Barbarosa
JF-Expert Member
- Apr 16, 2015
- 22,584
- 27,838
Kwa jinsi Magufuli alivyojiweka tangu awe Rais
naamini kabisa mtu yeyote anaetaka kumshauri jambo ambalo
anajua kabisa Rais 'hatalipenda' atahitaji kuwa na 'ujasiri'
na 'uzalendo' na kujitolea sana kwa maslahi ya Taifa...
Lakini hiyo kazi ni lazima 'awepo mtu' wa kuifanya
kwa faida yetu sote......
Hili la sukari limethibitisha kabisa kuwa 'washauri' wakiwa waoga
na watu wa kuongea tu ya kumpendeza Rais...basi 'mambo yanaharibika kama hivi'
Sasa badala ya Rais kuzungumza namna ya kwenda mbele..sasa Rais anaagiza polisi kukamata 'wafanyabiashara wa sukari'......walioficha sukari...
Washauri wangemzuia palepale Rais kupiga marufuku uagizaji sukari
na wakamwambia wazi viwanda vyetu vinazalisha nusu tu ya mahitaji
huku kote tusingefika......
Ukiwa ni mtu ambae Rais anakuamini wakati mwingine unapaswa kuongea kitu
ambacho hakipendi lakini unajua ni kweli na ni faida kwa taifa...
Niliwahi tazama filam ya Fidel Castro...kuna kitu kilinivutia mno
Che Guevara na Raul Castro walikuwa si tu wanamshauri Fidel
lakini pia sometimes 'wamamfokea kabisa'...hadi anaelewa 'makosa' yake...
Magufuli anahitaji watu wa karibu wanaoweza kumshauri ukweli na akikosea wanamwambia wazi 'hili ni kosa umefanya.'
je anao watu hao?
Kwani wewe Raisi Magufuli kama binadamu amekukosea nini mpaka umchukie kiasi hicho, kwa maana umesema wanaompenda ina maana wewe haumpendi, sasa embu tuambie amekukosea nini kwa maana umekwenda mbali sana, hizi ni siasa tu fisadi Lowasa hakujui na wala hatominya hata kope yake jicho akisikia siku umeanguka, hivyo acha chuki kwa mtu usiyemjua kwa sababu ya siasa!