
Kulingana na kitabu cha jasher baada ya maasi kuzidi sababu yake Mungu alikasirishwa sana na siku moja Nimrod akiwa amelala aliota ndoto kuwa utawala wake utaangushwa na mtoto anayekuja kuzaliwa..... Sio miaka mingi akazaliwa abraham na wataalam wa nyota na elimu ya kiroho wa utawala wake walimuambia kuwa huyu abraham ndio atakayekuja kufuta ufalme wake.

Story ni ndefu kidogo ila abraham alitoroshwa mapangoni alafu baba yake akaleta mtoto feki akauawa wakijua ni abraham ila bado kwa miaka 50 nimrod alikuwa anamuota huyo mtoto kuwa anamkata kichwa mwisho wa siku akashtuka lazma abraham hajafa.... Akasakwa na akakamatwa na akatupwa kwenye tanuru la moto ila bado hakuungua ikabidi nimrod amuachie kwa kuhamaki na watu wengi wakamfuata abraham na wakaona wazi nimrod ameshapata bingwa wake!!! Ushawishi tokea hapo ukaanza kuporomoka na miji iliokuwa chini yake kama ELAM ikaanza uasi chini ya mfalme Kedorlaoma aliyemtandika Nimrod na kumuweka chini yake... Mwishoni unabii ulikuja kutimia kwa nimrod kuangushwa na mtu wa kutoka uzao wa abraham yaani mjukuu wake alieitwa Esau.

KIFO CHAKE
Simulizi kadhaa za hadith,tafseer za kiislamu kama tabari II zinaeleza baada ya kumtupa Abraham kwenye tanuru la moto anashangaa kumuona Ametoka akiwa mzima bila kovu na ndio hapo ubishani ukaanza na kejeli kwa Mungu wa Abraham maana Nimrod alidai yeye ana ubavu kuliko huyo Mungu wa Abraham na ndipo zikatokea MBU zikaanza kuwala wale walinzi na Nimrod mwenyewe maana mbu wale walipenya maskioni puani na mdomoni na kumfanya nimrod ajipigize kichwa huku na kule hadi kufariki

Nadharia ya pili kutoka book of jasher inaeleza Nimrod aliuawa na Esau mwana wa Isaka alipokuwa akiwinda ili amuibie VAZI lake la maajabu na inadaiwa baada ya mpambano huu mkali esau akiwa amechoka sana ndipo alipodai chakula kwa yakobo hadi akaishia kuuza haki zake za uzaliwa wa kwanza

Nadharia ya tatu inaeleza baada ya kuona nimrod anaeneza upagani na dini yake ya kishetani... Shem mwana wa Nuhu anapatwa jazba na anaunda umoja na maadui 72 wa Nimrod wanakwenda kuvamia kasri lake na wanamteka kisa wanamkata vipande vipande na wakamzungusha kwenye miji yote aliyotawala kuwaonyesha kuwa Nimrod hakuwa mungu ila mwanadamu tu.

UTATA
Inaelezwa kwenye vitabu mbalimbali vya kishitoria nilivopata kusoma kuwa Nimrod alimuoa Mama yake baada ya baba yake ''kustaafu''uongozi , mke huyo alifahamika kama semiramis ila kiebrania alifahamika kama Shinar kwenye biblia yaani jina ambalo ndio inaelezwa kama Mji alioishi Nimrod.... Huyu mama naye alikuwa sio wa mchezo mchezo wajuaji wa mambo humu wanamfaham sana ila itabidi afunguliwe uzi wake siku nyingine na kwenye biblia anatambulika kma MALKIA WA MBINGU soma Yeremia 7:18

HITIMISHO
Mengi yamesemwa kuhusu mfalme huyu ningependa wajuaji wa mambo pia mtuongezee mbili tatu mnazofahamu kuhusu nguli huyu ili tuzidi kujifunza kuhusu nature ya wanadamu tulipotoka na tunapokwenda..... naomba kuwasilisha

Cc wanajukwa wotee
tower_of_babylon_by_shadrak.jpg
 
NB: Narudia tena nyuzi hii sio ya kidini ni ya kihistoria ila kuna reference chache tu nmetoa kwenye biblia na hadeeth za kiislam hivyo sitegemei kashfa za kidini humu na ningeomba tujadiliane kwa hoja tusiongozwe na mahaba ya kiimani ntashkuru kwa ushirikiano wenu

