Mkuu wa Wilaya ya Busega Mkoani Simiyu aagiza wanaomiliki fisi wawachunge wasidhuru watu

Hili bara kweli limelaniwa wanashindwa kufuga Twiga au wanyama wenye thamani wanafuga fisi
.... yaani wewe unadharau FISI?
kwa kisukuma fisi ana majina mengi sana kwa umaarufu wake! (Embiti ele na mina minge'no mjisukuma!)πŸ˜…πŸ˜… ... halafu mazishi yake sasaaa! ... yaani tunamgawana Kijiji kizima, mpaka na mchanga tu wa sehemu aliyofia!
DON'T JUDGE BOOKS BY THEIR COVERS!
 
Wanaomiliki fisi? Utadhani anazungumzia wanaomiliki assets kama maviete, ndege binafsi nkπŸ˜€

Halafu sijui hao fisi serikali inawaweka kwenye kundi gani?

Maana sidhani kama unaruhusiwa kumiliki Simba, Tembo, chui na Twiga bila kibali maalum cha serikali mfano zoo ya Wanyama nk
... In Sukumaland hyenas are domestic animals! ... and those roaming the Serengeti are just the FERAL VERSION!
welcome HOME NG'WANANGWA!
1711253531762.png
 
Mkuu wa Wilaya ya Busega Mkoani Simiyu, Faiza Salim amemuagiza Mwenyekiti wa Kijiji cha Nyamikoma, Kata ya Kabita Wilayani humo kuwaita Waganga wa tiba asilia Kijijini hapo ili kuwaomba Wawachunge na kuwadhibiti fisi ili wasidhuru Watu kwakuwa fisi hao inaaminika wanamilikiwa na baadhi ya Watu kijijini hapo ambao huwatumia kwenye masuala ya kishirikina.

DC ametoa agizo hilo wakati akiwa kwenye kikao cha kusikiliza kero za Wananchi Kijijini hapo ambapo Mwananchi Emmanuel Augustine amelalamikia uwepo wa fisi wanaosumbua Watu β€œKero yangu ni wanyama wanatusumbua sana, viboko wanatusumbua fisi nao wanaunguruma, mpaka saa moja fisi wapo ndani , kero ya pili ningebanwa haja sidhani kama ningeenda kujisaidia wapi soko hili kubwa lakini hatuna choo, Mh (DC) hata wewe sasa hivi ukibanwa utaenda wapi?, liangalie soko lipate choo, Diwani unaongea mambo mengi hautukumbuki”

Akijibu hoja hizo DC Faiza amesema β€œFisi wanamilikiwa na Watu, Mwenyekiti itisha Waganga wako wa tiba asilia wazungumze kuhusu fisi wawalinde fisi wao, lindeni fisi wenu wasidhuru Watu, mkiwaachia hivihivi mnamtisha Mzee Emmanuel anashindwa kufanya kazi nyingine kwasababu ya fisi”

β€œMwenyekiti itisha Waganga wako wa tiba asili waambie wachunge fisi wao, Mimi sitaki kuingia mgogoro na wao kuanza kuwaua fisi wasije wakanifuata nyumbani kwangu, maana nikianza kuwaua hapa kuna DC alikuwa anawaua wanamfuata mpaka kwake Mimi sitaki malizana nao ukishindwa niite nije kuwaomba jaman lindeni zana zenu”
Ka Mheshimiwa DC kaneogopa kufanyiwa yaliyomkuta Anna Abdallah miaka hiyo! Ilikuwa ni huko huko Busega. Ila poti nao wanazingua yaani mpaka karne hii wanaendekeza ushirikina tu mpaka huku mjini tunaogopa kujitambulisha kwamba tumetoka huko!
 
Huko kuna ma master balaa, kuna gari iligonga fisi, asubuhi kijiji kizima kikatoka mbio kwenda kukata mabaki ya fisi aliyegongwa, waliokosa mabaki wakawa wanazoa damu na mchanga almuradi wasikose.

Nassa ndio baba lao, imetoa akina Chenge, Mkuu wa Majeshi Mabeho, majaji na watu wakubwa, lakini hapaendelei, watu wanakimbilia lamadi wanaogopa uchawi
Ni kweli mkuu, Nassa tunatiwa aibu na wajinga wachache. Sungusungu ilitaka kutusaidia kabla haijaingiliwa na wanasiasa. Pale makao makuu ya wilaya pa zamani sana lakini hapasongi shauri ya uchawi!
 
pumbavu kuendekeza ma uchawi tu. ilipaswa maeneo kama hayo ningekua rais ni kuua wafe wote by any means tuanze upya.
 
