Mohamedi Mtoi
R I P
- Dec 11, 2010
- 3,321
- 6,331
Wakuu.
Leo unafanyika mkutano mkubwa wa hadhara kanda ya Serengeti hapa jimbo la Kahama. Ni mkutano ulioandaliwa na kanda ya Serengeti kabla ya kikao cha kamati tendaji ya kanda.
Kanda hii inaundwa na mikoa ya Mara, shinyanga na mkoa mpya wa simiyu.
Hoja zilizozungumzwa na Mwenyekiti Mbowe:-
1. Tutafanya mabadiliko ya mfumo wa utawala uliopo na kutekeleza mfumo wa Majimbo/Kanda kwa mujibu wa sera ya Chadema. Wananchi watakuwa na sauti kwenye mfumo wa uongozi na matumizi ya rasilimali zao.
2. Mamlaka ya Rais ya uteuzi wa nafasi mbalimbali yatapunguzwa kuliko ilivyo sasa
3. Mfumo wa kuandikisha wapiga kura kwa BVR hauwezi kutekelezwa kwa ukamilifu wake na kutumika kwenye kura ya maoni, nguvu kubwa ipelekwe kuandaa uchaguzi mkuu.
4. Katiba ya sasa na hata Katiba inayopendekezwa zote hatuzikubali. Madai ya Katiba mpya yapo palepale.
5. Wananchi wajitokeze kwa wingi kujiandikisha kwa ajili ya uchaguzi mkuu.
6. Marehemu na waathirika wa mvua ya mawe Kahama walifanyiwa dua maalum ya kiislam na kikristo uwanjani pamoja na sadaka kutolewa na wanachama.
7. Chadema itachangia mabati ya Tshs Mil. 10 kwa ajili ya waathirika wa mvua ya mawe.
Mwisho; Baada ya mkutano maelfu ya wananchi walimsindikiza Mwenyekiti Mbowe mpaka hotelini alikoshukia kwa ajili ya mapumziko mafupi kabla ya kushiriki vikao viwili vikubwa "Kamati Tendaji ya Kanda ya Ziwa Mashariki 'Serengeti' na Baraza la Uongozi la Kanda"
Leo unafanyika mkutano mkubwa wa hadhara kanda ya Serengeti hapa jimbo la Kahama. Ni mkutano ulioandaliwa na kanda ya Serengeti kabla ya kikao cha kamati tendaji ya kanda.
Kanda hii inaundwa na mikoa ya Mara, shinyanga na mkoa mpya wa simiyu.
Hoja zilizozungumzwa na Mwenyekiti Mbowe:-
1. Tutafanya mabadiliko ya mfumo wa utawala uliopo na kutekeleza mfumo wa Majimbo/Kanda kwa mujibu wa sera ya Chadema. Wananchi watakuwa na sauti kwenye mfumo wa uongozi na matumizi ya rasilimali zao.
2. Mamlaka ya Rais ya uteuzi wa nafasi mbalimbali yatapunguzwa kuliko ilivyo sasa
3. Mfumo wa kuandikisha wapiga kura kwa BVR hauwezi kutekelezwa kwa ukamilifu wake na kutumika kwenye kura ya maoni, nguvu kubwa ipelekwe kuandaa uchaguzi mkuu.
4. Katiba ya sasa na hata Katiba inayopendekezwa zote hatuzikubali. Madai ya Katiba mpya yapo palepale.
5. Wananchi wajitokeze kwa wingi kujiandikisha kwa ajili ya uchaguzi mkuu.
6. Marehemu na waathirika wa mvua ya mawe Kahama walifanyiwa dua maalum ya kiislam na kikristo uwanjani pamoja na sadaka kutolewa na wanachama.
7. Chadema itachangia mabati ya Tshs Mil. 10 kwa ajili ya waathirika wa mvua ya mawe.
Mwisho; Baada ya mkutano maelfu ya wananchi walimsindikiza Mwenyekiti Mbowe mpaka hotelini alikoshukia kwa ajili ya mapumziko mafupi kabla ya kushiriki vikao viwili vikubwa "Kamati Tendaji ya Kanda ya Ziwa Mashariki 'Serengeti' na Baraza la Uongozi la Kanda"