Karibuni wanajukwaa kwa maoni/michango na data zaidi kuhusu nguli huyu wa kale CC:hearly impongo Mchawi Mkuu Malcom Lumumba Elungata Da'Vinci Mshana Jr Palantir Eiyer Kudo900 Vi rendra N J subi Bujibuji Kipanga boy Kiranga Ziroseventytwo Che mittoga Ip man 3 mitale na midimu Mzee wa Torano Blaki Womani Grahnman za chembe jimmykb197 911sep11
 
Pole mkuu kwa changamoto ya moderators


Huyu bwana ni gumzo jingine katika historia ya dunia, humu jukwaani amezungumziwa sana hasa mr Eiyer.

Kwa ufupi maelezo yanatofutiana sana lakini ninachojua ni mmojawapo wa mwanzilishi wa imani zenye ukinzano na Mungu na mpaka leo hii watu wamwabudu kwa namna moja ama nyingine labda kwa kujua au laa!

Baada ya gharika watu walikua wakimwabudu Mungu lakini yeye alikuja na iman ya kuabudu nyota au sayari na kwa vile alikua na ushawishi watu walimuogopa na kumfuata.

Wazo la imani hio nadhani ni wale malaika waasi waliofungwa enzi hizo wakati wa gharika ili kuendeleza upinzani dhidi ya Mungu.

Imani hii haikumpendeza Ham baba yake hivyo aliamua kuua na kutawanya viungo vya mwili wake kamo onyo kwa yoyote ataedhubutu kufanya hizo ibada alizo anzisha nimrod.

Mke wake nimrod ambae pia inasemekana ni mama yake mzazi aliviokota vile viungo kwaajilili ya kuvizika lakini kiungo cha uzazi hakikuonekana. Na akasema mme wake amepaa, na wale watu wa babeli hawakucha ile imani baada ya kifo cha nimrod ilisemekana amepaa kwenye jua tokea hapo watu wakaanza kuabudu jua na ndipo imani za kuabudu jua zikaanza na alama ya imani hio ni kiungo cha uzazi cha mwanaume (uume) kama alama takatifu.

Imani hizo nadhani zimeendelea hadi leo hii ndio maana nikasema watu wanamuabufu ama kwa kutokujua au kujua!!
Ukiaangalia baadhi ya majengo ya iman hizi zetu mbili kuna style fulani ya ujenzi hata majengo ya uma au minara unakutwa imewekewa wanaita obelesk nadhani, ishara ya kuwa wamo mule mule kwa nimrodi

Mambo ni mengi sana na yote haya hayana ushahidi wa moja kwa moja ni mlolongo ule ule wa siri za dunia ambazo hazijafunuliwa kwa baadhi ya watu. Lakini kwa vile kizazi hiki jua limepambazuka kwetu hatutaacha kujua kila kinachotakiwa kujulikana.
 
Pole mkuu kwa changamoto ya moderators


Huyu bwana ni gumzo jingine katika historia ya dunia, humu jukwaani amezungumziwa sana hasa mr Eiyer.

Kwa ufupi maelezo yanatofutiana sana lakini ninachojua ni mmojawapo wa mwanzilishi wa imani zenye ukinzano na Mungu na mpaka leo hii watu wamwabudu kwa namna moja ama nyingine labda kwa kujua au laa!

Baada ya gharika watu walikua wakimwabudu Mungu lakini yeye alikuja na iman ya kuabudu nyota au sayari na kwa vile alikua na ushawishi watu walimuogopa na kumfuata.

Wazo la imani hio nadhani ni wale malaika waasi waliofungwa enzi hizo wakati wa gharika ili kuendeleza upinzani dhidi ya Mungu.

Imani hii haikumpendeza Ham baba yake hivyo aliamua kuua na kutawanya viungo vya mwili wake kamo onyo kwa yoyote ataedhubutu kufanya hizo ibada alizo anzisha nimrod.

