Kamanda Asiyechoka
JF-Expert Member
- Sep 13, 2020
- 3,166
- 4,581
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera ametangaza dau la milioni tano kwa yeyote atakaye fanikisha kupatikana kwa mwanafuunzi wa kidato cha tano Esther Noah Mwanyilu wa shule ya Sekondari ya Pandahill aliyetoweka shuleni Mei 18/2023
Kauli hiyo imekuja siku moja baada ya waziri Mkuu Kasimu Majaliwa kuiagiza ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya kufuatilia sakata la kupotea kwa Mwanafunzi huyo
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Joseph Kusaga amesema juhudi za kumtafuta zinaendelea ikiwa ni pamoja na kuwahoji wale wote aliwataja kwenye ujumbe aliocha kabla ya kuondoka.
Pia soma: Mkuu wa Mkoa Mbeya, Juma Homera: Kama kuna mtu yupo na mwanafunzi wa shule ya Pandahill, Ester Noah Mwanyilu ni vyema akamuachia