Wadau wataka Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Homera aondolewe, yasemekana ni Mshirikina

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,703
218,247
Taarifa zilizoibuliwa leo nje ya Mahakama kutoka kwa Mawakili waliopeleka kesi ya Mkataba mbovu wa Bandari , wamemtaja wazi wazi Mkuu wa Mkoa huo Juma Homera kwamba hafai kuongoza Mkoa wa Mbeya kwa vile anaamini Ushirikina.

Wamesema kitendo cha RC huyo kuwataka machifu na Waganga wa Mbeya kuwaloga Wanasheria wanaosimamia kesi hiyo kinachoenda sambamba na RCO wa Mbeya kuwakamata atakavyo na kuwadhalilisha Wazalendo wote wanaopambania Rasilimali za Nchi hakipaswi kufumbiwa macho maana kinaweza kuleta Maafa.

Wanashangaa kwanini Homera anaachwa pamoja na kwamba ameanza ushirikina siku nyingi tangu akiwa Katavi, ambapo kumbukumbu zinaonyesha kwamba, Wakati wa Ugonjwa wa Korona alikusanya Waganga na Wachawi Ofisini kwake akiwalazimisha watengeneze dawa ya Korona ili yeye apate sifa kutoka kwa Magufuli.

Binafsi kama mtu wa Mbeya naunga mkono RC huyo kung'olewa kwa vile anatia aibu , Mbeya inahitaji RC wa kisasa anayeamini katika Sayansi badala ya uchawi wa kuloga watu , muda wa kuamini uchawi ulishapita na ni Aibu kwa kijana kama Homera kudhani ushirikina utamsaidia chochote.
 
Ninachokijua GENTAMYCINE ni kwamba huyu Homera mnamuonea tu kusema ni Mchawi kwani Mtendaji wake Mwandamizi ( Mkuu ) ni Mchawi na anapenda Ushirikiano kiasi kwamba ilimlazimu hadi awape Yanga SC Waganga zake Watatu waende nao katika Fainali yao ya CAFCC...
Aiseeeee !!!
 
Taarifa zilizoibuliwa leo nje ya Mahakama kutoka kwa Mawakili waliopeleka kesi ya Mkataba mbovu wa Bandari , wamemtaja wazi wazi Mkuu wa Mkoa huo Juma Homera kwamba hafai kuongoza Mkoa wa Mbeya kwa vile anaamini Ushirikina....
Ebu pambaneni mumuondoe Mbowe kwanza kwenye uwenyekiti. Yaani tumezaa watoto, Mbowe Mwenyekiti na Sasa wanaanza kusoma vyuo vikuu, Mbowe bado Mwenyekiti! Huu kama sio ushirikina nini?
 
Ebu pambaneni mumuondoe Mbowe kwanza kwenye uwenyekiti. Yaani tumezaa watoto, Mbowe Mwenyekiti na Sasa wanaanza kusoma vyuo vikuu, Mbowe bado Mwenyekiti! Huu kama sio ushirikina nini?
Nakazia niliyoyasema mahali pengine mara nne sasa. Hoja ya Mbowe kukaa madarakani kwa kipindi kirefu inalenga kutuondoa kwenye hoja ya msingi iliyopo mezani inayohusu mkataba wa bandari. Hizo pilipili za shamba zakuwashia nini mwenzangu? Ulivyoandika ni kwamba wewe, kama nilivyo mimi, si mwanachama wa CHADEMA. Urefu wa kipindi alichokuwa Mbowe madarakani tuwaachie wao. Hoja ya uchawi wa RC wa Mbeya imeletwa kwa makandokando ya kesi inayoendelea kuhusu mkataba wa bandari. Hiyo ndiyo ibakie hoja ya kuzungumzia. Kama nia yako ni kuzungumzia kipindi alichokuwa madarakani Mbowe, anzisha uzi mwingine. Huu wa mada ya mkataba wa bandari usipotoshwe. Isije ikawa umeishiwa hoja za kutetea mkataba na kwa hiyo unaona afadhali upoteze lengo kwa kuleta mada nyingine ili watu wasahau suala zito linaloikabiri Tanzania na kuhamia kwenye suala lako. Wito wangu kwa Watanzania: tuungane sote kukosoa huo mkataba mbaya, bila kujali dini au chama gani cha siasa tunachokubaliana nacho. Nimesema mahali pengine kwamba mimi niko CCM. Lakini ninatofautiana na viongozi wangu wanaokubaliana na mkataba huo. Pindi ikifika kupiga kura, nitapiga kura ya kuwapinga hao, hata kama itabidi nipigie kura upinzani. Nikikariri maneno ya Mwalimu, CCM siyo baba au mama yangu. Napiga kura kufuatana na jinsi ninavyouona ukweli.
 
Nakazia niliyoyasema mahali pengine mara nne sasa. Hoja ya Mbowe kukaa madarakani kwa kipindi kirefu inalenga kutuondoa kwenye hoja ya msingi iliyopo mezani inayohusu mkataba wa bandari. Hizo pilipili za shamba zakuwashia nini mwenzangu? Ulivyoandika ni kwamba wewe, kama nilivyo mimi, si mwanachama wa CHADEMA. Urefu wa kipindi alichokuwa Mbowe madarakani tuwaachie wao. Hoja ya uchawi wa RC wa Mbeya imeletwa kwa makandokando ya kesi inayoendelea kuhusu mkataba wa bandari. Hiyo ndiyo ibakie hoja ya kuzungumzia. Kama nia yako ni kuzungumzia kipindi alichokuwa madarakani Mbowe, anzisha uzi mwingine. Huu wa mada ya mkataba wa bandari usipotoshwe. Isije ikawa umeishiwa hoja za kutetea mkataba na kwa hiyo unaona afadhali upoteze lengo kwa kuleta mada nyingine ili watu wasahau suala zito linaloikabiri Tanzania na kuhamia kwenye suala lako. Wito wangu kwa Watanzania: tuungane sote kukosoa huo mkataba mbaya, bila kujali dini au chama gani cha siasa tunachokubaliana nacho. Nimesema mahali pengine kwamba mimi niko CCM. Lakini ninatofautiana na viongozi wangu wanaokubaliana na mkataba huo. Pindi ikifika kupiga kura, nitapiga kura ya kuwapinga hao, hata kama itabidi nipigie kura upinzani. Nikikariri maneno ya Mwalimu, CCM siyo baba au mama yangu. Napiga kura kufuatana na jinsi ninavyouona ukweli.
Amen
 
Back
Top Bottom