Mke wake nimrod ambae pia inasemekana ni mama yake mzazi aliviokota vile viungo kwaajilili ya kuvizika lakini kiungo cha uzazi hakikuonekana. Na akasema mme wake amepaa, na wale watu wa babeli hawakucha ile imani baada ya kifo cha nimrod ilisemekana amepaa kwenye jua tokea hapo watu wakaanza kuabudu jua na ndipo imani za kuabudu jua zikaanza na alama ya imani hio ni kiungo cha uzazi cha mwanaume (uume) kama alama takatifu.

Imani hizo nadhani zimeendelea hadi leo hii ndio maana nikasema watu wanamuabufu ama kwa kutokujua au kujua!!
Ukiaangalia baadhi ya majengo ya iman hizi zetu mbili kuna style fulani ya ujenzi hata majengo ya uma au minara unakutwa imewekewa wanaita obelesk nadhani, ishara ya kuwa wamo mule mule kwa nimrodi

Mambo ni mengi sana na yote haya hayana ushahidi wa moja kwa moja ni mlolongo ule ule wa siri za dunia ambazo hazijafunuliwa kwa baadhi ya watu. Lakini kwa vile kizazi hiki jua limepambazuka kwetu hatutaacha kujua kila kinachotakiwa kujulikana.
Aseee nashkuru kwa mchango wako sikufahamu kabisa katika viungo vyake vyote vilivopatikana ni cha sehem za siri pekee hakikupatikana!! Duh hatari hii ..... Na hiki naona ndio kilisababisha hata semiramis akawashika watu vichwa pale alipopata mimba na kudai imetokana na Jua ilihali nimrod alishamuacha na ujauzito wa wiki kadhaa! na ndipo inadaiwa akazaliwa mungu TAMMUZ ambaye watu wakamuabudu wakifkiri nimrod kazaliwa upya na ndio maana akaitwa NIMROD pia kama cheo..... anaabudiwa na dini nyingi za kipagani hata nature ya siku ya 25 december ilikuwa sherehe yake ya kuzaliwa huyu TAMMUZ!!!

Na ile picha semiramis amemkumbatia mwanae TAMMUZ inatumika na dini nyingi kuu kwenye nyumba zao za ibada!!!
 
Umetoa caution kwamba Uzi huu sio wa kidini, na hapa umeanza kejeli dhidi ya imani zetu. Akina JamiiForums na Moderator please upelekeni huu Uzi jukwaa la dini ili mtoa mada akapate wajuzi wenzake wa kumjibu hizi kashfa
Mkuu nilitoa comment sababu niliyemquote alizungumzia dini ya kuabudu jua ila sijataja kanisa lolote kwa jina na wala sijataja sikukuu ya tarehe 25 ni ipi coz nafahamu uzi huu sio wa kidini ila post niliyojibu imegusia dini kama nmekuudhi samahani sana ntaifuta hiyo comment
 
Mkuu nilitoa comment sababu niliyemquote alizungumzia dini ya kuabudu jua ila sijataja kanisa lolote kwa jina na wala sijataja sikukuu ya tarehe 25 ni ipi coz nafahamu uzi huu sio wa kidini ila post niliyojibu imegusia dini kama nmekuudhi samahani sana ntaifuta hiyo comment
Cheers!
Ume edit, now comment ipo well balanced.
ahsante kwa uchambuzi mzuri
 
Mkuu nilitoa comment sababu niliyemquote alizungumzia dini ya kuabudu jua ila sijataja kanisa lolote kwa jina na wala sijataja sikukuu ya tarehe 25 ni ipi coz nafahamu uzi huu sio wa kidini ila post niliyojibu imegusia dini kama nmekuudhi samahani sana ntaifuta hiyo comment
Mkuu hivi inakuwaje ikitajwa tu dini watu huwehuka na kushindwa kuendana na maada iliyopo?. Dini sio imani kwamba ukiwa dini fulani na kuitetea mitandaoni ndo utapewa thawabu la hasha, ila imani ni matendo
 
