Dark City
JF-Expert Member
- Oct 18, 2008
- 16,253
- 11,598
Ndugu wana JF,
Katika safari zangu za kutembelea jiji la Tanga, nimekumbana na kitu ambacho sijakielewa kabisa. Nilipokuwa nazunguka mjini leo asubuhi, nimeshangaa kuona maduka yote na sehemu muhimu za huduma kama masoko zikiwa zimefungwa. Nilipouliza nikaambiwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mej Mstaafu Said Kalembo ametoa amri (kupitia barua ambayo sikubahatika kuiona) kwamba sehemu zote hizo zifungwe siku ya leo (16 Aprili 2011) kuanzia asubuhi hadi saa 6.00 mchana ili watu wafanye usafi wa maeneo yao. Hata maduka ya dawa nayo pia yamefungwa.
Naomba wajuzi wa sheria na mambo ya utawala waniambie kama Mkuu wa mkoa anayo mamlaka kama hayo kisheria. Nimeongea na wakili mmoja wa hapa Tanga akanambia kuwa kuna kitu kama by-laws kimetumika ila akakikiri kuwa hajaiona hiyo sheria ndogo wala kupata undani wake. Pia jamaa mmoja aliyekuwa amekwazwa kama mimi kampigia simu mwanasheria wa jiji ambaye kajibu kuwa mkuu wa mkoa ametumia penal code (sina hakika na spellings) au kanuni za adhabu kutoa amri hiyo.
Ndugu zangu nimekwazika sana na hali hii na naomba mnisaidie kwa michango yenu.
DC
Katika safari zangu za kutembelea jiji la Tanga, nimekumbana na kitu ambacho sijakielewa kabisa. Nilipokuwa nazunguka mjini leo asubuhi, nimeshangaa kuona maduka yote na sehemu muhimu za huduma kama masoko zikiwa zimefungwa. Nilipouliza nikaambiwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mej Mstaafu Said Kalembo ametoa amri (kupitia barua ambayo sikubahatika kuiona) kwamba sehemu zote hizo zifungwe siku ya leo (16 Aprili 2011) kuanzia asubuhi hadi saa 6.00 mchana ili watu wafanye usafi wa maeneo yao. Hata maduka ya dawa nayo pia yamefungwa.
Naomba wajuzi wa sheria na mambo ya utawala waniambie kama Mkuu wa mkoa anayo mamlaka kama hayo kisheria. Nimeongea na wakili mmoja wa hapa Tanga akanambia kuwa kuna kitu kama by-laws kimetumika ila akakikiri kuwa hajaiona hiyo sheria ndogo wala kupata undani wake. Pia jamaa mmoja aliyekuwa amekwazwa kama mimi kampigia simu mwanasheria wa jiji ambaye kajibu kuwa mkuu wa mkoa ametumia penal code (sina hakika na spellings) au kanuni za adhabu kutoa amri hiyo.
Ndugu zangu nimekwazika sana na hali hii na naomba mnisaidie kwa michango yenu.
DC