Mkweli ukweli hujamtendea haki Dr. Slaa pamoja na CHADEMA

Mkweli ukweli hujamtendea haki Dr. Slaa pamoja na CHADEMA

Barbaric

Member
Joined
Aug 14, 2011
Posts
34
Reaction score
9
MKWELI UKWELI HUJAMTENDEA HAKI DR. SLAA PAMOJA NA CHADEMA
Ukiisoma Makala ya ndugu MKWELI UKWELI katika gazeti la Raia mwema toleo namba 259 utagundua sio tu kwamba ndugu Mkweli ana chuki binafsi na DK. Slaa na chama anachokiongoza cha CHADEMA bali pia haitakii amani nchi yetu kwa kuto ueleza uma wa watanzania ukweli kuhusu chanzo cha migogoro na vifo vya watanzania vinavyotokea katika mikutano mingi ya nje ya chama cha CHADEMA.
Katika makala hiyo ndugu Mkweli ameonyesha dhahili kwamba makala yake ilikuwa na lengo la kuwachonganisha watanzania na chama cha chadema kwa sababu katika makala hiyo ndugu mkweli ametoa hukumu mbaya moja kwa moja kwa chadema bila kuwa katikati ya pande mbili alizokuwa anazijadili ambazo ni CHADEMA NA SERIKALI, Kwanza kabisa ameanza kwa kukataa kuwa Dk.Slaa hastahili kufananishwa na mfalme Solomoni ,mimi hiyo naiona kama chuki binafsi kwa sababu aliyemfananisha Slaa na Mfalme Solomoni ulikuwa mtazamo wake yeye na si ustaarabu kupinga kwa sababu ule ulikuwa ni mtazamo wa mwandishi mwanakijiji .
Pili katika makala ile ndugu mkweli alieleza tu juujuu kwamba mikutano ya CHADEMA inasababisha vifo kwa watanzania bila kueleza kinaganaga ni jinsi gani CHADEMA ni chanzo cha vifo, napingana na ndugu Mkweli kwa kuangalia matukio machache yafuatayo ambayo ni miongoni mwa mifano ya Mkweli na ambayo mimi naona sio kosa la CHADEMA.
Tukio la Msamvu Morogoro, Katika tukio lile polisi wenyewe walionekania kujichanganya juu ya sababu ya kifo cha Yule kijana, polisi ambao wanavyombo vyote vinavyoweza kuchunguza chanzo cha kifo kile na kutoa majibu ya uhakika walijikanyaga na kuanza kusema kifo kile kilisababishwa na kitu kilichorushwa kutoka upande usiojulikana wakati mashuhuda walioshuhudia tukio lile wanasema ilikuwa ni risasi, hata kama ndugu Mkweli alishindwa kuwaamini mashuhuda labda kwa kuhisi kuwa walikuwa wanaitetea CHADEMA, lakini kwa jinsi polisi wanavyotenda kazi kukandamiza upinzani walishindwa kuchunguza na kugundua kuwa chanzo ni CHADEMA? Lakini tukiachilia mbali kitu kilichopelekea kifo kile na tukirudi tukio zima Mkweli haoni kuwa maandamano yale yalikuwa ni ya amani na hayakustahili nguvu kubwa kiasi kile? Hapo kosa la CHADEMA lipo wapi?
Tukio la Nyololo Iringa,Katika tukio hili vyombo vya habari vilionyesha jinsi polisi walivyokuwa wanamburuza mwandishi wa habari Daud Mwangosi ilhali akiwa na alama zote zinazomtambulisha kama mwandishi wa habari lakini bado walimburuza na hatimaye kupelekea kifo chake mbele ya kamanda wa polisi wa mkoa wa Iringa, sasa hapa kosa la CHADEMA NA DR.Slaa lipo wapi? Na kama sikosei Mwandishi alipokuwa anaandika makala yale jeshi la polisi lilikuwa tayari limemfungulia mashtaka Mtuhumiwa wa mauaji ya Mwangosi, kwa hatua hiyo tu unaweza kutambua kuwa CHADEMA hawahusiki na tukio kifo kile , kwa nini Mkweli amewashutumu CHADEMA kwamba ndio chanzo cha kifo kile?
Sababu nyingine inayonifanya nimuone Ndugu Mkweli kama mwenye chuki binafsi na Dr.Slaa pamoja na CHADEMA ni kitendo cha yeye kutoandika choachote kuhusu ile mikutano ambayo ilipelekea mauaji kwa wafuasi wa CHADEMA mfano lile tukio la Igunga ambalo kuna kijana alipotea katika mazingira ya kutatanisha na hatimaye kukutwa amekufa, Ndugu Mkweli hajazungumzia lolote kuhusu hili utafikiri ni mtanzania aliyekuja juzi na kukuta matukio hayo tu aliyoyasema yeye.
Hitimisho, napenda kumuomba mwandishi ili aeleweke vizuri ni bora ayaeleze matukio kwa kuangalia pande zote kwa kuzikosoa zilipokosea na na kuzisifu zinapofanya vema ili kuzifanya pande zote zijisahihishe na kuimarisha shughuli zao kwa maslahi ya Taifa.
Mimi ni msomaji wa Raia Mwema, Iringa
 
