Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro akemea rushwa mahakamani

peno hasegawa

JF-Expert Member
Feb 24, 2016
12,833
21,466
Moshi. Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Nurdin Babu amewataka watumishi, watendaji na wadau wa Mahakama kujiepusha na vitendo vya rushwa na kuweka mifumo mizuri itakayowezesha utatuzi wa migogoro kwa njii ya usuluhishi ili kuondoa mrundikano wa mashauri na kesi mahakamani.

Babu ametoa rai hiyo leo jumatatu Januari 23, 2023 katika viwanja vya Mahakama ya Hakimu mkazi Moshi, wakati akizindua wiki ya Sheria kwa mkoa wa Kilimanjaro ambapo amesema mkoa huo unaongoza kwa kuwa na migogoro mingi hususani ya ardhi.

Amesema utatuzi wa migogoro kwa njia ya usuluhishi kutawezesha upatikanaji wa haki kwa wakati na kupunguza gharama na mrundikano wa kesi mahakamani

“Kauli mbiu yetu ni umuhimu wa utatuzi wa migogoro kwa njia ya usuluhishi katika kukuza uchumi endelevu, wajibu wa mahakama na wadau, kaulimbiu hii ni muhimu sana na kama tutaitumia vizuri, itasaidia kupunguza mrundikano wa kesi na mashauri mahakamani.

“Niombe wadau wa mahakama wanaoshulikia migogoro kuweka mifumo mzuri ili kuhamasisha utatuzi wa migogoro kwa njia ya usuluhshi, kwani hakuna Mkoa una migogoro mingi kama Kilimanharo, na hasa migogoro ya ardhi.

“Lakini pia nitoe rai kwa watumishi na watendajiwa mahakama, kujiepusha na vitendo vya rushwa na ukiukwaji wamaadili na kuachanana ufanyaji kazi wa mazoea, wahudumieni wale wanaohitaji haki kwa weledi,” Babu.
Amewataka wananchi kujitokeza katika wiki ya sheria kufika kupata msaada na ushauri wa kisheria ili kuweza kutatua migogoro inayowakabili kwa njia ya usuluhishi.

Kwa upande wake, Jaji mfawidhi Mahakama Kuu Kanda ya Moshi, Dk Juliana Massabo amesema katika wiki ya sheria watatoa huduma mbalimbali kwa wananchi na watumishi na wadau wa mahakama wamejipanga vizuri kutoa elimu ya sheria, utendaji kazi wa Mahakama na msaada wa kisheria.

“Mahakama imeona ni vyema utatuzi wa migogoro mbalimbali ikatatuliwa kwa njia ya suluhisho, ambayo hutoa fursa ya migogoro kwa haraka na kwa gharama nafuu ikilinganishwa na gharama zinazotumika katika kuendesha kesi mahakamani.

“Na huduma tutakazozitoa katika wiki hii ni kuonyesha wananchi umuhimu wa utatuzi wa migogoro kwa njia ya usuluhishi katika kujenga uchumi endelevu na kila mwananchi atakayefika atapata huduma lakini pia tutatoa elimu mashuleni, vyuoni, masokoni na katika mikusanyiko ya watu,” amesema Jaji Massabo.

Chanzo: Mwananchi
 
Silas Mangi hawezi kuacha Rushwa kwenye mahakama ya Ardhi wilaya ya Moshi.

Huyu mtu amesomea Rushwa.
 
Silas Mangi hawezi kuacha Rushwa kwenye mahakama ya Ardhi wilaya ya Moshi.

Huyu mtu amesomea Rushwa.
Wanajisumbua tangu lini mahakama zetu zinatenda haki?rushwa ktk mahakama zetu ni sehemu ya maisha yao.kuanzia mahakama za mwanzo mpaka mahakama za hakimu mkazi zinanuka rushwa. Wengine tuliishapitia huko tunajua mambo yalivyo. Rushwa nje nje tena wana mawakala wao wa kuchukua rushwa kama ilivyo kwa askari wa barabarani.

Hizo kauli za watendaji wetu hazina afya sababu hazina impact yoyote ile kwa wananchi.si leo wala jana,vyombo vinavyolalamikiwa kwa rushwa ni mahakama,polisi,ardhi,afya nk lkn hatuoni jitihada zozote za kukomesha hali hiyo.

Hiki ni kiashiria cha kuwa hata hao wakemeaji ni sehemu ya mfumo huo.takukuru hawana ubavu wa kupambana na rushwa kwani hata wao ni sehemu ya mfumo huo. Suluhisho pekee ni kuwa na katiba mpya ambayo itawafanya wala rushwa kukaa pembeni.
 
Wanajisumbua tangu lini mahakama zetu zinatenda haki?rushwa ktk mahakama zetu ni sehemu ya maisha yao.kuanzia mahakama za mwanzo mpaka mahakama za hakimu mkazi zinanuka rushwa. Wengine tuliishapitia huko tunajua mambo yalivyo. Rushwa nje nje tena wana mawakala wao wa kuchukua rushwa kama ilivyo kwa askari wa barabarani.

Hizo kauli za watendaji wetu hazina afya sababu hazina impact yoyote ile kwa wananchi.si leo wala jana,vyombo vinavyolalamikiwa kwa rushwa ni mahakama,polisi,ardhi,afya nk lkn hatuoni jitihada zozote za kukomesha hali hiyo.

Hiki ni kiashiria cha kuwa hata hao wakemeaji ni sehemu ya mfumo huo.takukuru hawana ubavu wa kupambana na rushwa kwani hata wao ni sehemu ya mfumo huo. Suluhisho pekee ni kuwa na katiba mpya ambayo itawafanya wala rushwa kukaa pembeni.
Mpaka sasa, kwe ye records, taasisi mbili zinazoongoza kwa rushwa, ni Polisi na Mahakama. Na hawataki kupoteza nafasi yao hiyo ya juu kwenye Taifa hili la rushwa.
 
Mkishindwa kesi, mnasema rushwa, mkishinda mnashangilia na kumuita shujaa.
Silas mangi alisomea wapi uhakimu unasema ukishindwa kesi?
Tena ameajiriwa kwa mkataba, asipokula rushwa Ili aweze kuhonga mkataba utaongezwa?
 
Kwa hiyo mkuu wangu RC rushwa itaisha kwa kukemea kama ulivyofanya!,kuna sehemu hii nchi ilikosea njia kabisa, yaani baada ya kukata kulia, sisi tukaenda kushoto, soma hii; President Nyerere anasoma Uingereza elimu yake ya juu na anarudi Tanzania na kufanikiwa kuwa Rais, President S. Khama naye anamaliza masomo Uingereza na kurudi Botswana na kuwa Rais (wote hawa wametoka kwenye koo za kichifu), Botswana wanapiga vita rushwa kitaalamu, Tanzania tunapiga rushwa kwa vitisho, matokeo yake rushwa inatamalaki nchini na Botswana inakua almost a corruption free country, hadi leo rushwa ndani ya Botswana ni adimu mno, my RC rushwa mkoani mwako inahitaji science sio mabavu kuishinda.
 
Back
Top Bottom