Mnaotaka na kulilia jeshi lichukue nchi hamjitambui

Mnaotaka na kulilia jeshi lichukue nchi hamjitambui

Keynez

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2007
Posts
3,635
Reaction score
6,535
Nilikaa mbali na mijadala ya kisiasa kwa muda ila nimelazimika kulisema hili. Huu uzi nilikusudia kuuleta kitambo sana ila nikawa napotezea au kuahirisha kuuleta.

Kuna watu kutokana na sababu wanazojua wao wamekuwa wanatoa kauli za kutaka JWTZ lichukue uongozi wa nchi. Kuna wakati hadi nahisi kuna wanaharakati ambao ni mapandikizi waliowekwa ili kuwalinda CCM na viongozi wake pale hali itakapokuwa ngumu sana kwao.

Nasema hili la jeshi linaweza kuwa pona ya CCM. Kama mnataka mrudi nyuma hatua 50 kwenye demokrasia basi mkubaliane na hilo.

Sehemu kama Sudan, harakati za demokrasia zilizikwa rasmi baada ya jeshi kuingilia kati. Misri ni hivyo hivyo. Maeneo mengi tu demokrasia ilirudi nyuma sana baada ya mapinduzi ya kijeshi.

Mnapopambana kupata uchaguzi huru na wa haki, msitamani kamwe njia za mkato kama hizo za kutaka jeshi lichukue nchi.
 
Nilikaa mbali na mijadala ya kisiasa kwa muda ila nimelazimika kulisema hili. Huu uzi nilikusudia kuuleta kitambo sana ila nikawa napotezea au kuahirisha kuuleta.

Kuna watu kutokana na sababu wanazojua wao wamekuwa wanatoa kauli za kutaka JWTZ lichukue uongozi wa nchi. Kuna wakati hadi nahisi kuna wanaharakati ambao ni mapandikizi waliowekwa ili kuwalinda CCM na viongozi wake pale hali itakapokuwa ngumu sana kwao.

Nasema hili la jeshi linaweza kuwa pona ya CCM. Kama mnataka mrudi nyuma hatua 50 kwenye demokrasia basi mkubaliane na hilo.

Sehemu kama Sudan, harakati za demokrasia zilizikwa rasmi baada ya jeshi kuingilia kati. Misri ni hivyo hivyo. Maeneo mengi tu demokrasia ilirudi nyuma sana baada ya mapinduzi ya kijeshi.

Mnapopambana kupata uchaguzi huru na wa haki, msitamani kamwe njia za mkato kama hizo za kutaka jeshi lichukue nchi.
Jerry Rawlings na Obasanjo ni mifano mizuri.
 
Hujitambui wewe

Watanzania tuko tayari na tunataka sana Jeshi lichukue nchi na tuanze upya.

CCM mmeharibu kila kitu sasahivi nchini.

Mmeua mifumo yote Si Bunge, Si Mahakama, Si Polisi si Usalama si TAKUKURU

Wanasiasa ndo wamekuwa miungu watu na Ufisadi ndo umetamalaki.

Wananchi wanauliwa na kutekwa wengine kuwekwa Magerezani na kufungwa bila hatia kwa sababu ya kusimamia ukweli.

Wananchi kwa sauti moja tunataka Jeshi lichukue nchi na tuanze upya.

Lisimamie mchakato wa Katiba Mpya ili Wananchi ndo tuwe na sauti ya mwisho juu ya nchi yetu.
 
Mjinga wee ,ndezi, na mpuuzi mkubwa.

Angela Kiziga mkubwa wee.


Unadhan hata Wananchi tukiandamana na kuchukua Nchi, nani atawasaidia Wananchi kuleta Utulivu.
Majeshi yote yatimize majukumu yao ya kulinda raia na mali zao pamoja na mipaka ya nchi bila kuingilia mivutano ya kisiasa.

Kuingilia mivutano ya kisiasa ni pamoja na hayo baadhi ya watu msiojitambua mnaotaka jeshi lichukue nchi.

Yule anayekiuka katiba na sheria za nchi ashughulikiwe na majeshi hayo kulingana na sheria zinavyosema bila kujalisha cheo wala chama chake.
 
Hujitambui wewe

Watanzania tuko tayari na tunataka sana Jeshi lichukue nchi na tuanze upya.

CCM mmeharibu kila kitu sasahivi nchini.

Mmeua mifumo yote Si Bunge, Si Mahakama, Si Polisi si Usalama si TAKUKURU

Wanasiasa ndo wamekuwa miungu watu na Ufisadi ndo umetamalaki.

Wananchi wanauliwa na kutekwa wengine kuwekwa Magerezani na kufungwa bila hatia kwa sababu ya kusimamia ukweli.

Wananchi kwa sauti moja tunataka Jeshi lichukue nchi na tuanze upya.

Lisimamie mchakato wa Katiba Mpya ili Wananchi ndo tuwe na sauti ya mwisho juu ya nchi yetu.
Narudia tena, kutaka jeshi lichukue nchi ni kulinda CCM na mafisadi walioiibia nchi. Dawa ni kupata mabadiliko ya kidemokrasia ambayo yanaweza kupatikana bila vurumai hizo za jeshi.

Mabadiliko ya kidemokrasia yakipatikana kupitia mashinikizo ya kisiasa, ni rahisi kupata hayo unayotamani tena kwa haraka zaidi.

Shida yenu mnatafuta njia za mkato kwa mambo magumu na mnataka wengine ndiyo wawafanyie kazi ngumu ambayo imo ndani ya uwezo wenu.
 
