Mnaionaje hii safu ya CHADEMA 2014-2019

Mnaionaje hii safu ya CHADEMA 2014-2019

Maoni mema sana lakini #Bavicha ningependa kuiona sura ya #Mwakibinga Jamaa yuko vyema sana ktk kuunganisha vijana

Ni kweli asee, ila akiwa katika zile Kamati za Utekelezaji/Uhamasishaji BAVICHA nchi nzima itakuwa powa sana. Ingawa Yes if not Ben basi Philliph Mwakibinga... KUSHOKA
 
Last edited by a moderator:
Bora ww umeongea ukweli mkuu,mwenyekiti wa bavicha si lazima atoke zenj coz atakuwa Muislam
BOMBAY hata Bara kuna waislam pia kama ilivyo kwa Wakristo. Hoja haikuwa Dini ya mtu, bali kubalance maeneo watokako viongozi ili kuleta Sura ya Kitaifa. Thanx for the concern anyway
 
Last edited by a moderator:
Sidhani ni jambo la busara kubadilisha rubani wakati ndege ipo angani, hata hivyo hao ambao wanaona wanafaa kuingoza CDM basi wajitokeze hakuna anayewazuia kwani uchaguzi huo umeshafika.

Nafasi ya ukatibu mkuu ni ya uteuzi, ni busara tu za mwenyekiti ajaye kuona ni yupi anamfaa kwenye safu yake ya uongozi ili amchague na aidhinishwe na kamati husika za chama.
FUSO you seem to know CHADEMA's protocols. Thanx
 
Last edited by a moderator:
Wewe Una mapendekezo gani? Nani kakufundisha kuwa uongozi unaparikana kwa kuangalia Kanda?

Kuchagua viongozi kwa kuangalia Kanda ama maeneo watokako sio Sheria na wala haijaandikwa popote Mkuu tweve ila ni busara tu ya kawaida inaongoza kufikiria kufanya Uteuzi ama Uchaguzi kwa kuweka kigezo hicho kisicho rasmi lakini muhimu sana...Otherwise you have the Point
 
Last edited by a moderator:
Fanya Editing kidogo, naamini Mnyika ni zaidi ya kuwa mwenezi wa chama, tuna vijana wengi tu wanaweza kufanya kazi ile.

Naibu Katibu Mkuu Bara: John Mnyika

Tundu Antiphas Lissu:
Aendelee na kitengo chake cha sheria, tunamwitaji mwanasheria mahili kwani chama sasa kinaenda kushika dola, misingi ya kisheria inahitajika sana!!

Nimekusoma Mkuu FUSO. Ila nina angalizo kwamba Tayari kuna Kurugenzi ya Sheria ambapo Kamati Kuu ilimuidhinisha Peter Kibatala kuiongoza wakati huohuo Tundu Lissu akapewa nafasi ya Mwanasheria wa Chama. Kwa maoni yangu. Wote Tundu Lissu, Peter Kibatala na hata Albert Msando ni wanasheria wa Chama. Kwa hiyo hiyo nafasi ya Tundu Lissu itoke. Tubaki na Kurugenzi. Hata tunapoandika Organogram inasomeka.....
 
Last edited by a moderator:
Kama katiba ingeruhusu hata Kamanda mkuu wa Red brigade angekuwa anachaguliwa ili kukabiliana na hawa maintarahamwe. Na ninayempendekeza angekuwa mimi mwenyewe kamanda Chakaza. Huko tunakokwenda hujuma za maccm zitashika kasi kubwa na inahitajika kuwa na kikosi makini kupambana na hujuma hizo kwa nguvu zote.


Sent from my iPad using JamiiForums
Chakaza wewe ni mdau muhimu sana kama lilivyo jina lako...Kaa tayari muda wote
 
Last edited by a moderator:
Hapa tz hakipo chama hata ki1 cha dini! labda Misri, Libya, Iraq n.k; anayesema kuna chama cha kidini hapa tz huyo ni mjinga mwenye uelewa mdogo mpaka ubustiwe kwanza
 
As much as I respect Freeman Mbowe and Dr Wilbroad Slaa but I think it's time for CHADEMA to have new faces on the echelons of its leadership. Kwa mliosoma Consumer Psychology bila shaka mtakuwà mnafahamu kwanini adverts or products zinabadilishwa kimwonekano kila baada ya muda fulani.Ni ukweli usiopingika kuwa akina Mbowe wamezoeleka mno na Wananchi kiasi kwamba watu wanahisi hakuna jipya kutoka kwao.Kuweka Uongozi mpya hakumaanisha kubadilisha sura ya uongozi tu bali pia ni kwaajili ya mambo ya kimkakati. There are some negative arguments against the Party need to be buried for good by reforming the Party's image into positive one.

Mkuu TEKNOLOJIA ungekuja na Pendekezo ili tuwajadili hao unaodhani wanaweza kuwa New faces na wakaweza kukabiliana na Changamoto zilizopo kwa sasa. Hoja yako ni njema sana
 
Last edited by a moderator:
Naona umezingatia kabila japo si kwa kiasi kikubwa sana. Sijui kama Mtei atakubali pendekezo lako. Kwa sababu azimio lililopo ni kuwa baada ya uchaguzi wa chama mwaka huu, vikao vitaendeshwa kwa kutumia kabila letu, ili kuzuia taarifa za kikao kuvuja kiholela.

Hii nimeitoa
hukooooo.....Kuna mtu kapendekeza. Mimi pia imenivutia. Hebu sema
lolote!!!


Imependekezwa kama ifuatavyo:

CHAMA CHENYEWE:
Mwenyekiti: Freeman Aikael Mbowe
Makamu Mwenyekiti Bara: Prof. Abdalah Safari
Makamu Mwenyekiti Zanzibar: Issa Issa Mohamed
Katibu Mkuu: Dr. Willbrod Peter Slaa
Naibu Katibu Mkuu Bara: Tundu Antiphas Lissu
Naibu Katibu Mkuu Zanzibar: Hamad Yusuph
Habari na Uenezi: John Mnyika

JUMUIYA ZA CHAMA:

BAWACHA:
Mwenyekiti: Halima Mdee
Makamu Mwenyekiti: Suzan Kiwanga/ Mhe. Maryam Msabaha/ Rose Mayemba
Katibu: Paulina Gekul/Naomi Kaihula

BAVICHA:
Mwenyekiti: Ben Saanane
Makamu Mwenyekiti: Atoke Zanzibar
Katibu: Mohamed Mtoi

BARAZA LA WAZEE:
Mwenyekiti: Mzee Sylivester Masinde
Makamu Mwenyekiti: Mzee Peter Mpema (Kata ya Somangira, Tawi la Kizani -
Kigamboni)
Katibu: Prof. Mwesiga Baregu


NB: Nimelazimika kupendekeza Mhe. Tundu Lissu awe Naibu Katibu
Mkuu wa Chama upande wa bara kwa sababu sioni tofauti iliyopo baina ya
Mkurugenzi wa Sheria na Mwanasheria wa Chama. Akiwa kama Naibu Katibu
Mkuu aweza pia kufanya kazi za kisheria zinazihusu chama kama wafanyavyo
Mabere Marando na Prof. Abdalah Safari.

Aidha, safu yangu hii niliyopendekeza nimezingatia Changamoto ambazo
CHADEMA imekuwa ikipitia na pengine itaendelea kupitia hasa masuala ya
Propaganda za Ukanda na Udini.

Zaidi mapendekezo yangu yamejikita katika watu wenye nguvu na ushawishi
kwa Umma wa Watanzania. Mapendekezo yangu yamelenga sana kwamba hii
Safu mpya ya Uongozi kila mtu awe na uwezo wa kupanda jukwaani na
kutema cheche. Tunakubalina kimsingi kuwa watu tuna vipaji tofauti.
Wakati wengine wana kipaji cha kaundika na kusoma maandishi, wengine
wana vipaji vya kuyaongea hayo maandishi na kuyanakshi vizuri na
yakaeleweka miongoni mwa wasikilizaji. Hao wote niliowapendekeza bila
shaka mtakubaliana nami kuwa ni waongeaji wazuri katika majukwaa.

Tunataka BAWACHA yanye Mwenyekiti, Makamu mwenyekiti na Katibu
machachari kwelikweli. BAWACHA itakayotembea nchi nzima kuwaamsha akina
mama ndani ya miezi tisa hadi kumi baada ya uchaguzi na kuzindua
Vuguvugu mbalimbali kama ambavyo Conchester Rwamlaza anafanya kule
Mkoani Kagera au kule Mkoani Geita kwa Kamanda Husna Amri. Tunataka
wanawake waamke kwa vyovyote vile.

Tunataka BAVICHA itakayouwaunganisha vijana. BAVICHA itakayoendelea
kuvutia wasomi zaidi. BAVICHA itakayowashawishi, wasomi wetu baada ya
kumaliza vyuo vikuu wale wenye interest na siasa wakagombee kwenye
maeneo yao kuanzia Udiwani. BAVICHA itakayokwenda kupata vijana kuanzia
Shule za Msingi, Sekondari ya Kati na juu hadi vyuo vya Ufundi....Hapa
ndio maana BEN SAANANE anatakiwa kuongoza jahazi hili

Tunataka BARAZA LA WAZEE wenye hekima na msimamo. Wazee walio tayari
kukifia Chama. Hapa Mzee Sylivester Masinde na Katibu akiwa Prof Baregu
nina hakika CHADEMA 2015 Ikulu itakuwa nyeupe kupitia washirika wetu wa
CUF, NCCR, DP na NLD

Aluta Continua
 
Udini utabaki pale pale hao Waislamu wamewekwa kama boya tu
 
Naona mwenyekiti wa chama kaskazini.
katibu wa chama kaskazini.
mwenyekiti bawacha kaskazini.
mwenyekiti bavicha kaskazini.

Chadema sio chama cha ukanda kabisa, ila kanda ya kaskazini inaongoza kwa sababu nyie watu wa kanda zingine hamuaminiki.

BOMBAY hata Bara kuna waislam
pia kama ilivyo kwa Wakristo. Hoja haikuwa Dini ya mtu, bali kubalance
maeneo watokako viongozi ili kuleta Sura ya Kitaifa. Thanx for the
concern anyway
 
Last edited by a moderator:
Peter Msigwa, Heche??? au kwa kuwa hawatoki Kaskazini wala Zanzibar?
 
chama chenyewe kimepoteza muelekeo hiko ukiingia ndani zaidi utaona weengi wametokea kanda moja je inamaana watu wa kanda nyingine hawaaminiki....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom