Mkutano wa CHADEMA Sombetini

Mkutano wa CHADEMA Sombetini

Mazungumzo yanasitishwa kwa muda kupisha swala ya kiislamu
 
nimemukubali sana baba bony kwa maneno mazuri kwa wanaarusha.. cdm wanasema ni ya wakristo mbna bendera yao haina msalaba? kama ni ya wakirstu kwann kimempitisha ally kuwa mgombea wa sombetin? kama ni cha wakristo mbna hakibatizi wanachama wake? kwa kwel baba bony amefunguka vzr sana
 
Kamanda Bush, anasema serikali ya ccm mawaziri wenyewe wameshindwa kazi kila mara kikwete kufukuza na kubadilisha ngoma ile ile sasa kama mawaziri wameshindwa diwani anakwenda kufanya nini?
chadema ushindi ni wa kwetu.

kichekesho Bush akisema CCM!!!!! Watu wanaitikia Namba ya Kiatuuuuu!!!!

Akisema CUF!!!! Watu wanaitikia namba ya yeboyeboooo!!!!
 
Msoffe,
Anasema Bananga ni jembe, pamoja na kuwa Sombetini hakuna diwani lakini tulikuwa tunaitumikia Sombetini kama vile kuna diwani.... hii yote ni kazi ya chadema......
Ubovu wa barabara za sombetini ni mbovu kutokana na uhuni wa serikali ya ccm, hivyo tunamhitaji Bananga akasimamie miradi ya maendeleo sombetini......... anasema Barabara zote mjini zinaitwa Lema road kwasababu ya usimamizi mzuri
 
DSC07354.JPG DSC07354.JPG chadema kazini
 
cdm juu, CUF namba ya yeboyebo, CCM namba ya viatu hayo ni maneno ya kamanda Bush wa sokon one..
 
Tunamuomba MUNGU awape wanadamu utu wasije wakaendeleza tabia ya kurusha mabomu tena kama walivyofanya mwaka jana 2013.
 
Mwenyekiti wa Wilaya Diwani wa Levolosi Kamanda Ephata Nanyaro anasema hatuendi kumtafutia Bananga ulaji, na sisi kama chadema siyo waheshimiwa, bali watumishi wa wananchi, na safari hii tumejiandaa kwa namna yoyote na kama ni noma na iwe noma, titahakikisha tunalindana wenyewe...... wamezoea kupiga mabomu kwenye mikutano yetu, wamezoea kuua watu wetu, awamu hii tumejiandaa
 
Nanyaro anasema tutahakikisha kikao cha bajeti kwenye baraza la halmashauri kabla ya uchaguzi wa sombetini. baada ya bananga kuingia kwenye baraza la madiwani chadema wataongoza kamati zote na maendeleo lazima yaje kwa kasi
 
Kamanda Alfonce Mawazo anasema ukiitwa mheshimiwa ni title kubwa sana, manake kila kitu chake, na kuanzia leo amemwachia Bananga uheshimiwa. cha pili nimemwachia posho, mimi siyo mheshimiwa tena....... na uheshimiwa huu una maana ya kuwatumikia wananchi wa sombetini, siyo uheshimiwa wa kujiona mkubwa kuliko wengine. jambo la muhimu nakuachia mpenzi wangu wa kweli na wa pekee duniani ambaye ni kata ya Sombetini, na nakuomba umlee vizuri
 
Tunamuomba MUNGU awape wanadamu utu wasije wakaendeleza tabia ya kurusha mabomu tena kama walivyofanya mwaka jana 2013.

Tunashukuru Mungu sasa hivi Miwigulu kawa waziri, sijui mkitupa mabomu kwenye mikutano yenu mtamsingizia nani tena.
 
Huku kata ya kiboriloni moshi mgombea wa cdm ameambiwa akalale wakutane ukumbi wa manispaa siku ya kuapishwa kwake.
 
Wakuu,
Mkutano wa kampeni wa chadema sombetini ndiyo umefunguliwa rasmi na Mwenyekiti wa Kata ya Sombetini Kamanda Madava ndiyo amefungua rasmi, lakini amegusia suala la utulivu, kwamba tunaombe tuwe watulivu kwa kipindi hiki cha kampeni, tuwe wapole, wavumilivu, lakini tusiwe wanyonge. Amesema tusimguse wala kumchokoza mtu, lakini tukiguswa tusimwache....

Diwani wa Ngarenaro Doita anawasalimia wananchi, anasema maendeleo yanayoonekana Arusha ni kwasababu ya chadema, wakati hatupo hawakuthubutu, lakini tulipoingia tukikohoa wanafanya..... chezea chadema.
.............................................

CDM NI FUNIKO ILE MBAYA HAPA TOWN,RAHA TUNAJIPA WENYEWE magamba kwish nei.
 
Mawazo;
pamoja na matatizo yote niliyowahi kupata, nakiri kuwa kama kuna wakati naona kuna raha ni wakati huu wa kupigania ukombozi wa watu maskini.......
 
Back
Top Bottom