Nimeishi maeneo tofauti tofauti hapa Tanzania husani pwani hasa uzaramoni jambo la uchawi ni kawaida kabisa Na Kuna kipindi inafika watu wanakuja na coster wamejazana kuja kufanya ushirikina na uchawi hadharani Tena mchana kweupeeee.

Bila kupindisha nimewahi ishi kisarawe Kijiji kimoja kinaitwa Gwata mzaramo kuzuia mvua Ili wacheze ngoma zao au kigodolo ni jambo la kawaida sana.
Kuoga uchi njia panda na watu wakiona Tena mchna kweupe bila aibu ni kitu kilichozoeleka sana sambamba na kupasua Nazi maswala ya chuma ulete nk vitu visivyo vya kushangaa.

Nikaishi maeneo ya manyara pale babati na kateshi vijijin ndani ndani huko kama Dirima kama sijakosea, Nangwa,Endasaki nk maswala ya ushirikina yapo wazi wazi pale dodoma Hali Ile Ile.


Moja Kwa Moja kwenye mada kama Uzi unavyosema kiboko ya yte ni huko Kanda ziwa yaani Kwa wasukuma hapa Sasa ndo nasogeza kiti na kukaa kabisa.

Katika harakati zangu za hapa na pale Ninafika Kanda ya ziwa maeneo ya kahama, geita,Nyang'hwale, Sengerema naanza kukutana vioja mbalimbali vya kishirikina na uchawi Ile siku nafika tu Kwa ajiri ya kukusanya mpunga Kwa wakulima majira ya saa12 jioni tunasikia yowe tukiwa na wenyeji wa Eneo Hilo.Moja Kwa Moja tunaenda Hadi eneo la tukio (sitakisema Kijiji hapa) tunafika eneo la tukio tunakuta mtoto kaliwa na fisi.
Kilicho tushangaza sio kile kitendo Cha kuliwa na fisi Bali vile yule mtoto alivyo vuliwa zile nguo na zikawekwa pembeni then fisi akamla nguo zikiwa hazina hata tone la damu hata Moja! Jiulize fisi anaweza via nguo ya mtoto bukta na shati?
Tulishangaa sana

Basi haikuishia hapo wakaja wawindaji kutoka vijiji fln wale wawindaji nao sio wa mchezo ni wataalam sio Hivi hivi wanazaidi ya mbwa 100+
Siku ya msako wa kuwa Saka wale fisi ikafika (ikumbkwe Watoto waliliwa sana na fisi Hadi serkali ya wilaya ikaita game waje wawasaidie Cha kushangaza hao askari game hawakuweza kuua hata fisi mmoja! )

Jamaa walikuja wakaingia mlimani na mbwa wao Cha ajabu fisi anatoka nduki Hadi kwenye kaya/ familia za watu na wanapotelea ndani ya nyumba Hadi watengeneze dawa ndo fisi anaonekana akiwa ndani ya nyumba
Vioja vya kustaajabisha baadhi ya fisi walikuwa wakiuliwa walikutwa na hirizi,bangili, na rozali za ndg zetu wa Rc!!
Tukio lililo muacha Kila mtu mdomo wazi bibi wa Eneo hilo kwenda Kwa mtendaji wa Kijiji kushitaki kuwa fisi wake wamemuua je nani atakuwa ana mletea mahitaji?
Wengine walikuwa Tyr wamebeba baadhi ya viungo vya fisi ilibidi wavirudishe haraka sana
emoji23.png
emoji23.png

