Mnamkumbuka mzee Magambo?

Mnamkumbuka mzee Magambo?

Wewe ukadhani dsm wote tumekulia ushwazi..??? Kuna mtu hajawahi panda daladala hapa dsm..
Hahaha mkuu ilitawala uda na ikalusi kumbakumba gari zenu zikiharibika mlikuwa mnapanda kulikuwa na luti za masaki mpaka maiki o cheni(mikocheni)
 
Alikuwa maarufu sana watoto wengi nikiwemo na Mimi tulikuwa tukimuogopa,alikuwa akiuza Karanga kwenye Kikapu sambamba na kuimba alikuwa akivalia kiasili,,,nimegundu humu jf wengi ni watoto ama ni mangosha yamekuja mjini wamekula idi mbili tatu afu wanasumbua
Kuna kitu kinakupungua ndugu, unafikiri kila aliyemo JF ni mtu wa mjini? Au unafikiri kila unayemjua ni lazima wote wamjue?
 
Kamasikosei alikua akiitwa Majambo, kwahakika yule alikua ni kiboko ya watoto, maana kile kinyago changozi na yale meno sijui yalikuwa ya mnyama gani, kichwani anafunga manyoya ya ndege, sura ya kile kinyago ilitishasana watoto.
Na yule jamaa alikua anazunguka karibu DSM yote kwa nyakati tofauti. Ukiacha uuzaji wa karanga ilikua mteja unatoa fedha ili yeye aimbe na kucheza. Mkono mmoja ana manyanga mkono mwingine ameshika kapu la karanga, kifuani amevaa ngozi sijui ya mnyama gani, usoni amevaa kinyago cha ngozi chenye meno ya kutisha.

Ile ilikua miaka ya 80 ni kitambo kidogo. Enzi za mwanafunzi kulipa sentano kwenye uda. Uwanja wa taifa kuna mlango wa kuingia watoto/wanafunzi kuangalia mpira kwa shilingi tano.

Dar ilikua haina foleni kama leo. Bustani za mnazi mmoja ilikua sehemu ya watu kupumzika, Kwenye uzio wa ikulu mnakwenda kuangalia ndege na wanyama. Dar ilikua haina Joto kama ilivyo sasa. Mleta mada umenikumbusha mbali.
Salaam mhenga mwenzangu
 
Miaka ya 80 kulikuwa na mtu kama huyo maeneo ya Kigogo ila tulikuwa tunamwita KILAMBO.
Sijajua kama ndiyo huyo au?
 
Kamasikosei alikua akiitwa Majambo, kwahakika yule alikua ni kiboko ya watoto, maana kile kinyago changozi na yale meno sijui yalikuwa ya mnyama gani, kichwani anafunga manyoya ya ndege, sura ya kile kinyago ilitishasana watoto.
Na yule jamaa alikua anazunguka karibu DSM yote kwa nyakati tofauti. Ukiacha uuzaji wa karanga ilikua mteja unatoa fedha ili yeye aimbe na kucheza. Mkono mmoja ana manyanga mkono mwingine ameshika kapu la karanga, kifuani amevaa ngozi sijui ya mnyama gani, usoni amevaa kinyago cha ngozi chenye meno ya kutisha.

Ile ilikua miaka ya 80 ni kitambo kidogo. Enzi za mwanafunzi kulipa sent hamsini/thumni kwenye uda. Uwanja wa taifa kuna mlango wa kuingia watoto/wanafunzi kuangalia mpira kwa shilingi tano.

Dar ilikua haina foleni kama leo. Bustani za mnazi mmoja ilikua sehemu ya watu kupumzika, Kwenye uzio wa ikulu mnakwenda kuangalia ndege na wanyama. Dar ilikua haina Joto kama ilivyo sasa. Mleta mada umenikumbusha mbali.
Dah! kweli kabisa wakati kutembea kutoka kinondoni kwenda airpot kwa mguu kuangalia ndege ilikuwa kitu cha kawaida sana haijalishi una umri gani,kwenda pale Drive In kuangalia sinema lakini mpo nje hata sauti hamsikii hahaaaaaa!
 
Kuna kitu kinakupungua ndugu, unafikiri kila aliyemo JF ni mtu wa mjini? Au unafikiri kila unayemjua ni lazima wote wamjue?
Ungesoma heading ya huu uzi usingeuliza hili swali,ila kwa vile umekurupuka....
 
Miaka ya 80 kulikuwa na mtu kama huyo maeneo ya Kigogo ila tulikuwa tunamwita KILAMBO.
Sijajua kama ndiyo huyo au?
Ndiye huyo huyo mkuu, wazawa wa mji huu wote tunamjua.

Chinichini ilikuwa inavuma jamaa ni usalama.[emoji16][emoji16][emoji16]
 
Kamasikosei alikua akiitwa Majambo, kwahakika yule alikua ni kiboko ya watoto, maana kile kinyago changozi na yale meno sijui yalikuwa ya mnyama gani, kichwani anafunga manyoya ya ndege, sura ya kile kinyago ilitishasana watoto.
Na yule jamaa alikua anazunguka karibu DSM yote kwa nyakati tofauti. Ukiacha uuzaji wa karanga ilikua mteja unatoa fedha ili yeye aimbe na kucheza. Mkono mmoja ana manyanga mkono mwingine ameshika kapu la karanga, kifuani amevaa ngozi sijui ya mnyama gani, usoni amevaa kinyago cha ngozi chenye meno ya kutisha.

Ile ilikua miaka ya 80 ni kitambo kidogo. Enzi za mwanafunzi kulipa sent hamsini/thumni kwenye uda. Uwanja wa taifa kuna mlango wa kuingia watoto/wanafunzi kuangalia mpira kwa shilingi tano.

Dar ilikua haina foleni kama leo. Bustani za mnazi mmoja ilikua sehemu ya watu kupumzika, Kwenye uzio wa ikulu mnakwenda kuangalia ndege na wanyama. Dar ilikua haina Joto kama ilivyo sasa. Mleta mada umenikumbusha mbali.

Mkuu unanitoa machozi. Nakumbuka mbali sana. Nahisi atakuwa ameshafariki ila Sipo sure maana miaka ile ya 80+ alikuwa mtu mzima kiasi[emoji24][emoji24]
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom