Mkwepa kodi mkubwa huyu hapa

Mkwepa kodi mkubwa huyu hapa

rosemarie

JF-Expert Member
Joined
Mar 22, 2011
Posts
6,887
Reaction score
3,439
IMG_7643.jpg
naona wameona vema kutuletea picha kwa sababu jeshi la polisi limeshindwa kumkamata,,,,,,,

attachment.php
 
Taarifa haijalamilika hio. Anaitwa nani na kosa gani?
 
Itatolewa zawadi ya Mill 20 atakaefanikisha kukamatwa.
 
Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam Kamishna, Suleiman Kova akionyesha picha ya Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya REGIONAL CARGO SERVICES LTD,ABDULKADIR S/O KASSIM ABDI, Miaka 38, Mkazi wa Temeke Mikoroshini ambaye anatuhumiwa kwa kutoa makontena 329 kwenye bandari kavu ya AZAM (AZAM ICD) bila kulipia kodi anayetafutwa na jeshi hilo pia ni mmoja wa wakurugenzi wa kampuni za ?JAS EXPRESS FREIGHT LTD? na ?XL CLEARING AND FOWARDING Co. LTD? ambazo zote zilitumika kutoa makontena hayo. Ameonyesha picha ya mtuhumiwa huyo wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo.
JESHI la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam linawashikilia watuhumiwa 40 ambao wanahojiwa kwa tuhuma za kula njama na kuikosesha serikali mapato. Uchunguzi unafanywa kwa pamoja na maafisa wa Jeshi la Polisi na Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) kwa lengo la kubaini jinsi ambavyo makontena 329 na mengine 2489 yalivyotolewa bandarini kinyume cha taratibu.
Kati ya hao, watuhumiwa 26 ni watumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)na watumishi 03 kutoka Bandari kavu (ICD) YA AZAM wanatuhumiwa kuhusika na upotevu wa makontena 329. Aidha, watuhumiwa 11 ambao ni watumishi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) kwa kuhusika na upotevu wa makontena 2489.
Uchunguzi unaoendelea pia unahusisha kupitia kumbukumbu mbalimbali na kadhia za forodha ili kubaini mtindo uliotumika na kuwabaini wote waliohusika katika mchakato huo. Makontena 329 yaligundulika kukosekana kwenye ICD ya AZAM kuanzia mwezi Julai hadi Novemba 2015, wakati makontena 2489 yaligundulika kutolewa Bandarini kuanzia Mwezi Machi mpaka Septemba, Mwaka 2014 kinyume cha taratibu kwa lengo la kukwepa kodi na ushuru.

Uchunguzi bado unaendelea ili kuwabaini wote wanaohusika na hatimaye majalada ya kesi yatapelekwa kwa mwanasheria wa serikali ili watuhumiwa watakaobainika kuhusika na makosa mbalimbali wafikishwe mahakamani.
 
Taja jina la papa na uweke ushahidi hapa...
Huyu zaidi ya kuweka picha yake kuna ushahidi gani umewekwa? Wengine wakisema huyu ni kidagaa mapapa wapo, ndiyo mnadai ushahidi, si mdai ushahidi kwa Kova kwanza athibitishe kwamba huyu mwenye hii picha ni mkwepa kodi. Nyie ndiyo huwa mkianza kula mnanawa mikono kwa maji bila ya sabuni mkimaliza kula ndiyo mnauliza, sabuni iko wapi!?
 
naona wameona vema kutuletea picha kwa sababu jeshi la polisi limeshindwa kumkamata,,,,,,,

attachment.php

Huyo Msomali analindwa na Ofisa wa TRA anaitwa Gasper martini Mhina yupo TRA Temeke huyo ofisa kabla ya kuhamia huko alikuwa TRA mwenge anamiliki kikundi kikubwa cha wasomali, Wachina na wengineo weusi Watanzania ambao huwasaidia na kumlipa cash anamiliki nyumba nyingi kuliko masamaki, lakini ni mafia hakuna anayejua majina ya mali zake kwani kaandika majina ya Ndugu zake kwenye nyumba zake za Tanga, Dodoma, Arusha na Huko Dsm ana nyumba nyingi sana na huyo Msomali kamficha nyumbani kwake mbezi makabe anaandaa kumtorosha kwa njia ya barabara usiku hadi Zambia au malawi.
 