Nimatukio ya kuona Kwa macho yangu haya sio ya kusimuliwa


Nafahamiana na mzee mmoja Kwa ukaribu sana kutoka hapo Kijijin ndo ananiambia mawili matatu.... Tumuite "mayala (sio jina lake)"
Anasema huku Kila familia Ina mtaalamu wake (Mganga wa kienyeji)walau mmoja hadi 3 bila hivo mambo hayaendi.ananimbia matukio ya nyuma kidgo kuwa kulikuwa na majitu ya ajabu sana pale kwenye miembe ya ( ) Kwa kisukuma yanaitwa makabheba kiswahili tuyaite majitu ya kutisha au mizumu inayoonekana marefu sana.
Mzeee anasema ilikuwa ikifika sa3 Hadi sa4 usiku huwez pita maeneo hayo na pengine unaweza ukatembea Hadi asbh Kuna kucha bila kufika uendako japo wewe utaona umekaribia!!!
Muda mwingine unaweza kusikia kelele za ngoma fifijo na nderemo (lupundu Kwa kisukuma) usiku wa manane.
Anasema "Nakumbka siku Moja natoka kunywa pombe zangu naambia pita vizuri usitukanyagie chakula chetu "
Mzee alinambia mambo mengi sana huku akinisihi sana ishi vzr na watu wa huku ni wapole na wakarimu sana hawapendi kesi na ugovi hata siku Moja. Anasema msukuma unaweza ukamdhurumu haki yake nae akakuambia hakuna tatizo maguzu masese nawewe ukajua hapa umepitisha lkn kamwe tatizo halijaisha ndo limeanza mwanzo atatumia gharama yoyoye kutafta dawa Ili akumalize kbisa.
Mzee alinambia mengi sana.

Break ya mwisho ni pale nilipo enda kupanga kwa mzee wa kanisa fln la kilokole.
Mzee alikuwa smart sana na maswala ya kikanisa na kiroho wagonjwa walikuwa wanaletwa kwakwe anawaombea vzr kabisa Cha ajabu nikuwa alikuwa ana leta waganga wa kienyeji wa Kila aina pale kwake vifaranga vya kuku vilikuwa vinachinjwa sana nikaona hapa hapanistahili nikaondoka....nakumbka siku Moja nikiwa nae tuna badilishana mawazo nikachombeza kidgo kuwa kwann wewe ni kiogozi wa kanisa na unaaminika vile lkn Bado unaenda na upande wa pili jamaa alinijibu vizuri sana Kwa kusema hata Mungu anasaidiwa pale unapoona unaomba lkn hupati majibu kwakwe hivo ktupa akri ya kuchagua lipi jema lipi baya kama umeenda Kwa mganga Kwa Nia ovu ni juu Yako.
Hapo Sasa nikarudisha kumbukumbu Kwa mzee alie niambia kuwa huku Kila familia Ina mtalaamu wakee (mganga) nikasema kama Hali ndo hii Hadi Kwa mtumishi je Kwa wengine ipoje. Nikatoka pale.
Kwa hakika hayo ni kwauchache tu niliyoona Kanda ya ziwa na sehem nilizo zitaja.

Nikiri tu Kwa maoni yangu.sisi Waafrica hizi dini hazikuwa zetu Bali zilikuwa za wenzetu imagine kule pwani karibia miji yote ilikuwa ni ya waislamu Cha ajabu ushirikina ulikuwa Nje Nje maana unaweza hesabu hata nyumba 13 na unakuta familia ya mkristo walau mmoja au familia2 Kwa mbali mbali sana sijajua Kwa Sasa.
Ukija huku Kanda ya ziwa na hata manyara walio wengi ni wakristu lkn mambo ni Yale Yale.Ebu tuchagueni Moja either tuendelee na Imani zetu za mizimu au tuachane nazo basi!! Tusilimu au tuokoke.

Mwisho.


Nimeamua Uzi niuweke sawa baada ya watu kusakama kuwa nimewakosea watu wa Kanda ya ziwa Kwa maana niliongelea ni wasukuma tu.
Ikubukwe kuwa Kanda ya ziwa pamoja nakuwa na makabila mengi sana lkn kabila la wasukuma ndo kubwa kuliko makabila yte na pengine ndo kabila no 1 Kwa Tanzania Kwa ukubwa likiwa na jumla ya mikoa kama6 Kwa Sasa!
Hivo nimejikita sana Kwa wasukuma maana ndo kabila kubwa na vioja vingi nimeviona kwao na hakuna kupinga ndo ukweli wenyewe.. nilihitaji sana kujua gamboshi sikupata muda mzuri wa kufatilia Kwa kina Nini hasa pale gamboshi.

