Mnaionaje hii safu ya CHADEMA 2014-2019

Mnaionaje hii safu ya CHADEMA 2014-2019

Nani kakupa ruksa kuwaweka hao Waislam kwenye safu za uongozi hauoni kama utakuwa msaliti.
 
Ndani ya CHADEMA watu wa kanda nyingine wasahau kabisa kupata uongozi. hicho ni chama chao.
 
Kama katiba ingeruhusu hata Kamanda mkuu wa Red brigade angekuwa anachaguliwa ili kukabiliana na hawa maintarahamwe. Na ninayempendekeza angekuwa mimi mwenyewe kamanda Chakaza. Huko tunakokwenda hujuma za maccm zitashika kasi kubwa na inahitajika kuwa na kikosi makini kupambana na hujuma hizo kwa nguvu zote.


Sent from my iPad using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Nani kakupa ruksa kuwaweka hao Waislam kwenye safu za uongozi hauoni kama utakuwa msaliti.

Hivi nyie CCM kabla ya kupewa uongozi kumbe mnaulizana dini? Ona hii. Rais mwislamu,makamu wa Rais mwislamu,Rais wa Zanzibar mwislamu,makamu wa kwanzana wa pili Zanzibar waislamu, katibu mkuu CCM mwislamu nk nk.
Mbona hilo watu hawalisemei? Acheni fikra za kidini katika utawala mtajiumbua bure.


Sent from my iPad using JamiiForums
 
Hii nimeitoa hukooooo.....Kuna mtu kapendekeza. Mimi pia imenivutia. Hebu sema lolote!!!


Imependekezwa kama ifuatavyo:

CHAMA CHENYEWE:
Mwenyekiti: Freeman Aikael Mbowe
Makamu Mwenyekiti Bara: Prof. Abdalah Safari
Makamu Mwenyekiti Zanzibar: Issa Issa Mohamed
Katibu Mkuu: Dr. Willbrod Peter Slaa
Naibu Katibu Mkuu Bara: Tundu Antiphas Lissu
Naibu Katibu Mkuu Zanzabar: Hamad Yusuph
Habari na Uenezi: John Mnyika

JUMUIYA ZA CHAMA:

BAWACHA:
Mwenyekiti: Halima Mdee
Makamu Mwenyekiti: Suzan Kiwanga/ Mhe. Maryam Msabaha/ Rose Mayemba
Katibu: Paulina Gekul/Naomi Kaihula

BAVICHA:
Mwenyekiti: Ben Saanane
Makamu Mwenyekiti: Atoke Zanzibar
Katibu: Mohamed Mtoi

BARAZA LA WAZEE:
Mwenyekiti: Mzee Sylivester Masinde
Makamu Mwenyekiti: Mzee Peter Mpema (Kata ya Somangira, Tawi la Kizani - Kigamboni)
Katibu: Prof. Mwesiga Baregu


NB: Nimelazimika kupendekeza Mhe. Tundu Lissu awe Naibu Katibu Mkuu wa Chama upande wa bara kwa sababu sioni tofauti iliyopo baina ya Mkurugenzi wa Sheria na Mwanasheria wa Chama. Akiwa kama Naibu Katibu Mkuu aweza pia kufanya kazi za kisheria zinazihusu chama kama wafanyavyo Mabere Marando na Prof. Abdalah Safari.

Aidha, safu yangu hii niliyopendekeza nimezingatia Changamoto ambazo CHADEMA imekuwa ikipitia na pengine itaendelea kupitia hasa masuala ya Propaganda za Ukanda na Udini.

Zaidi mapendekezo yangu yamejikita katika watu wenye nguvu na ushawishi kwa Umma wa Watanzania. Mapendekezo yangu yamelenga sana kwamba hii Safu mpya ya Uongozi kila mtu awe na uwezo wa kupanda jukwaani na kutema cheche. Tunakubalina kimsingi kuwa watu tuna vipaji tofauti. Wakati wengine wana kipaji cha kaundika na kusoma maandishi, wengine wana vipaji vya kuyaongea hayo maandishi na kuyanakshi vizuri na yakaeleweka miongoni mwa wasikilizaji. Hao wote niliowapendekeza bila shaka mtakubaliana nami kuwa ni waongeaji wazuri katika majukwaa.

Tunataka BAWACHA yanye Mwenyekiti, Makamu mwenyekiti na Katibu machachari kwelikweli. BAWACHA itakayotembea nchi nzima kuwaamsha akina mama ndani ya miezi tisa hadi kumi baada ya uchaguzi na kuzindua Vuguvugu mbalimbali kama ambavyo Conchester Rwamlaza anafanya kule Mkoani Kagera au kule Mkoani Geita kwa Kamanda Husna Amri. Tunataka wanawake waamke kwa vyovyote vile.

