Mkuu wa wilaya Kilosa utambue hakuna wilaya ngumu Tanzania kama Kilosa. Unayoyafanya kijiji cha Mbigiri yatakugharimu

nguruka wa kig0ma

JF-Expert Member
Jan 16, 2020
2,946
2,929
Kwa upendo heshima na taadhima nimeona nichukue nafasi hii kukueleza kinagaubaga kuwa wilaya ya Kilosa ni ngumu kiutawala kuliko wilaya zote Tanzania.

Wilaya imejaa wapumbavu na pesa za wapumbavu( upumbavu ni sifa siyo tusi)

Viongozi wanaokwenda Kilosa wanakutana na wapumbavu wakiwana pesa za wapumbavu, zinawapumbaza viongozi.

Wilaya inasitawisha mifugo na mimea hicho ndicho chanzo cha ugumu wa hiyo wilaya.

Watu unaotakiwa kuwa na tahadhari nao ni jamii ya wafugaji wa kimasai, wana pesa za kipumbavu, zitakupumbaza ghafla

Afisa tarafa ndugu Nchimbi wa tarafa ya Magole/Dumila huyu amenogewa na pesa za kipumbavu yupo tayari kumlaghai kiongozi yeyote wa wilaya ili nae apumbazike na pesa za kipumbavu

Ukitaka ushahidi wa maneno yangu waulize wafuatao

1. Ole Sanare aliyekuwa mkuu wa mkoa Morogoro
2. Adam Mgoi, aliyekuwa mkuu wa wilaya aliyekutangulia.

Hawa walipumbazwa na pesa na ardhi ya wakulima, kuwadi akiwa kijana Nchimbi.

Ulipofika tu Kilosa na kuanza kazi watu wa Kilosa waona umeanza vizuri, lakini unayofanya sasa watu hawakutofautishi na mtangulizi wako.

Kupanda mipaka ya vijiji vya Mbigiri, Kitete, Mfulu nk ni agizo la Serikali, lakini kunyang'anya mashamba ya watu kwa madai eti hawakai Mbigiri hapo unavunja katiba ya nchi maana inatamka kuwa mtu (Mtanzania) anaweza kwenda popote ndani ya Jamhuri ya Tanzania na kufanya shughuri zake bila kuvunja sheria.
MASWALI

Wewe umetamka mkutanoni kuwa wanaolima Mbigiri siyo wakaaji wa Mbigiri, sheria hiyo umeitoa wapi ya watu wa sehemu moja wasiende Fanya shughuri zao sehemu nyingine?

2. Je, hao wamasai wanaishi Kilosa na kufanya ufugaji ni wenyeji wa hapo?

3. Wafuatao wana mashamba wilaya za Mvomero na Kilosa.
1. JK Kikwete - wilaya ya Mvomero
2. Ally Mwinyi - Mvomero
3. Lowassa - Kilosa
4. Gharib Bilal - Mvomero nk

Hawa ni wakaaji wa wilaya hizi?

Unataka kupokonya mashamba ya watu ili uwagawie wanakijiji.
Umeshajiuliza hao wakulima na wanakijiji ni nani aliyetangulia kufika hapo?

Hao unaowaita wakaaji walikuwa wanalima wapi miaka yote?( hao mashamba yao wameyauza)
Umeshajiuliza hao unaotaka kuwapora hayo mashamba wamekuwa nayo kwa miaka mingapi?

Umeshajiuliza, ni nani waliosafisha hayo mashamba?

Wakati hao unaowaita siyo wakazi, wanasafisha hayo mashamba hayo wakazi walikuwa wapi kwa nini hawakuchukua hatua stahili?

JE, NA WEWE UMESHAPUMBAZWA NA WATU WAPUMBAVU NA PESA ZA KIPUMBAVU?

Kibaya zaidi kama alivyokuwa anafanya mgoi kutumia ubabe hata kwenye mikutano hataki kusikia maoni ya watu ndimo unamopita.