Kwa kifupi tu nimefika ukere kule kisiwani Kwa wakerewe nao wapi vizuri sijaona ila niliambiwa kuwa ukikosana na mzee au bibi wa kikerewe mambo ni halali Yako nikwamba yaani usije ukaona maji yoyote yametwama ukayakanyanga unaliwa na maji msemaji alienda mbali zaidi Kwa kusema hata kama kwenye kikombe unakunywa maji mamba anatokea anasepa nawewe!
emoji23.png
emoji23.png
Sina uhakika japo wengi walithibitisha kuwa ni kweli ila Kwa Sasa watu wameachana na hayo mambo!
Fika Kwa wajita huko bunda ndani ndani Kwa wakurya mambo ya uchawi yako Nje Nje tu sema sikukaa sana lkn mambo kama hayo yapo ya watu kufunga mamba ni jambo la kawaida sana kama Kuna mwenyeji wa maeneo niliyo yataja na nimesingizia aje Athibitishe kuwa Mimi PharaohMtakatifu nimeongopa aje hapa.
Huko chato sehemu Moja inaitwa mganza nilikutana na mzee mmoja wa kabila la mlongo kama sikosei aseee nondo alizo nipa sio powa.

Hapa siwezi kuandika vyote lkn ukweli ndo huo ukienda Kwa watu jaribu kuishi nao vzr upate mawili matatu. Utaishi vizuri mno kama mwenyeji.Ova
Ukifa mke wako namuoa mimi!
 
I like her sense of Homour.... On Serious Note hao walio-design hilo Soko hawakuweka Vyoo ? Na hii dunia ya Viumbe wote sisi Binadamu tunaongezeka na kuigia kwenye hayo Makazi ya Fisi tunategemea wanyameze ili wasitusumbue....
Wakikuwekea choo hutoingia polini kujisaidia, hao Fisi watapata wapi Lishe.
 
Mkuu wa Wilaya ya Busega Mkoani Simiyu, Faiza Salim amemuagiza Mwenyekiti wa Kijiji cha Nyamikoma, Kata ya Kabita Wilayani humo kuwaita Waganga wa tiba asilia Kijijini hapo ili kuwaomba Wawachunge na kuwadhibiti fisi ili wasidhuru Watu kwakuwa fisi hao inaaminika wanamilikiwa na baadhi ya Watu kijijini hapo ambao huwatumia kwenye masuala ya kishirikina.

DC ametoa agizo hilo wakati akiwa kwenye kikao cha kusikiliza kero za Wananchi Kijijini hapo ambapo Mwananchi Emmanuel Augustine amelalamikia uwepo wa fisi wanaosumbua Watu β€œKero yangu ni wanyama wanatusumbua sana, viboko wanatusumbua fisi nao wanaunguruma, mpaka saa moja fisi wapo ndani , kero ya pili ningebanwa haja sidhani kama ningeenda kujisaidia wapi soko hili kubwa lakini hatuna choo, Mh (DC) hata wewe sasa hivi ukibanwa utaenda wapi?, liangalie soko lipate choo, Diwani unaongea mambo mengi hautukumbuki”

Akijibu hoja hizo DC Faiza amesema β€œFisi wanamilikiwa na Watu, Mwenyekiti itisha Waganga wako wa tiba asilia wazungumze kuhusu fisi wawalinde fisi wao, lindeni fisi wenu wasidhuru Watu, mkiwaachia hivihivi mnamtisha Mzee Emmanuel anashindwa kufanya kazi nyingine kwasababu ya fisi”

β€œMwenyekiti itisha Waganga wako wa tiba asili waambie wachunge fisi wao, Mimi sitaki kuingia mgogoro na wao kuanza kuwaua fisi wasije wakanifuata nyumbani kwangu, maana nikianza kuwaua hapa kuna DC alikuwa anawaua wanamfuata mpaka kwake Mimi sitaki malizana nao ukishindwa niite nije kuwaomba jaman lindeni zana zenu”
Dah wasukuma na ushirikina ni kama wali na maharage, Kati ya wasukuma 10, tisa wanachale
 
Tushike lipi sasa.
Kigoma serikali imepiga marufuku rambaramba kigezo hakuna ushirikina huko nako dc anaukiri na kuukubali ushirikina
 
Ukishangaa ya Mussa utaona ya Firauni.
Kijiji cha Kìsaki mkoani Morogoro kuna mwananchi amekutwa na Njiwa wa porini (Tetere) ameshtakiwa kwa kosa la uhujumu uchumi. (Kukutwa na kiumbe pori bila kibali)
Shinyanga raia wanamiliki Fisi, tena wanasababisha madhara kwa raia, lakini cha kushangaza serikali inatoa kauli za kubembeleza.
Waziri wa Maliasili na Utalii atoe tamko kuhusu uhalali wa kumiliki Fisi ili wengine wenye uhitaji nao wawamiliki.
 
Back
Top Bottom