Sehemu kama Sudan, harakati za demokrasia zilizikwa rasmi baada ya jeshi kuingilia kati. Misri ni hivyo hivyo. Maeneo mengi tu demokrasia ilirudi nyuma sana baada ya mapinduzi ya kijeshi.
Nini kitazika demokrasia endapo jeshi litachukua nchi?

Kwa taarifa yako jeshi litachukua nchi kwa kipindi cha mpito tu, na katika kipindi hicho wataruhusu marekebisho ya katiba na kisha uchaguzi utaitishwa.
 
Nilikaa mbali na mijadala ya kisiasa kwa muda ila nimelazimika kulisema hili. Huu uzi nilikusudia kuuleta kitambo sana ila nikawa napotezea au kuahirisha kuuleta.

Kuna watu kutokana na sababu wanazojua wao wamekuwa wanatoa kauli za kutaka JWTZ lichukue uongozi wa nchi. Kuna wakati hadi nahisi kuna wanaharakati ambao ni mapandikizi waliowekwa ili kuwalinda CCM na viongozi wake pale hali itakapokuwa ngumu sana kwao.

Nasema hili la jeshi linaweza kuwa pona ya CCM. Kama mnataka mrudi nyuma hatua 50 kwenye demokrasia basi mkubaliane na hilo.

Sehemu kama Sudan, harakati za demokrasia zilizikwa rasmi baada ya jeshi kuingilia kati. Misri ni hivyo hivyo. Maeneo mengi tu demokrasia ilirudi nyuma sana baada ya mapinduzi ya kijeshi.

Mnapopambana kupata uchaguzi huru na wa haki, msitamani kamwe njia za mkato kama hizo za kutaka jeshi lichukue nchi.
Sisi au wanaotaka Samia aendelee nani hana akili
 
CCM inaweza kuondoka vizuri tu kwa mashinikizo ya kisiasa. Hao wanajeshi wangesisitizwa wabaki makambini watimize viapo vyao kwa ukamilifu, siasa wawaachie wananchi, wanasiasa na vyombo vya kisiasa.
Ikiwa vyama vya kisiasa vinaminywa unashauri nini?
 
Nini kitazika demokrasia endapo jeshi litachukua nchi?

Kwa taarifa yako jeshi litachukua nchi kwa kipindi cha mpito tu, na katika kipindi hicho wataruhusu marekebisho ya katiba na kisha uchaguzi utaitishwa.
Hiko unachotaka jeshi ikifanye, raia na taasisi za kiraia wanaweza kukifanya kwa ufanisi zaidi. Ukiruhusu jeshi liingie leo, nini kitalizuia kesho kuingia tena?

Mashinikizo ya kisiasa ndiyo njia pekee sahihi ya kuiondoa CCM. Ilibidi kuishinikiza hadi kuipeleka katika meza ya mazungumzo. Njia za mashinikizo zipo na mnazijua ila hamtaki kuzitumia kwa sababu ya woga, uvivu na kutegeana.
 
CCM inaweza kuondoka vizuri tu kwa mashinikizo ya kisiasa. Hao wanajeshi wangesisitizwa wabaki makambini watimize viapo vyao kwa ukamilifu, siasa wawaachie wananchi, wanasiasa na vyombo vya kisiasa.
Hata kama wanatishia tu ni hivi msg sent delivered in full package. Watawala wajue chochote kinawezekana.

New Tanganyika ipo karibu kuzaliwa.
Ukiona mpaka ayo kapost kuna watu watalala na viatu,

Tuheshimiane nchi siyo ya familia fulani kila mtu arudi kwao.
 
Hata kama wanatishia tu ni hivi msg sent delivered in full package. Watawala wajue chochote kinawezekana.

New Tanganyika ipo karibu kuzaliwa.
Ukiona mpaka ayo kapost kuna watu watalala na viatu,

Tuheshimiane nchi siyo ya familia fulani kila mtu arudi kwao.
Leo Lissu yupo mahabusu kwa sababu kuna watu wameshindwa kudili na siasa kisiasa, wakakimbilia mihimili ya mahakama iwaokoe. Na nyie leo mnaunga mkono jeshi iingizwe katika mambo ya kisiasa. Mnafeli sana.
 
Wanatamani lakini haitatokea , hata wewe huwezi kujitoa kwa hawa wa Tz ambao hawana tofauti na nyumbu, siku ukijitoa kwaajili yao mambo yakiharibika wao watakuacha mwenyewe, walimuacha mbowe peke yake kwenye maandamano akajikuta yuko barabarani yeye na binti yake tu, wameiacha familia ya mdude , soka na wengine waliopotea kwenye harakati za kupinga serekali wameziacha familia za hao watu peke yao.

Wamemuacha Lissu anatoboa miezi 6 mahabusu hata kuandamama kwaajili yake wanaogopa, sasa ndo mtu a take risk kupindua serekali kwaajili ya hawa nyumbu ambao mambo yakiharibika wanakuacha peke yako kazi kukata viuno tiktok !
Hilo halitatokea.
 
Ikiwa vyama vya kisiasa vinaminywa unashauri nini?
Vyama vya siasa vimejaa mapandikizi. Wananchi walitakiwa wenyewe kwa umoja wao wasimamie kile wanachokitaka na mwanasiasa yoyote anayewakwamisha walitakiwa wamuwajibishe.

Viongozi wa kweli watajulikana katikati ya fukuto la shinikizo la wananchi.
 
Back
Top Bottom