Mkuu hivi inakuwaje ikitajwa tu dini watu huwehuka na kushindwa kuendana na maada iliyopo?. Dini sio imani kwamba ukiwa dini fulani na kuitetea mitandaoni ndo utapewa thawabu la hasha, ila imani ni matendo
Mwanzisha thread ameelewa na kuweka comment yake vema. Kwa kujua sensitivity ya eneo hili, ndio maana jukwaa la dini lipo lakini limefichwa huko, ukiamua kuingia ni kwa ridhaa yako mwenyewe. Mabishano ya kidini hayajengi wala hayajawahi kujenga.
Ahsante
 
Aseee nashkuru kwa mchango wako sikufahamu kabisa katika viungo vyake vyote vilivopatikana ni cha sehem za siri pekee hakikupatikana!! Duh hatari hii ..... Na hiki naona ndio kilisababisha hata semiramis akawashika watu vichwa pale alipopata mimba na kudai imetokana na Jua ilihali nimrod alishamuacha na ujauzito wa wiki kadhaa! na ndipo inadaiwa akazaliwa mungu TAMMUZ ambaye watu wakamuabudu wakifkiri nimrod kazaliwa upya na ndio maana akaitwa NIMROD pia kama cheo..... anaabudiwa na dini nyingi za kipagani hata nature ya siku ya 25 december ilikuwa sherehe yake ya kuzaliwa huyu TAMMUZ!!!

Na ile picha semiramis amemkumbatia mwanae TAMMUZ inatumika na dini nyingi kuu kwenye nyumba zao za ibada!!!
kumbe unaifahamu vyema nature. ya hiyo tarehe 25 December....safi sana."" dunia hii Ina mambo ya ajabu mnooo ..kama hujifunzi huwezi kuutambua ulimwengu " na makusudi ya binaadamu wake ....dunia ina visa hii looooo
 
Mkuu nilitoa comment sababu niliyemquote alizungumzia dini ya kuabudu jua ila sijataja kanisa lolote kwa jina na wala sijataja sikukuu ya tarehe 25 ni ipi coz nafahamu uzi huu sio wa kidini ila post niliyojibu imegusia dini kama nmekuudhi samahani sana ntaifuta hiyo comment
hahaa ina maana ka mind ..daahh imani hizi ""!! haya ngoja tuendlee kujifunza
 
Niliona movie ya UNCLE SADDAM ya kumuhusu saddam hussein,kuna mahali kama walieleza kua saddam hussein aliujenga upya mnara huo (sio wote,sehemu tu ya maghofu) ila sikumbuki vizuri
Yes mkuu miaka ya 80 saddam alijaribu kuijenga upya babylon ya kale hata mnara alikuwa ana mpango huo ila wenye dunia yao walimuua kabla hajakamilisha ili wao waujenge upya mwaka 2012 !!! Hizi mambo ndio zilimfanya hadi papa ajiuzuru miezi michache baadae.... Sorry sio uzi wa dini naishia hapa
 
Yes mkuu miaka ya 80 saddam alijaribu kuijenga upya babylon ya kale hata mnara alikuwa ana mpango huo ila wenye dunia yao walimuua kabla hajakamilisha ili wao waujenge upya mwaka 2012 !!! Hizi mambo ndio zilimfanya hadi papa ajiuzuru miezi michache baadae.... Sorry sio uzi wa dini naishia hapa
tililika mkuu, unajua kuna baadhi ya coment ili uzijibu na mtu akuelewe ni lazima ugusie maswala ya dini/imani hili halipingiki, anaeboreka ni vema akakaa Mbali na uzi huu.
 
Kwa kifupi, alianzisha taasisi ya kumpinga Mungu, Mungu aliifutilia mbali. Kumbuka neno Babeli humaanisha machafuko, Mungu amekuwa akiiangamiza babeli, kisha wababeli kuisimika tena. Mara ya kwanza Babeli kuharibiwa ni kipindi cha mnara. Mara ya pili ni Babeli ya kina Nebkadreza, ambayo ilisambaratishwa kupitia Koreshi mwajemi. Na mpaka sasa tunaishi na kufuata mambo ya Babeli ya kisasa, ila nayo si mbali itaharibiwa, na ndiyo utakuwa mwisho rasmi wa Babeli. Kwa maelezo mapana ya Babeli ya kisasa, soma UFUNUO sura ya 17 na 18.
 
Back
Top Bottom