hii nchi bwana hahahahaha! Nimeamini linapokuja suala la kutengeneza sinema za kipolisi hata Hollywood hawatuwezi!
 
Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam Kamishna, Suleiman Kova akionyesha picha ya Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya REGIONAL CARGO SERVICES LTD,ABDULKADIR S/O KASSIM ABDI, Miaka 38, Mkazi wa Temeke Mikoroshini ambaye anatuhumiwa kwa kutoa makontena 329 kwenye bandari kavu ya AZAM (AZAM ICD) bila kulipia kodi anayetafutwa na jeshi hilo pia ni mmoja wa wakurugenzi wa kampuni za ?JAS EXPRESS FREIGHT LTD? na ?XL CLEARING AND FOWARDING Co. LTD? ambazo zote zilitumika kutoa makontena hayo. Ameonyesha picha ya mtuhumiwa huyo wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo.
JESHI la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam linawashikilia watuhumiwa 40 ambao wanahojiwa kwa tuhuma za kula njama na kuikosesha serikali mapato. Uchunguzi unafanywa kwa pamoja na maafisa wa Jeshi la Polisi na Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) kwa lengo la kubaini jinsi ambavyo makontena 329 na mengine 2489 yalivyotolewa bandarini kinyume cha taratibu.
Kati ya hao, watuhumiwa 26 ni watumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)na watumishi 03 kutoka Bandari kavu (ICD) YA AZAM wanatuhumiwa kuhusika na upotevu wa makontena 329. Aidha, watuhumiwa 11 ambao ni watumishi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) kwa kuhusika na upotevu wa makontena 2489.
Uchunguzi unaoendelea pia unahusisha kupitia kumbukumbu mbalimbali na kadhia za forodha ili kubaini mtindo uliotumika na kuwabaini wote waliohusika katika mchakato huo. Makontena 329 yaligundulika kukosekana kwenye ICD ya AZAM kuanzia mwezi Julai hadi Novemba 2015, wakati makontena 2489 yaligundulika kutolewa Bandarini kuanzia Mwezi Machi mpaka Septemba, Mwaka 2014 kinyume cha taratibu kwa lengo la kukwepa kodi na ushuru.

Uchunguzi bado unaendelea ili kuwabaini wote wanaohusika na hatimaye majalada ya kesi yatapelekwa kwa mwanasheria wa serikali ili watuhumiwa watakaobainika kuhusika na makosa mbalimbali wafikishwe mahakamani.

Yupo kajificha nyumbani kwa Mhina kule mbezi makabe Ndani ndani sana ni vigumu kufika.
 
hizi sanaa tu! huyu jamaa kashapewa mpunga ili aangushiwe msala na wamemsepesha!
 
Kamanda kova Msomali sasa yupo njiani usiku huu anatoroka atapitia ile mipaka bubu ya vijijini ni vigumu kumkamata maana maafisa wengi wa TRA wanamlinda ili asikamatwe akatoa Siri zao.
 
hizi sanaa tu! huyu jamaa kashapewa mpunga ili aangushiwe msala na wamemsepesha!

Hii mbinu ya kuwaokoa wengi msala utabebeshwa kwake wote kisha wengine watapeta.
 
Wasaidieni taarifa ili apatikane

Alikuwa kwa Gasper.M.Mhina afisa TRA wa Temeke anayeishi mbezi makabe, lakini usiku huu anatoroka baada ya kuona Kova kaitoa picha yake Live.
 
Back
Top Bottom