Ndugu yangu wala usishangae haya mambo, waandishi/wachambuzi wa namna hiyo wapo wengi sana, ukweli wanaujua lakini kwa kutaka kuendekeza njaa ndio wanaeneza propaganda za ajabu kabisa.

Hizo makala wakishaziandika kabla ya kuchapishwa mara nyingi wanazileta hapa Lumumba zihaririwe vizuri, maana bila hivyo hakuna mshiko.

Mkuu wala usijali kila mtu anayefuatilia mambo anajua ukweli ni ipi, watawala wanahaha usiku na mchana kupotosha lakini watashindwa tu.
 
Mkuu usiumize kichwa, huyo tayari keshajibiwa kwenye gazeti hilohilo la raiamwema
 
Sauti ya watu ni sauti ya MUNGU.ukiona wanachama wapya wanavyomiminika kujiunga na CHADEMA ujue wameshato hukumu yao tayari.ukweli ni kwamba wauaji ni serikali,Kwahiyo huyo mwandishi anajisumbua bure. MUNGU AMICHAGUA CHADEMA na watu wapo na chadema.
 
MKWELI UKWELI tupa kule, CCM TUPA HUKO,TUACHIENI CHADEMA YETU.
 
Hili gazeti nilliona nilipata kichefuchefu na mada zilizoandikwa ni za kipuuzi zikiwepo za mkandara, zitto na hii.Hili gazeti nililichana na kulitupa.Nilidhani litakuwa hata mbadala wa mwanahalisi kipindi hichi cha majonzi.Dr. Slaa na Mbowe wamekuwa target kwa muda mrefu sana wa hizi kampeni dhaifu na chafu.
 
Kama Katumwa vile!

siku hizi hata usipotumwa, unaweza ukajituma mwisho wa siku unaenda lumumba na kusema hii ni kazi yangu unakaguliwa unaambiwa haya kaungane na wenzako kwenye msitari utawakuta rejao, ritz na ............ watakuelekeza utaratibu
 
Sauti ya watu ni sauti ya MUNGU.ukiona wanachama wapya wanavyomiminika kujiunga na CHADEMA ujue wameshato hukumu yao tayari.ukweli ni kwamba wauaji ni serikali,Kwahiyo huyo mwandishi anajisumbua bure. MUNGU AMICHAGUA CHADEMA na watu wapo na chadema.
+ Freemason=CHADEMAFREEMASON!
 
tusililaumu raia mwema kwani lenyewe linachapisha makala za kila upande, mara nyingi linakuwa katikati, ndo maana limechapisha pia majibu yaliyotolewa na arcado ntagazwa kuhusu makala ile!
 
Back
Top Bottom