Kama umepumbazwa ninakwambia itakugharimu.

TAMBUA WEWE SIYO MTU WA MWISHO KWENYE MAAMUZI KTK NGAZI YA KIUTAWALA.

NAKUSHAURI PANDA MIPAKA YA VIJIJI LAKINI KWENYE MASHAMBA YA WATU USIGUSE.
 
Morogoro haijawah kimuacha kiongoz wa wilaya au mkoa salama

Wakumbuke Hawa

Bakari Msulwa

Rajav Rutengwe

Ole Sanare

Huyo mkuu wa wilaya hana muda mrefu atachinjwa

Kazi ndogo tu kumtoa huyo anzishen fujo za wakulima na wafugaji mama hachukui round anamtoa huyo

Na huyo Nchimbi namsikia kila Mara humu huyo mrudishen kwao Songea akiwa kilema msimchekeee
 
Mkuu mbona unaandika mambo ambayo hayaeleweki, japo ujumbe wako unaonekana ulikuwa mzuri? Mara upumbavu sio tusi ni "sofa" nk..
 
Ndugu andiko lako hata kama lina ukweli basi limeambatana na chuki.

Sheria ni msumeno kwa nini useme mipaka itambuliwe lakini kwenye mashamba asiguse? Hapo ndipo penye chuki.
Kumbuka hawa ma DC wanafanya kazi chini ya timu za wataalamu tena waliobobea katika utatuzi wa migogoro ya Ardhi.
Muhimu Sheria inazingatiwa?
 
Mkuu japo kidogo kiuwasilishaji kuna makosa madogo lakini unachosema ni kweli tupu kabisa kabisa na ikumbukwe sehemu yeyote yenye shida ya wakulima na wafugaji asilimi a75 wafugaji wanakua na shida wana msemo wao uza ng'ombe/honga ng'ombe shinda kesi sasa ndugu yangu mkulima mpaka mahindi yakomae ndio akapapatue inawezekana? Kwa mustakabali huo basi imepelekea wafugaji kupendelewa sna kama alivyoita mtoa uzi kwa pesa zao za " kipumbavu"
 
Muongo wewe na hicho Techno chako. Muondoe Lowassa kwenye hiyo orodha. Hajawahi kuwa na ardhi Kilosa na hamiliki hata nukta moja ya ardhi.

Pia wewe unaonekana kama dalali wa ardhi na mbaguzi dhidi ya jamii za kitanzania. Hakuna mtu mwenye fedha za kijinga fedha zote watu wamejaaliwa na mwenyezi Mungu.

Tunakushauri mfunga mkanda chapa kazi. Huu ujinga wako wa kukaa Dumila kunywa na wanawake utakugharimu
Kwa upendo heshima na taadhima nimeona nichukue nafasi hii kukueleza kinagaubaga kuwa wilaya ya kilosa ni ngumu kiutawala kuliko wilaya zote Tanzania...
 
Mkuu japo kidogo kiuwasilishaji kuna makosa madogo lakini unachosema ni kweli tupu kabisa kabisa na ikumbukwe sehemu yeyote yenye shida ya wakulima na wafugaji asilimi a75 wafugaji wanakua na shida wana msemo wao uza ng'ombe/honga ng'ombe shinda kesi sasa ndugu yangu mkulima mpaka mahindi yakomae ndio akapapatue inawezekana? Kwa mustakabali huo basi imepelekea wafugaji kupendelewa sna kama alivyoita mtoa uzi kwa pesa zao za " kipumbavu"
Sheria ni msumeno na kama ushahidi upo Sheria ichukue mkondo wake kuliko kueneza chuki ya kuanzisha vurugu. Tuache wagogo wanasema "Hear Say"
 
Aliyosema mwandishi wa mada hii ni kweli. Lowasa anayo mifugo mingi sana tena sana pale ranchi ya Mkata, sisi wazaliwa wa hapo tunalijua hilo.
 
Muongo wewe na hicho Techno chako. Muondoe Lowassa kwenye hiyo orodha. Hajawahi kuwa na ardhi Kilosa na hamiliki hata nukta moja ya ardhi.

Pia wewe unaonekana kama dalali wa ardhi na mbaguzi dhidi ya jamii za kitanzania. Hakuna mtu mwenye fedha za kijinga fedha zote watu wamejaaliwa na mwenyezi Mungu.

Tunakushauri mfunga mkanda chapa kazi. Huu ujinga wako wa kukaa Dumila kunywa na wanawake utaku
Kwa upendo heshima na taadhima nimeona nichukue nafasi hii kukueleza kinagaubaga kuwa wilaya ya kilosa ni ngumu kiutawala kuliko wilaya zote Tanzania.

Wilaya imejaa wapumbavu na pesa za wapumbavu( upumbavu ni sofa siyo tusi)
Viongozi wanaokwenda kilosa wanakutana na wapumbavu wakiwana pesa za wapumbavu,zinawapumbaza viongozi.

Wilaya inasitawisha mifugo na mimea hicho ndicho chanzo cha ugumu wa hiyo wilaya.
Watu unaotakiwa kuna na tahadhari nao ni jamii ya wafugaji wa kimasai,wanapesa za kipumbavu,zitakupumbaza ghafla

Afisa tarafa ndugu nchimbi wa tarafa ya magole/dumila huyu amenogewa na pesa za kipumbavu yupo tayari kumlaghai kiongozi yeyote wa wilaya ili nae apumbazike na pesa za kipumbavu

Ukitaka ushahidi wa maneno yangu waulize wafuatao
1.Ole sanare aliyekuwa mkuu wa mkoa morogoro
2. Adam mgoi,aliyekuwa mkuu wa wilaya aliuekutangulia.

Hawa walipumbazwa na pesa na ardhi ya wakulima,kuwadi akiwa kijana Nchimbi.
Ulipofika tu kilosa na kuanza kazi watu wa kilosa waona umeanza vizuri,lakini unayofanya sasa watu hawakutofautishi na mtangulizi wako.

Kupanda mipaka ya vijiji vya mbigiri,kitete,mfulu nk ni agizo LA serikali,lakini kunyang'anya mashamba ya watu kwa madai eti hawakai mbigiri hapo unavunja katiba ya nchi maana inatamka kuwa mtu (mtanzania) anaweza kwenda popote ndani ya jamhuri ya Tanzania na kufanya shughuri zake bila kuvunja sheria.
MASWALI

Wewe umetamka mkutanoni kuwa wanaolima mbigiri siyo wakaaji wa mbigiri,sheria hiyo umeitoa wapi ya watu wa sehemu moja wasiende Fanya shughuri zao sehemu nyingine?

2. Je hao wamasai wanaishi kilosa na kufanya ufugaji ni wenyeji wa hapo?
3. Wafuatao wanamashamba wilaya za mvomero na kilosa.
1. Jk kikwete,wilaya ya mvomero
2. Ally Mwinyi, mvomero
3. Lowasa. Kilosa
4. Gharib bilal. Mvomero nk
Hawa ni wakaaji wa wilaya hizi?

Unataka kupokonya mashamba ya watu ili uwagawie wanakijiji.
Umeshajiuliza hao wakulima na wanakijiji ni nani aliyetangulia kufika hapo?

Hao unaowaita wakaaji walikuwa wanalima wapi miaka yote?( hao mashamba yao wameyauza)
Umeshajiuliza hao unaotaka kuwapoka hayo mashamba wamekuwa nayo kwa miaka mingapi?

Umeshajiuliza,ni nani waliosafisha hayo mashamba?
Wakati hao unaowaita siyo wakazi, wanasafisha hayo mashamba hayo wakazi walikuwa wapi kwa nini hawakuchukua hatua stahili?

JE NA WEWE UMESHAPUMBAZWA NA WATU WAPUMBAVU NA PESA ZA KIPUMBAVU?

Kibaya zaidi kama alivyokuwa anafanya mgoi kutumia ubabe hata kwenye mikutano hataki kusikia maoni ya watu ndimo unamopita.

Kama umepumbazwa ninakwambia itakugharimu.
TAMBUA WEWE SIYO MTU WA MWISHO KWENYE MAAMUZI KTK NGAZI YA KIUTAWALA.

NAKUSHAURI PANDA MIPAKA YA VIJIJI LAKINI KWENYE MASHAMBA YA WATU USIGUSE.








Sent from my TECNO CA7 using JamiiForums mobile app

Mkuu japo kidogo kiuwasilishaji kuna makosa madogo lakini unachosema ni kweli tupu kabisa kabisa na ikumbukwe sehemu yeyote yenye shida ya wakulima na wafugaji asilimi a75 wafugaji wanakua na shida wana msemo wao uza ng'ombe/honga ng'ombe shinda kesi sasa ndugu yangu mkulima mpaka mahindi yakomae ndio akapapatue inawezekana? Kwa mustakabali huo basi imepelekea wafugaji kupendelewa sna kama alivyoita mtoa uzi kwa pesa zao za " kipumbavu"
Ni mzawa na mkaazi wa Kilosa kwa zaidi ya miaka 30. Kilosa ni Bonde la Sodoma na Gomora wamejaa wenye tamaa kama Lutu. Wako wanaotamani kurudi kwenye maovu kama mke wa Lutu.

Viongozi wengi wastaafu, walioko madarakani wana maeneo mengi ambayo hayaendelezwa. Wengine wamekodisha kwa wakulima wadogo. Wengine wanamiliki bila kufanyia kitu chochote.

Wafugaji waliopo Kilosa wameuza mifugo yao wamenunua maeneo makubwa wanafuga kisasa na ufugaji wao una tija. Ni wachangiaji wazuri wa maendeleo, ni wachangiaji wazuri wa CCM, ni wachangiaji wazuri Mwenge wa Uhuru. Wafugaji wakizingulia wanatafuta haki mahakani.

Wafugaji na wakulima wa kilosa wa siku nyingi hawana ungomvi. Ugomvi unasababishwa na viongozi wanaofanya siasa za maji taka.

Wakulima na wafugaji wanakopeshana fedha, wanaona, waombana chakula. Wafugaji wanachukuwa mchele na mahindi kwa wakulima. Wakulima wanachukuwa maziwa na nyama kwa wafugaji. Mara nyingi kwenye sherehe za wafugaji wapishi hodari ni wakulima. Wakulima wanakopa ada za watoto wa shule kwa wafugaji. Wakulima wanalipa mikopo hiyo bila riba.

Shida iliyopo ni watu baki, wahamiaji leo hii Msowero imejaa Warundi wanaojifanya wanaojitambulisha kama waha. Pingine hao wanamadhara kuliko wakulima na wafugaji wazawa. Kwa sababu ya chuki iliyojengeka au iliyojengwa na siasa nyepesi, rushwa na tamaa ya kohodhi ardhi ndiyo maana waovu wanajificha kwa mgongo wa migogoro kati ya wafugaji na wakulima.

Wakulima na wafugaji wa Kilosa ni ndugu. Tujiulize kwa nini tangu Prof. Paramangamba Kabudi kuchuchaguliwa kuwa mbunge hakuna ugomvi?

Tujiulize kwa nini Murad wa Mvomero na siyo Amos Makalla akiwa mbunge lazima kuzuke mgogoro kati ya wafugaji Mvomero? Au yule aliyeondolewa na Kabudi lazima migogoro itokee Kilosa. Hapa naomba tujiongeze tusifarakanishwe na wale ambao hawatutakii mema.

