Mkuu ZITTO tatizo sio PINDA ni KIKWETE

Jumakidogo

R I P
Jul 16, 2009
1,851
417
Mh ZITTO naona kama PINDA mnataka kumsukumia zigo la dhambi kwa kumuwajibisha kutokana na makosa ya mawaziri wengine. Kwa ni nini tusilie na yule aliyewateua na kuunda baraza lao. Tunajua Pinda naye alishiriki lakini mwenye maamuzi ya mwisho ni rais mwenyewe. Huyu rais kwani hajui ubovu na ubadhirifu wa mawaziri wake?

Kwa nini asiwapige chini wote wanaotuhumiawa kwa uzembe? Nionavyo rais ndiye anayepaswa kupigiwa kura ya kutokuwa na imani naye kwa sababu masanamu aliyoyachonga yeye mwenyewe sasa yanamzidi akili na maarifa ya uhalifu. Hivi timu ikifanya vibaya anawajibishwa kocha aliyepanga timu? Au kapteni (nahodha) wa timu?
 
Zitto alichosema yupo sawa maana kwa mujibu wa katiba ndani ya bunge huwezi kupiga kura ya kumwondoa waziri yeyote ispokuwa inapigwa kura ya kutokuwa na imani na serikari,bungeni waziri mkuu ndiyo anayesimamia shughuli za serikali
 
JK(kichwa cha nazi pale magogoni) ndio anawatia kiburi. Kamng'ang'ania waziri wa afya mpaka leo bado yupo. Hata hao wenye tuhuma siajabu amekwisha waambia hakuna kujiuzuru. Nchi hii matatizo yanaanzia magogoni. Anachokifanya baba watoto huwa wanaiga. JK alivyo mwizi kwani wao hawaoni? ndiyo maana anauchuna wakifanya maovu ili wasije kumuumbua yakwake. Unataka kusema JK hajui kuwa Mkulo kavunja CHC kwa maslahi binafsi? naye ana pasu la mgao. Bandari ya Mtwara kuwapa wa Lebanon kwani JK hajui? mie nadhani tutafute sniper wa kutuondolea huyu mtu.

Kumbuka EL alimuumbua kwenye vikao vya ndani kuwa kila alichokifanya alikuwa anajua..asituchezee.
 
Acha ku DILUTE wewe mchakato umeshaanza na tumebakiza vipoint 6 ngoma inoge. Alipopashika Zitto ndo penyiwe haswaa!!!
 
hili nalo neno tungeanza na huyo aliyewaweka

pengine ndiye anayewatuma ndo maana anakaa kimya

kama hausiki angeshawapiga chini yeye ndiye mwizi wetu
 
ndg zanguni haya yote tumekuwa kukiyaona, alisimama Dr. Slaa kwenye kampeini lakini kuna watanzania ambao vichwa vimejaa maji ya kijani na njano, yakatuangusha na yale majizi ya kura yakatuangusha - tusingefika hapa kama tungechukua maamuzi ya kuyang'oa ma sisiemu!
Tatizo ni la watanzania wote ambao ni mbumbumbu.
 
Zitto alichosema yupo sawa maana kwa mujibu wa katiba ndani ya bunge huwezi kupiga kura ya kumwondoa waziri yeyote ispokuwa inapigwa kura ya kutokuwa na imani na serikari,bungeni waziri mkuu ndiyo anayesimamia shughuli za serikali

Mkuu usemayo ni sawa, lakini mzunguuko wote huo ulikuwa na haja gani wakati ushahidi wa watu kufanya madudu uko wazi? Kwa rais kuwawajibisha wote. Hata waziri mkuu angetaka ilikuwa ni kitendo cha dakika 5 tu. Kwani rais haoni kama suala hili liko wazi na ushahidi upo?
 
Mh ZITTO naona kama PINDA mnataka kumsukumia zigo la dhambi kwa kumuwajibisha kutokana na makosa ya mawaziri wengine. Kwa ni nini tusilie na yule aliyewateua na kuunda baraza lao. Tunajua Pinda naye alishiriki lakini mwenye maamuzi ya mwisho ni rais mwenyewe. Huyu rais kwani hajui ubovu na ubadhirifu wa mawaziri wake?

Kwa nini asiwapige chini wote wanaotuhumiawa kwa uzembe? Nionavyo rais ndiye anayepaswa kupigiwa kura ya kutokuwa na imani naye kwa sababu masanamu aliyoyachonga yeye mwenyewe sasa yanamzidi akili na maarifa ya uhalifu. Hivi timu ikifanya vibaya anawajibishwa kocha aliyepanga timu? Au kapteni (nahodha) wa timu?

Naomba nikufamishe kitu kimoja, hizi ni kanuni pale mambo ya serekali napoenda kombo na moja ya tatu ya wabunge wakikubali kupia kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu kwa sababu yeye yuko pale kwa ajili ya serekali na kumwakilisha rais...na yeye waziri kuu ndo anayeshauri rais na kwa kuwa yeye ndiye anamwakilisha bungeni. akishauri rais akikataa basi alipaswa kuuzulu kwa kuubadhirifu wa mawaziri wake
 
Hapo umesema ukweli. In fact hata Zitto analijua hilo. Lakini hana jinsi ya kumuokoa. Inabidi aondoke kwa manufaa ya taifa
 
Acha ku DILUTE wewe mchakato umeshaanza na tumebakiza vipoint 6 ngoma inoge. Alipopashika Zitto ndo penyiwe haswaa!!!

Mku ukitaka kuua nyoka unapiga mkiani? au kichwani? Kichwa cha nyoka ndicho chenye madhara. Mkia wa nini?
 
