Nilikuja huku MMU msimu ule ambapo JF ilianza kuhit katika billboard na kupata tuzo za grammy kwa mods kupiga watu ban na kufuta threads za watu hasa jukwaa la siasa na Jamii Intel kipindi kile cha mhemko wa mapinduzi, nyakati za wizi mkubwa na projects kama za Richmond, EPA, Chenge, Karamagi, mvua za kutengeneza, Mkurabita, kilimo kwanza, Babu wa Loliondo, Nabii tito, Nabii Flora etc.,
Sasa wakati huo ilikuwa ukiweka bandiko hasa kama lina misumari lazima linyofolewe, mpaka nilianza kujiuliza hao jamaa wameiteka au kuinunua JF au nini!
Kutokana na hizo adha nikawa nimetua MMU kama mtu aliyekuja mjini kwa mbio za mwenge. Sijui ndio nilikutana na uzi wa AshaDii!
Enzi hizo hakuna mtu anamjua lara 1 (nadhani naye alikuja kwa pepo za monsoon kutoka majukwaa mengine.), The Boss anapewa heshima na kila mtu, pia nilikuwa naamini Kongosho ni mwanamke. Baadaye nilikutana na uzi wa gfsonwin, niliusoma nikaona kama una mantiki. Nilikuwa nasoma nyuzi za watu kama vile nasoma thesis ya mtu mwenye mawazo mapya kabisa.
Nyuzi hizo na zingine zilinipa imani kwamba huenda MMU ni mahali pazuri. Ukizingatia kulikuwa na sexy na romantic threads zilizokuwa zinaibuka kama uyoga, hasa Loveconnect! Basi nikasema hapa si ndio penyewe, mwaka hauishi nitaondoka na mchuchu kutoka huku na kuweka ndani kabisa, mbona wangeisoma namba!
Siku zilienda zikarudi, ndio kidogo kidogo nikaanza kustuka, MMMMMhhhhhh, nyuzi za MMU ni matango pori. Nilijipa moyo nikiamini huenda hizo siku nilikutana na nyuzi za wehu, wote wametoka baa kunywa konyagi.
Kuna siku nilipata hasira, nikawa najiuliza mods wamenipiga ban, lakini kuna watu wanaandika magarasha humu kila kukicha mbona wameachwa tu! Ndio nilipofunguka macho na kugundua, MMU hata kama ingefanyiwa tambiko, tayari ilikuwa haisafishiki!
Kwa mbali wadada walikuwa wanaonekana decent kwa avatar na michango yao. Ni kama walinimotivate kuwasiliana nao, dah, sijawahi kusogea hata hatua moja.
PM mdada, salimiana, fahamiana, mjulie hali kila asubuhi, mtakie jioni njema, mpe maneno mazuri, mkaribishe lunch! Ikija swala la kupanga kukutana, duh, nikutane na nani!
Kuna wadada washawahi kuniweka busy utadhani mie mtumwa wao - nyoooooooo zao! Yaani nakumbuka nilishawahi kulala njaa hivi hivi najiona baada ya kununulia hela ya msosi internet bundle kisa nachat nao - sasa PM nichelewe kuijibu tena si ndio ningejifukuzisha bahati!
Baadaye sana, ndipo nilipogundua kumbe MMU zaidi ya 99% ya watu ni full fake (huenda hata niliochat nao hawakuwa wanawake)! Nitashangaa sana kama misukule, mandondocha, mazombie na hata majini (MziziMkavu) humu MMU hamuna. Hata mizimu labda ipo.
MMU imenipa matumaini fake, yaani muda wa kutosha umesepa tangu 2010 mpaka leo, hakuna the way forward yoyote.
Yaani, wanawake kama sio wote waliomo humu, walio wengi wamepitia suluba za mapenzi, kama vile uchumba sugu, uchumba kuvunjika, kuibiwa wachumba, mahusiano kuisha vibaya, kupewa mimba wasizotarajia, kudanganywa; hata kama wengine wameolewa kuna majanga kama vile mwanaume kununua nyumba ndogo au kupata kiunyoya au kiunywele kutoka mtaani au chuo, etc., (angalia threads zao). Humu wanawake wamejizatiti kama Al-shabaab, nimpate nani?
Yaani unakuta mtu mmebadilishana PMs mwaka mzima, ikitokea siku umemwambia mkutane sehemu, majibu ni "aku, hee makubwa, mmh yamekuwa hayo tena, lol hii mpya, mmmmhh wapi!, thubutu,"
Nimeweka appointments na wadada miezi nenda rudi, ah wapi, hata wale niliowazoea kama akina King'asti, Heaven on Earth, Smile, Cynthia Chriss hawakamatiki. Preta ndio kabisa!
MMU haina maana, inaweza kukuweka pending kama kusubiria vocha ya mkopo au kufuatilia mkopo NMB! Mbona utajuta, utakaposhtuka na umri wako ndio umeyoyoma kama wa Kapuya!
MMU ina wenyewe, magwiji yaliyobobea, mie nimenyosha mikono juu.
Jamani, nilikuja MMU kwa pepo za msimu naondoka na pepo hizo hizo, maana zikinipita nitaendelea kubaki.
