Mnamuona Hamisi Kigwangalla anavyozunguka huko maporini?

Mnamuona Hamisi Kigwangalla anavyozunguka huko maporini?

Huko maporini kuna mahoteli makali balaa. Kwa hiyo mheshimiwa inawezekana kaenda kurusha karoho kake huko kwa muda ili kuondoa sitress za dar! 😉😉😉
Umenikumbusha ya Simba..chawene akiwa waziri wa Nishati na madini.
 
Hii tumbua tumbua ya juzi ni kama imewastua mawaziri waoga wa maisha na kujipendekeza. Sasa hivi kila siku ni Mbarawa, Lugola, Kigwangwala na Ummy mwalimu. Naona wanatembea na waandishi wa habari kabisa ili kumhadaa mkulu wanafanya kazi.
haha kama kuna kaukweli hivi wajamen mweeeh! Maana hata Mbarawa nae kasala eti hhaaa
 
Huyu jamaa ni muda wa mwezi sasa, kila siku kwenye taarifa ya habari ni ziara zake katika hifadhi na mapori mbalimbali huku akiwa katika magwanda ya maliasili.
Ni wakati sasa wa kumpa credit zake, japo nae kazidisha sana makamera.
Nimemuona leo dah,naona jamaa kasahau hata kunyoa ndevu.Yes,hapa kazi tu.Hongera JPM.
 
Anakosea tu kwenye micamera kila siku ,ila upande mwingine ana staili merit,wenzake waliopita walikua wakishinda nje ya nchi kula bata ,yeye ni Mbuga kwa mbuga
 
Kuzunguka kwake huko maporini n kwenye hifadhi sijui kunaongeza vipi watalii.
Akikaa ofisi...maneno akienda field maneno...!!? Vipi ninyi !?

Nimeisha pata sababu nikipewa nafasi ya kuongoza...mimi washauri wangu wakuu watakuwa ni vitabu vya miiko ya uongozi, majukumu ya kiuongozi kulingana na kazi nitayopewa, kanuni taratibu, ilani ya Chama kitakachokuwa madarakani, sera, mipango ya serikali ya muda mrefu na muda mfupi, sheria za nchi, na Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania na Kitabu kitukufu cha Imani yangu baaasi!!!. Yaani sisikilizi cha mtu labda wale tu watu maalumu kwa ajiri ya kunishauri tena kwenye utaratibu maalumu. Yaani baadhi ya watanzania (kama siyo wapinzani wetu wa kimaendeleo wa ndani na nje ya nchi), mnachosha.
 
Hajazidisha chochote!
Tena anatakiwa kuishi huko!
Asante sana kwa kumpa credit!
Mola akuzidishie baraka Waziri wetu!
 
Akikaa ofisi...maneno akienda field maneno...!!? Vipi ninyi !?

Nimeisha pata sababu nikipewa nafasi ya kuongoza...mimi washauri wangu wakuu watakuwa ni vitabu vya miiko ya uongozi, majukumu ya kiuongozi kulingana na kazi nitayopewa, kanuni taratibu, ilani ya Chama kitakachokuwa madarakani, sera, mipango ya serikali ya muda mrefu na muda mfupi, sheria za nchi, na Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania na Kitabu kitukufu cha Imani yangu baaasi!!!. Yaani sisikilizi cha mtu labda wale tu watu maalumu kwa ajiri ya kunishauri tena kwenye utaratibu maalumu. Yaani baadhi ya watanzania (kama siyo wapinzani wetu wa kimaendeleo wa ndani na nje ya nchi), mnachosha.
Well said
 
Angekuwa wizara ya mambo nje.
Kwa hulka hii..
Mkulu angemruhusu kweli?
 
Kuna mengi sana kwenye vitengo au sijui taasisi.. mnaita.. ni panahitaji mengi kutendeka pia.
 
Huwa najiuliza Sana, taarifa za Habari ITV na [emoji342] TV nyingine za bongo hakuna Habari zaidi ya mawaziri hawa, ukiangalia CNN ni tofauti kabisa
 
Kiufupi hivi anavyofanya kigwangala ni juhudi sana lakini ukifuatilia utagundua anafanya kwa woga kuhusu kitumbua chake hivyo anajitahidi kumeki headlines aonekane naye yupo bussy
 
Kwa muda mrefu nimekuwa najiuliza hili swali. Hamisi ni msanii kama walivyo wateule wengi wa jiwe
Yule ananyota ya mgambo alipopewa unaibu wizara ya afya akakimbilia getini kulinda sasa kapewa uwaziri wa utalii kageuka kuwa mgambo wa hifadhi za wanyama
Wizara ya maliasili na utalii ni zaidi ya uwo usanii anaofanya maporini
 
Huyo jamaa ni kituko haswaa. Utamuona mara anabiringika kwenye maporomoko mara anatambaa kama nyoka mwisho wa siku tutaambiwa "WANAZURURA TU HUKO" Naona ameamua kujiita hadi "Mzee wa pori kwa pori"

Anakula tu vumbi hadi machoni!

Teh teh teh jiwe utakuja kulipia huu utumwa ujue!
 
Watanzania hawana jema!!!!....

Mtumishi akishinda ofisini maneno

Akiwajibika pia ni maneno...
 
Kafanya kazi nzuri, mapori yaliyoelekea kumalizwa na mifugo sasa hali imerejea upyaaaa - viva waziri
 
Huyu jamaa ni muda wa mwezi sasa, kila siku kwenye taarifa ya habari ni ziara zake katika hifadhi na mapori mbalimbali huku akiwa katika magwanda ya maliasili.
Ni wakati sasa wa kumpa credit zake, japo nae kazidisha sana makamera.
Lakushangaza kila mwezi pori la kule simiyu anafanya ziara huko mara kwa mara sijui vile vitalu ni vyake,,
 
Back
Top Bottom