GE2025 Mnaolitegemea Jeshi imekula kwenu!

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025
That's what they are
 
Wakati nakubaliana na wewe kuwa wanajeshi wetu ni mandina na waoga kama tu tulivyo sisi watanzania wa kawaida...

...Hata wao pia baadhi yao wamechoshwa na huyu boss wao wa sasa ambaye haheshimu viapo vyake vya kikatiba na wala haliheshimu hata hilo jeshi lenyewe.

...Hivyo basi kama ambavyo sisi watanzania wa kawaida tuna tamani kuiangusha serikali ya Samia ila hatujui tuanzie wapi, hata wap pia wanatamani sana hichi kitu kitokee ila ndiyo hivyo tena hawajui wafanye vipi.

Kwa hiyo sasa hapo kinachosubiriwa ni sisi wanainchi kulianzisha, ambapo wao watakuja kumalizia tu kwa kutupa support, kama ilivyotokea Madagascar.

Kule Madascar yule bwana mdogo alikuwa ameshachokwa siku nyingi sana na jeshi lake, na ndio maana juzi baada ya police kuzidiwa nguvu na waandamanaji aliamuru jeshi liingilie kati kumsaidia, surprisingly jeshi likakaidi amri yake na kuungana na waandamanaji, sasa hivi amejificha kwenye uvungu wa meza pale France Embassy.

Nakuhakikishia hata sisi wanajeshi wanasubiri kufanya kile ambacho wanajeshi wa Madagascar
 
Tangu jeshi letu lilivyojiingiza kwenye mgogoro wa mashariki ya Congo na kuzingirwa kiboya na M23, hatimaye kutekwa kabisa... Sina imani kabisa na JWTZ.
Jeshi limetekwa kisiasa na kuacha kabisa majukumu yao ya msingi, ni kiashirio kuwa hata amri zinazotolewa na kutekelezwa na askari wapiganaji zina mkanganyiko!.
Silioni tena lile jeshi lililozima shambulizi la Iddi Amin mwaka 1970 au lile lililomng'oa Idd Amin miaka kumi baadaye. 😇
 
Huu ni ujumbe mujarab na wenye uzito kwa wanajeshi wa kada za chini.(sent n delivered). Kazi kwao.
 
Nasikia walichalazwa bakora za kutosha, baadae wakafurushwa na kurudi kimyakimya
 
Kutegemea jeshi lilete demokrasia, haki na uhuru ni contradiction.

Jeshi linatawala kijeshi na halina guarantee yoyote ya kuheshimu demokrasia, haki wala uhuru wa watu.

Watanzania wanaotajataja sana jeshi lichukue nchi wengi wana tabia hizi.

1. Wako desperate. Desperate people do desperate things. Mfa maji haishi kutapatapa. Mtu anayezama hata akiona unywele ataushika ili asizame.

2. Wavivu. Watu wavivu wanapenda kuwapangia wengime wafanye kazi wanayotakiwa kufanya wao. Badala ya wao kufanya wajibu wao kuitoa serikali wanayoona dhalimu madarakani, wanalisukumia wajibu huo jeshi.

3. Wanapenda shortcuts. Badala ya kufanya kazi kubwa na nzito ya kuelimisha jamii ili jamii ijue uhuru ni nini, ifanye mabadiliko ya kimsingi ya kijamii, wanakimbilia shortcut ya kutaka jeshi lichukue madaraka.

4. Wanapenda kutumia nguvu kuliko kutumia akili. Ni watu ambao wanaona jeshi ni alama ya kutumia nguvu. Wanaamini katika kutumia nguvu sehemu ambayo panatakiwa kutumia akili. Wanapenda show za kibabe. Ndiyo maana hata marais ambao hawamo jeshini ukiondoa vyeo vya kisiasa kama Commander In Chief, wanapenda kuvaa magwanda ya kijeshi. Wanasiasa washajua wakivaa magwanda ya kijeshi wananchi wanalainika. Just the projection of military power does it for most Tanzanians.

5. Hawana akili za kuangalia mambo kama unintended consequences, bad precedent, na madhara ya muda mrefu ya mapinduzi ya kijeshi. Kifupi ni watu wenye akili fupi sana ambao hawawezi kupima mambo kwa kina.
 
5. Hawana akili za kuangalia mambo kama unintended consequences, bad precedent, na madhara ya muda mrefu ya mapinduzi ya kijeshi. Kifupi ni watu wenye akili fupi sana ambao hawawezi kupima mambo kwa kina.
Jeshi kuchukua madaraka ya kuongoza nchi ni precedent mbaya sana.

Ni mbaya kwa sababu inatoa ‘uhalali’ kwa jeshi hilo hilo kuitoa madarakani serikali ingine kwa sababu tu serikali hiyo haikidhi matarajio ya wananchi.

Matokeo yake unatengeneza a vicious circle ambayo ni ngumu kujinasua.

Itakuwa kila inapotokea watu hawaipendi serikali iliyopo, solution ni jeshi kuchukua nchi.

Pia, sidhani kama watu wamefikiria kwa kina kuhusu kuishi chini ya martial law!
 
Naam.

Na hakuna serikali inayopendwa na watu wote.

Maana yake hapo umeingia katika mtego wa kukubali mapinduzi ya kijeshi muda wowote na wote.
 
Hv ccm ni nani na ni wangapi?
Usidhan kwamba ccm ni kikundi cha kamati kuu pale chadomo kwamba wanahesabika!
 
Kama jeshi limeshindwa kulinda wananchi kwanini tusiombe majeshi kutoka nje yaje yatulinde kama ilivyo kongo la muhimu sisi raia tuyaunge mkono majeshi ya nje
 
Atleast iko sawa kuliko Afya,polisi na Walimu ...nasikia asiyekua na cheo chochote anapewa zaidi ya 900k.

Humu wanajeshi wapo watatusaidia
Luteni, mwenye nyota 2 anachukua take home zaidi ya 2m.
 
Kama jeshi limeshindwa kulinda wananchi kwanini tusiombe majeshi kutoka nje yaje yatulinde kama ilivyo kongo la muhimu sisi raia tuyaunge mkono majeshi ya nje
Jeshi (JWTZ) linawalinda wananchi dhidi ya kuvamiwa na majeshi ya nje, linalinda mipaka.

Idi Amin alipovamia Tanzania Jeshi lilikuwa na wajibu wa kuilinda nchi, kuwalinda Watanzania.

Kazi ya kulinda usalama wa raia ndani ya nchi ni kazi ya Polisi.

Ndiyo maana ukivamiwa na majambazi nyumbani kwako unaenda Polisi, huendi JWTZ.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…