Kubaini ukweli huu Mh. Rais SSH aunde tume ya majaji kubaini kwa upana na marefu mgongano wa wadau mbalimbali (wafufaji, wanasiasa, wakulima, viongozi wa serikali za mitaa na wa serikali kuu, viongozi wa kimila nk) uliopo Kilosa. Aunde tume ya jopo la majiji wanao heshimika. Aunde yeye na siyo ile tume ya Lukuvi. Nasema siyo ya Lukuvi. Lukuvi kwa kificho ana maslahi Mabwegere, asimamishwe kama waziri wa ardhi wakati wa kutafuta ukweli huu, ili kuzuia mgongano wa kimaslahi.

Tume hii ikiundwa itaweza kuishauri serikali vizuri sana. Lakini kikubwa kuliko yote wakulima na wafugaji ni ndugu na huu undugu ulishamiri vizuri sana kipindi cha Hayati Magufuli. Mungu amurehemu.

Siku moja Hayati Magufuli akitokea Morogoro kuelekea ziarani Kilosa alitamka njiani kuwa..."na ya jua mengi ambayo...hata wewe waziri wa ardhi, mkurungezi na DC hamkutakiwa kuwa hapo mplipo....". Kiashiria kuwa nyuma ya pazia pamejificha jambo.

Kilosa ni bonde nzuri la mpunga. Kilosa ni ardhi nzuri ya ufugaji. Kilosa ina misitu mizuri ya asili. Kilosa ina mbuga nzuri ya wanyama ya Mikumi. Kilosa inahitaji jina nzuri. Iundwe tume ya majaji ili kubaini ukweli. Hii tume itasaidia watu kuishi uhalisia na kuacha kuishi kwa hisia. Kilosa ni salama. Kilosa tunapendana. Kilosa ni jina lenye manukato. Karibu kilosa ya watanzania!
 
Mleta mada anasema ukweli...pale mbigiri wafugaji wanatawala...wakute pale lotus bar wanavojimwambafai
 
Ndugu andiko lako hata kama lina ukweli basi limeambatana na chuki.
Sheria ni msumeno kwa nini useme mipaka itambuliwe lakini kwenye mashamba asiguse??? Hapo ndipo penye chuki.
Kumbuka hawa ma DC wanafanya kazi chini ya timu za wataalamu tena waliobobea katika utatuzi wa migogoro ya Ardhi.
Muhimu Sheria inazingatiwa?
Unachangia usichokielewa,hata bandiko langu hujalielewa. Kama kimya
 
Wale marasta wa mbigiri bado huko!
Walishaondoka nasikia.
Ujue watu wanachangia kishabiki,
Hoja yangu ni kwamba mkuu wa wilaya anataka kunyanganya mashamba ya watu ambao wametoka sehemu mbalimbali ktk mkoa wa morogoro ambayo walipewa na kijiji,wakayasafisha yakiwa na msitu wa kuishi tembo.

Wamelima wengine zaidi ya miaka15, mkuu.
Ikumbukwe hao wa na kijiji walikuwepo na ktk miaka hiyo chaguzi nyingi zilipita na viongozi kubadirika,hapakuwa na malalamiko wala mtu yeyote kudai shamba,wala kauli ya kibaguzi eti wanaolima kule siyo wa na kijiji.
 
Kilosa ni Bonde la Sodoma na Gomora wamejaa wenye tamaa kama Lutu.!
Husipende kutumia mifano kutoka kwenye vitabu vitakatifu, mifano ambayo hata huifahamu vema.Umesoma wapi kwamba Lutu alikuwa mtu mwenye tamaa?.
 
Kilosa haiwezi kutulia kama viongozi wenye uchu wa madaraka wamehozi maeneo makubwa..wakati hawayaendelezi hawa wahujumiwe maeneo yarudishwe kwa wananchi.

#MaendeleoHayanaChama
 
Back
Top Bottom