Tunataka BAVICHA itakayouwaunganisha vijana. BAVICHA itakayoendelea kuvutia wasomi zaidi. BAVICHA itakayowashawishi, wasomi wetu baada ya kumaliza vyuo vikuu wale wenye interest na siasa wakagombee kwenye maeneo yao kuanzia Udiwani. BAVICHA itakayokwenda kupata vijana kuanzia Shule za Msingi, Sekondari ya Kati na juu hadi vyuo vya Ufundi....Hapa ndio maana BEN SAANANE anatakiwa kuongoza jahazi hili

Tunataka BARAZA LA WAZEE wenye hekima na msimamo. Wazee walio tayari kukifia Chama. Hapa Mzee Sylivester Masinde na Katibu akiwa Prof Baregu nina hakika CHADEMA 2015 Ikulu itakuwa nyeupe kupitia washirika wetu wa CUF, NCCR, DP na NLD

Aluta Continua
As much as I respect Freeman Mbowe and Dr Wilbroad Slaa but I think it's time for CHADEMA to have new faces on the echelons of its leadership. Kwa mliosoma Consumer Psychology bila shaka mtakuwà mnafahamu kwanini adverts or products zinabadilishwa kimwonekano kila baada ya muda fulani.Ni ukweli usiopingika kuwa akina Mbowe wamezoeleka mno na Wananchi kiasi kwamba watu wanahisi hakuna jipya kutoka kwao.Kuweka Uongozi mpya hakumaanisha kubadilisha sura ya uongozi tu bali pia ni kwaajili ya mambo ya kimkakati. There are some negative arguments against the Party need to be buried for good by reforming the Party's image into positive one.
 
Wewe Una mapendekezo gani? Nani kakufundisha kuwa uongozi unaparikana kwa kuangalia Kanda?
 


Imependekezwa kama ifuatavyo:

CHAMA CHENYEWE:
Mwenyekiti: Freeman Aikael Mbowe
Makamu Mwenyekiti Bara: Prof. Abdalah Safari
Makamu Mwenyekiti Zanzibar: Issa Issa Mohamed
Katibu Mkuu: Dr. Willbrod Peter Slaa
Naibu Katibu Mkuu Bara: Tundu Antiphas Lissu
Naibu Katibu Mkuu Zanzabar: Hamad Yusuph
Habari na Uenezi: John Mnyika


Fanya Editing kidogo, naamini Mnyika ni zaidi ya kuwa mwenezi wa chama, tuna vijana wengi tu wanaweza kufanya kazi ile.

Naibu Katibu Mkuu Bara: John Mnyika

Tundu Antiphas Lissu:
Aendelee na kitengo chake cha sheria, tunamwitaji mwanasheria mahili kwani chama sasa kinaenda kushika dola, misingi ya kisheria inahitajika sana!!
 
Ndani ya CHADEMA waislam hawana nafasi. Prof Safari asahau kabisa

kujieleza na kutoa maoni ni haki ya kila mwanadamu. Kwa hivyo hata vichaa kama wewe mna haki pia
 
As much as I respect Freeman Mbowe and Dr Wilbroad Slaa but I think it's time for CHADEMA to have new faces on the echelons of its leadership. .
Sidhani ni jambo la busara kubadilisha rubani wakati ndege ipo angani, hata hivyo hao ambao wanaona wanafaa kuingoza CDM basi wajitokeze hakuna anayewazuia kwani uchaguzi huo umeshafika.

Nafasi ya ukatibu mkuu ni ya uteuzi, ni busara tu za mwenyekiti ajaye kuona ni yupi anamfaa kwenye safu yake ya uongozi ili amchague na aidhinishwe na kamati husika za chama.
 
Safu nyepesi sana hiyo. Ni zaidi ya timu ya Brazil iliyopigwa 7-1 na Ujerumani huku ikiwaacha hoi wapenzi na washabiki wake. Ndivyo itakavyotokea ka chadema

you're hit!
 
Bora ww umeongea ukweli mkuu,mwenyekiti wa bavicha si lazima atoke zenj coz atakuwa Muislam
Naibu katibu mkuu lissu ? Hapana, apangwe mwingine, makamu mwenyekiti Bawacha apangwe Esther Wassira, makamu mwenyekiti Bavicha si lazima atoke Zanzibar, na bado wengine potential watajitokeza, tusubiri
 
sio campaign ila main goal ya iyo safu ni kuhakikisha tunashika dola na kuongeza umaarufu wa chama au unazani iyo safu imweka kwa ajili ya nini mzeee lakini na wewe ni haki yako ya kikatiba kucomment
Hizi ni campaign sasa. Ila ni haki yako kikatiba kutoa maoni yako
 
Nani kakupa ruksa kuwaweka hao Waislam kwenye safu za uongozi hauoni kama utakuwa msaliti.
Ritz utaacha lini mambo ya Udini mkuu?
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom