Mlevi huwa hakumbuki alichokinena au alichotenda

clet 8

JF-Expert Member
Mar 14, 2011
1,127
322
Mlevi ni mtu wa ajabu sana! Ana uwezo wa kuona,kusikia na kuzungumza. Ulevi upo katika namna nyingi na madhara makubwa ya ulevi ni kupoteza kumbukumbu kwa urhisi.Ni afadhari ulevi wa pombe kuliko ulevi wa madaraka.

"Viongozi wetu wamelewa" nathubutu kutamka hivyo kwa masikitiko makubwa. Nimekuwa mfuatiliaji wa mambo mengi yanayohusu nchi yetu kwa muda mrefu. Katika haya naamini utakubaliana nami kuwa watawala wetu waeshaleewa! Katika bunge la bajeti lilopita serikali kupitia waziri wa nishati na madini mh.Ngeleja ilisema itapandisha bili za umeme kwa makampuni makubwa jana waziri mkuu kasema umemeutapanda kwa watumiaji wote!

Watawala haohao waliasisi utaratibu wa kujisafisha kwa staili ya magamba, lakinii cha kushangaza ni kuwa haohao wanatakiwa kuvua magamba wanawanyanyua ktkt majukwaa kwa mbwembwe na kuwanadi kwetu kuwa ni wazuri.


Huu ni ulevi na ni hatari katika mstakabali wetu. Je, nani atuokoe ktk hili?
 
Back
Top Bottom