Jamani, sijasikia lolote wala kuwaona viongozi wetu wakubwa kama B. Mkapa, A. H. Mwinyi,spika, na wengine wengi katika kampeni za kumnadi mgombea urais CCM. kuna mtu anajua lolote mtu amelisikia?
Sababu kubwa ya wao kutofanya hivyo ni kutoombwa na Mh. Kikwete. Kikwete na wenzke wameona maji bado si ya shingo kivile au hata kama wanajua hali ni tete lakini wana hakika ya "kumanuva" matokeo kwa namna wajuavyo wao, hivyo haono sababu ya kuwatembeza wazee hao bali aliwataka wapuumzike. Vile vile hususani Mkapa siyo msafi sana hivyo uwezekano wa kumuua katika kampeni kupitia mikataba mingi ya kifisadi ungekuwa mkubwa na kumpotezea wapiga kura.
Mwisho Kikwete alishaamua kutumia "Strategy" ya kuitumia familia yake akidhani ingekuwa na ufanisi mkubwa lakini mkakati huo haukuzaa mtunda makubwa zaidi ya kukosolewa vikali na wadau ndani na nje ya chama chake mwenyewe.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.