Ni kweli Tatizo la msingi ni JK ... "People pleaser", hata ukimweieka Mawaziri wazuri hataweza kuchukua maamuzi sahihi kwa wakti muafaka. Lakini kwa hali ilivyo kwakweli lazima kuchukua hatua kwa ajili ya heshima ya Nchi na wananchi lazima kufanyike jambo.

Hatuwezi kusubiri hadi kumchukulia hatua Jk jambo lenye mshiko kwa sasa si lingine zaidi ya Kumwekea JK rekodi ya kuwa Raisi wa kwanza Kupoteza mawaziri wakuu wawili kupitia Bunge.
 
Naomba nikufamishe kitu kimoja, hizi ni kanuni pale mambo ya serekali napoenda kombo na moja ya tatu ya wabunge wakikubali kupia kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu kwa sababu yeye yuko pale kwa ajili ya serekali na kumwakilisha rais...na yeye waziri kuu ndo anayeshauri rais na kwa kuwa yeye ndiye anamwakilisha bungeni. akishauri rais akikataa basi alipaswa kuuzulu kwa kuubadhirifu wa mawaziri wake

Hiyo najua mkuu. Pamoja kanuni za bunge. Je rais hajui ubovu, wizi na ubadhirifu wa aliowaweka? Ushahidi si upo? Mbona kakaa kimya siku zote? Ndo maana nikasema kura za kutokuwa na imani naye zianzie kwake. Nyoka ni adui wa binadamu, tumpigapo tunaanza na kichwa hatuanzi na mkia wala kiuno.
 
Ni kweli Tatizo la msingi ni JK ... "People pleaser", hata ukimweieka Mawaziri wazuri hataweza kuchukua maamuzi sahihi kwa wakti muafaka. Lakini kwa hali ilivyo kwakweli lazima kuchukua hatua kwa ajili ya heshima ya Nchi na wananchi lazima kufanyike jambo.

Hatuwezi kusubiri hadi kumchukulia hatua Jk jambo lenye mshiko kwa sasa si lingine zaidi ya Kumwekea JK rekodi ya kuwa Raisi wa kwanza Kupoteza mawaziri wakuu wawili kupitia Bunge.

Tukumbuke kuwa, nchi za wenzetu wananchi wakichoka na kuanza kuandamana huanza moja kwa moja na harakati za kumtoa rais ama mkuu wa nchi. Mbovu si yule aliyeshindwa kuwajibika, mbovu ni yule aliyeshindwa kumuwajibisha yule ambaye hakuwajibika.
 
Mh ZITTO naona kama PINDA mnataka kumsukumia zigo la dhambi kwa kumuwajibisha kutokana na makosa ya mawaziri wengine. Kwa ni nini tusilie na yule aliyewateua na kuunda baraza lao. Tunajua Pinda naye alishiriki lakini mwenye maamuzi ya mwisho ni rais mwenyewe. Huyu rais kwani hajui ubovu na ubadhirifu wa mawaziri wake?

Kwa nini asiwapige chini wote wanaotuhumiawa kwa uzembe? Nionavyo rais ndiye anayepaswa kupigiwa kura ya kutokuwa na imani naye kwa sababu masanamu aliyoyachonga yeye mwenyewe sasa yanamzidi akili na maarifa ya uhalifu. Hivi timu ikifanya vibaya anawajibishwa kocha aliyepanga timu? Au kapteni (nahodha) wa timu?

Mtoto wa mkulima kaonyesha effort gani katika kushughulikia ufisadi unaoripotia mwaka nenda mwaka rudi. kama hakubaliani na maamuzi ya rais kwa nini asijiuzuru na kumshitakia kwa wananchi waliompa dhamana ya nchi hii. Yule mama Banda pale Malawi alifanya nini. Kama jitu linakuwa joga lipate matunda ya uoga wake
 
Mh ZITTO naona kama PINDA mnataka kumsukumia zigo la dhambi kwa kumuwajibisha kutokana na makosa ya mawaziri wengine. Kwa ni nini tusilie na yule aliyewateua na kuunda baraza lao. Tunajua Pinda naye alishiriki lakini mwenye maamuzi ya mwisho ni rais mwenyewe. Huyu rais kwani hajui ubovu na ubadhirifu wa mawaziri wake?

Kwa nini asiwapige chini wote wanaotuhumiawa kwa uzembe? Nionavyo rais ndiye anayepaswa kupigiwa kura ya kutokuwa na imani naye kwa sababu masanamu aliyoyachonga yeye mwenyewe sasa yanamzidi akili na maarifa ya uhalifu. Hivi timu ikifanya vibaya anawajibishwa kocha aliyepanga timu? Au kapteni (nahodha) wa timu?

huwezi kutoka kutambaa ukaanza kucheza soka... wacha aanze na kusimama, pinda ndio step one
 
Hiyo najua mkuu. Pamoja kanuni za bunge. Je rais hajui ubovu, wizi na ubadhirifu wa aliowaweka? Ushahidi si upo? Mbona kakaa kimya siku zote? Ndo maana nikasema kura za kutokuwa na imani naye zianzie kwake. Nyoka ni adui wa binadamu, tumpigapo tunaanza na kichwa hatuanzi na mkia wala kiuno.

Tatizo mmesahau kabisa kwamba hii siriKALI ni ya kishkaji zaidi....lazima kuoneana soo, kamwe kuwajibishana hakuwezi kuwepo.....mlitegemea nini?! Keep it up Zito.
 
Back
Top Bottom