CC: mimi49, christine ibrahim, Sista, sister, Ablessed mdida, charminglady, Madame B, madameA madame X, tinna cute, mkunde Original, Mapi, Asnam, Evelyn Salt, Money Stunna, watu8, Himidini, Lady doctor, mwekundu, Nazjaz, Eiyer, Boflo, Mashaxizo, Mshinga, mzabzab, Bujibuji, KOKUTONA, farkhina
BCC: MMU senior bachelors
Kwa hisani ya wana MMU wote.
ufs: @Mods
Sasa wakati huo ilikuwa ukiweka bandiko hasa kama lina misumari lazima linyofolewe, mpaka nilianza kujiuliza hao jamaa wameiteka au kuinunua JF au nini!
Kutokana na hizo adha nikawa nimetua MMU kama mtu aliyekuja mjini kwa mbio za mwenge. Sijui ndio nilikutana na uzi wa AshaDii!
Enzi hizo hakuna mtu anamjua lara 1 (nadhani naye alikuja kwa pepo za monsoon kutoka majukwaa mengine.), The Boss anapewa heshima na kila mtu, pia nilikuwa naamini Kongosho ni mwanamke. Baadaye nilikutana na uzi wa gfsonwin, niliusoma nikaona kama una mantiki. Nilikuwa nasoma nyuzi za watu kama vile nasoma thesis ya mtu mwenye mawazo mapya kabisa.
Nyuzi hizo na zingine zilinipa imani kwamba huenda MMU ni mahali pazuri. Ukizingatia kulikuwa na sexy na romantic threads zilizokuwa zinaibuka kama uyoga, hasa Loveconnect! Basi nikasema hapa si ndio penyewe, mwaka hauishi nitaondoka na mchuchu kutoka huku na kuweka ndani kabisa, mbona wangeisoma namba!
Siku zilienda zikarudi, ndio kidogo kidogo nikaanza kustuka, MMMMMhhhhhh, nyuzi za MMU ni matango pori. Nilijipa moyo nikiamini huenda hizo siku nilikutana na nyuzi za wehu, wote wametoka baa kunywa konyagi.
Kuna siku nilipata hasira, nikawa najiuliza mods wamenipiga ban, lakini kuna watu wanaandika magarasha humu kila kukicha mbona wameachwa tu! Ndio nilipofunguka macho na kugundua, MMU hata kama ingefanyiwa tambiko, tayari ilikuwa haisafishiki!
Kwa mbali wadada walikuwa wanaonekana decent kwa avatar na michango yao. Ni kama walinimotivate kuwasiliana nao, dah, sijawahi kusogea hata hatua moja.
PM mdada, salimiana, fahamiana, mjulie hali kila asubuhi, mtakie jioni njema, mpe maneno mazuri, mkaribishe lunch! Ikija swala la kupanga kukutana, duh, nikutane na nani!
Kuna wadada washawahi kuniweka busy utadhani mie mtumwa wao - nyoooooooo zao! Yaani nakumbuka nilishawahi kulala njaa hivi hivi najiona baada ya kununulia hela ya msosi internet bundle kisa nachat nao - sasa PM nichelewe kuijibu tena si ndio ningejifukuzisha bahati!
Baadaye sana, ndipo nilipogundua kumbe MMU zaidi ya 99% ya watu ni full fake (huenda hata niliochat nao hawakuwa wanawake)! Nitashangaa sana kama misukule, mandondocha, mazombie na hata majini (MziziMkavu) humu MMU hamuna. Hata mizimu labda ipo.
MMU imenipa matumaini fake, yaani muda wa kutosha umesepa tangu 2010 mpaka leo, hakuna the way forward yoyote.
Yaani, wanawake kama sio wote waliomo humu, walio wengi wamepitia suluba za mapenzi, kama vile uchumba sugu, uchumba kuvunjika, kuibiwa wachumba, mahusiano kuisha vibaya, kupewa mimba wasizotarajia, kudanganywa; hata kama wengine wameolewa kuna majanga kama vile mwanaume kununua nyumba ndogo au kupata kiunyoya au kiunywele kutoka mtaani au chuo, etc., (angalia threads zao). Humu wanawake wamejizatiti kama Al-shabaab, nimpate nani?
Yaani unakuta mtu mmebadilishana PMs mwaka mzima, ikitokea siku umemwambia mkutane sehemu, majibu ni "aku, hee makubwa, mmh yamekuwa hayo tena, lol hii mpya, mmmmhh wapi!, thubutu,"
Nimeweka appointments na wadada miezi nenda rudi, ah wapi, hata wale niliowazoea kama akina King'asti, Heaven on Earth, Smile, Cynthia Chriss hawakamatiki. Preta ndio kabisa!
MMU haina maana, inaweza kukuweka pending kama kusubiria vocha ya mkopo au kufuatilia mkopo NMB! Mbona utajuta, utakaposhtuka na umri wako ndio umeyoyoma kama wa Kapuya!
MMU ina wenyewe, magwiji yaliyobobea, mie nimenyosha mikono juu.
Jamani, nilikuja MMU kwa pepo za msimu naondoka na pepo hizo hizo, maana zikinipita nitaendelea kubaki.
CC: mimi49, christine ibrahim, Sista, sister, Ablessed mdida, charminglady, Madame B, madameA madame X, tinna cute, mkunde Original, Mapi, Asnam, Evelyn Salt, Money Stunna, watu8, Himidini, Lady doctor, mwekundu, Nazjaz, Eiyer, Boflo, Mashaxizo, Mshinga, mzabzab, Bujibuji, KOKUTONA, farkhina
BCC: MMU senior bachelors
Kwa hisani ya wana MMU wote.
ufs: @Mods
Last edited by a moderator: