Msafara wa Mamba na kenge huwa hawakosekani na ukiangalia vizuri utawaona mpaka mijusi na magong'ole..........mpuuze tu huyo kama wapuuzi wengine.Hujamaliza, juu kwa juu. Nimekusihi uombe msamaha kwa kumwita Mwita muongo. Baada ya hapo ndipo mtakuwa pamoja.
Mkuu wa Wilaya ya Serengeti bw. Edward Ole Lenga akiwa ameambatana na watumishi kadhaa wa Wilaya hiyo wamekamatwa hivi karibuni wakiendesha hujuma ndani ya hifadhi ya Serengeti, eneo linalofahamika kwa jina la Goga.
Katika hujuma hiyo, DC ole Lenga alikuwa ameambatana na mkuu wa polisi Wilaya(OCD), Afisa Usalama wa Wilaya (DSO) pamoja na watumishi wengine wa vyeo vya chini.
Watu hao walikamatwa baada ya kuwekewa mtego na mkuu wa hifadhi ya Serengeti kufuatia taarifa za siri alizopenyezewa na wananchi.
Imedaiwa DC huyo kwa kushirikiana na wakuu wa vyombo vya dola wilayani humo OCD na DSO wamekuwa wakishirikiana na askari wa wanyamapori kuingia ndani ya hifadhi na kufanya ujangili pamoja na uchimbaji wa madini kinyume na sheria.
Kinachowasikitisha wananchi wa wilaya hiyo ni kitendo cha wakubwa hawa; DC, OCD na DSO kuachiwa huru huku watumishi wengine wakiendelea kusota ndani.
MY TAKE:
Vitendo hivi vya viongozi wakubwa katika wilaya kufanya uhalifu ndani ya wilaya waliyokabidhiwa kulinda na kuimarisha usalama ni cha kufedhehesha sana na kama tungekuwa ni nchi inayojali utawala bora, hawa watu walitakiwa kuwa wamejiudhuru nyadhifa zao na sasa wangekuwa wamefikishwa mbele ya vyombo vya sheria kujibu tuhuma zao.
Lakini cha kusikitisha ni kwamba DC, OCD na DSO wako nje wakiendelea na majukumu yao huku watumishi wengine wa kada za chini walioshirikiana nao wakiwa tayari wamekamatwa na kufunguliwa mashitaka mahakamani.
Tunaomba uthibitisho wa madai yako.
gazeti la habari leo la jumanne tarehe 27/3/12 ukurasa wa mbele.
Ocd amevuliwa wadhifa wake na kurudisha ofisi ya kamanda wa mkoa kwa mahojiano zaidi na hatua za kijeshi. Wananchi waliokuwa wameambatana nao wamekamatwa kwa uchunguzi.
Source: tbc taifa.
Mytake: Mkuu wa wilaya yupo juu ya sheria? Mbona hawajasema hatua alizochukuliwa?
Tunaomba uthibitisho wa madai yako.
Kakojowe ukalale kesho shule , huna hoja ya kuchangia,......by the way ni busara ukawaacha wanaume kamili wachangie hoja hii.Hilo gazeti sio gazeti la magamba kweli?
Wacha wachukue tu madini na wanyama wao, nacho shauri waachiwe huru kwani wengi wameiba sana mali za umma wapo huru, sasa hao washikwe wamekosa nini? Wacha tuendelee na siasa.